KERO Kigamboni: Barabara ya Dege kwenda Mkwajuni mpaka kwenye Machimbo ya Vifusi ni mbovu kuliko maelezo

KERO Kigamboni: Barabara ya Dege kwenda Mkwajuni mpaka kwenye Machimbo ya Vifusi ni mbovu kuliko maelezo

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
Mimi ni Mkazi wa Mbutu Kigamboni kwa namba ya Wanambutu.

Changamoto ya Mbutu ni Barabara ya kutoka Dege kwenda Mkwajuni mpaka kwenye Machimbo ya Vifusi.

Kwanza naomba niwafahamishe yafuatayo;

1. Barabara zote za Kigamboni zitakazojengwa material yake nikimaanisha kifusi chake kitatoka Mbutu kupitia Kwa Malale hiyo njia ya
2. SJR material yalitoka hapo.
3. Daraja la Tanzanite na yametoka kwetu.
4. Barabara ya kimbiji material yametoka kwetu Mbutu.
5. Viwanda vya cement vinachukua materia kwetu.
6. Barabara zote na madaraja yaliyoharibiwa na hizi mvua wanategemea kifusi kutoka Mbutu.

Jambo la kushangaza, sisi ndio tuna Barabara mbovu kupindukia. Jamani tunajiona kama hatuna mwakilishi wa kutusemea. Tumetelekezwa Magari ya kifusi usiku kucha yanaharibu Barabara na kutucha na mavumbi tupu mvua zikikatika.

Viongozi wanaohusika waone na wasikie kilio chetu.
 
Uko yupo Yericko Nyerere, yeye yuko bize kutaka Yanga wapokonywe point, shida za msingi za anapoishi hana habari nazo, jinga kabisa.
 
na wanaendelea kula mwamba bahari siku hard table itapocheka sasa. tuttatafutana
 
Magari ya kubeba material za ujenzi yanaharibu sana barabara.
 
Back
Top Bottom