BAKIIF Islamic
JF-Expert Member
- Jul 11, 2021
- 600
- 1,843
Utakapokufa katu hutoweza kurudi tena duniani.
Ukweli ni kwamba watu wengi wanaogopa kufa, ijapokuwa wapo ambao inafikia hatua hawaogopi kifo kabisa, lakini pia inaweza kufikia hatua kwa baadhi ya watu mpaka wakakiomba kifo. Hii huwenda ni kutokana na shida na taabu walizo nazo. Lakini katika uislamu IMEKATAZWA KATU KUTAMANI KIFO.
Mtume (s.a.w) amesema: “Asitamani mmoja wenu MautI (kifo) ima akiwa ni mwema kwani huenda akazidisha heri ama akiwa ni muovu huenda akatubia.
Mtume wa Allah ametukataza tusitamani kufa yaani mauti.
Tusitamani kufa kwa hali zozote tulizo nazo tukiwa ni wachamungu sana ama tukiwa ni waovu sanaa.
Ukiwa mchamungu uhai wako unaweza kuutumia vyema na ukazidisha uchamungu hivyo ukapandisha daraja yako kwa Allah
Ukiwa ni muovu unaweza kutumia fursa ya uhai uliyonayo na ukatubu na Allah akakusamehe na ukaweza kuipata pepo. Kwani Allah husamehe madhambi yote pindi mja akitumia toba ya kweli.
Uhai ni wa thamani pindi tu ukiukosa hutoweza kufanya jambo lolote tena.
Mtume s.a.w amesema “asitamani mmoja wenu mauti na wala asiyaombe mauti kabla hayajamjia kwani hakika pindi atakapokufa, amali zake zote zinakatika, na kwa hakika hautamzidishia muumini umri wake isipokuwa heri”.
Tusitamani kufa na si kutamani tu bali hata tusithubutu kufa, kwani kama tutapewa uhai zaidi na tukiwa wema huenda uhai wetu ukawa ni chachu ya sisi kuzidisha wema. Na kama tukiwa ni waovu huenda tukatubu.
Mtu akifa amali zake zote zinakatika. Yaani kama ni muovu na hajatubia madhambi yake kwa Allah basi hatoweza tena kutubia, na kama ni mwema hatoweza kufanya tena mambo mema.
”Atakapokufa mwanadamu amali zake zote (matendo) hukatika isipokuwa matendo ya (amali) aina tatu SADAKA YENYE KUENDELEA, ELIMU YENYE KUPATISHA MANUFAA AU MTOTO MWEMA ATAKAYEMUOMBEA DUA”. Haya ni katika matendo ambayo yataweza kutupatisha faida pindi tutakapo fariki.
P.O.BOX 55185
Kimara Korogwe,
KAM College Road, Kivulini Street
House no 36
Phone +255 755 351 262
Ukweli ni kwamba watu wengi wanaogopa kufa, ijapokuwa wapo ambao inafikia hatua hawaogopi kifo kabisa, lakini pia inaweza kufikia hatua kwa baadhi ya watu mpaka wakakiomba kifo. Hii huwenda ni kutokana na shida na taabu walizo nazo. Lakini katika uislamu IMEKATAZWA KATU KUTAMANI KIFO.
Mtume (s.a.w) amesema: “Asitamani mmoja wenu MautI (kifo) ima akiwa ni mwema kwani huenda akazidisha heri ama akiwa ni muovu huenda akatubia.
Mtume wa Allah ametukataza tusitamani kufa yaani mauti.
Tusitamani kufa kwa hali zozote tulizo nazo tukiwa ni wachamungu sana ama tukiwa ni waovu sanaa.
Ukiwa mchamungu uhai wako unaweza kuutumia vyema na ukazidisha uchamungu hivyo ukapandisha daraja yako kwa Allah
Ukiwa ni muovu unaweza kutumia fursa ya uhai uliyonayo na ukatubu na Allah akakusamehe na ukaweza kuipata pepo. Kwani Allah husamehe madhambi yote pindi mja akitumia toba ya kweli.
Uhai ni wa thamani pindi tu ukiukosa hutoweza kufanya jambo lolote tena.
Mtume s.a.w amesema “asitamani mmoja wenu mauti na wala asiyaombe mauti kabla hayajamjia kwani hakika pindi atakapokufa, amali zake zote zinakatika, na kwa hakika hautamzidishia muumini umri wake isipokuwa heri”.
Tusitamani kufa na si kutamani tu bali hata tusithubutu kufa, kwani kama tutapewa uhai zaidi na tukiwa wema huenda uhai wetu ukawa ni chachu ya sisi kuzidisha wema. Na kama tukiwa ni waovu huenda tukatubu.
Mtu akifa amali zake zote zinakatika. Yaani kama ni muovu na hajatubia madhambi yake kwa Allah basi hatoweza tena kutubia, na kama ni mwema hatoweza kufanya tena mambo mema.
”Atakapokufa mwanadamu amali zake zote (matendo) hukatika isipokuwa matendo ya (amali) aina tatu SADAKA YENYE KUENDELEA, ELIMU YENYE KUPATISHA MANUFAA AU MTOTO MWEMA ATAKAYEMUOMBEA DUA”. Haya ni katika matendo ambayo yataweza kutupatisha faida pindi tutakapo fariki.
BAKIIF ISLAMICP.O.BOX 55185
Kimara Korogwe,
KAM College Road, Kivulini Street
House no 36
Phone +255 755 351 262