Kigamboni planning authority

Kigamboni planning authority

Tuna matatizo makubwa Bandari ya Tanga imekufa hivi hivi tunaona leo hii unajenga lingine kwa mwenye akili ni vigumu kuona mantiki ya uamauzi huu!

Mie si Mchumi wana uchumi watatupa mwanga wa kipi hasa is Economicaly viable!

Kigamboni Blue Diamond haizungumzwi tena ,na mwelekeo ni Bagamoyo kwa sasa!



Tega siko pengine Mhe.Tibaijuka naye anavijisenti vya kuwalipa wale wa Kibada!




Bagamoyo mpya mbioni




Aliongeza kuwa kwa mwaka huu wa fedha, Serikali imetenga Sh7 bilioni kwa ajili ya kumalizia ulipaji fidia katika eneo la Bagamoyo.

Alifafanua kwamba mwaka 2013/14, kampuni 31 zilipewa leseni za kujenga viwanda chini ya Mamlaka ya EPZ na tayari kampuni nane zimeanza uzalishaji. Kampuni hizo zinatarajiwa kuwekeza mtaji wa jumla ya Dola za Marekani 485 milioni na kuajiri watu 10,276.
 
Leo nimewasikia waziri mkuu na waziri wake wa ardhi akipiga propaganda pale Bungeni,hivi hawa watu wa Kigamboni mnataka wawe wezi au panya road ndio muwapige risasi !! Mpaka sasa mnajua wanaishije wao na familia zao ikiwa sasa ni mwaka wa sita tangu wazuiwe kufanya shuhuli yoyote ktk maeneo yao ?kuna maneno yanasemwa mtaani itabidi tuyaamini sasa kuwa Kigamboni ilishauzwa kwa George Bush ili awekeze na fedha zote alishatoa serikali imezitafuna kupitia CCM.
 
Leo nimewasikia waziri mkuu na waziri wake wa ardhi akipiga propaganda pale Bungeni,hivi hawa watu wa Kigamboni mnataka wawe wezi au panya road ndio muwapige risasi !! Mpaka sasa mnajua wanaishije wao na familia zao ikiwa sasa ni mwaka wa sita tangu wazuiwe kufanya shuhuli yoyote ktk maeneo yao ?kuna maneno yanasemwa mtaani itabidi tuyaamini sasa kuwa Kigamboni ilishauzwa kwa George Bush ili awekeze na fedha zote alishatoa serikali imezitafuna kupitia CCM.


Ujue inachosha zaidi na kuumiza unaposikia porojo ile ile kiwa wakati tena kwa watu waliopewa dhamana kubwa!

Mhe. Anna Tibaijuka anafahamu vizuri hoja za Wanakigamboni kwa Undani Kabisa na Hata Ikulu ina Nakala za kutosha kuhusu hoja za Wakaazi wa Kigamboni.

Mhe.Waziri amekutana na Kamati ya Wakaazi Wakigamboni Bungeni na pia aliahidi kufanya nayo Kazi katika Mkutano wake uliofanyika Uwanja wa Machava.

Leo hii kutamka maneo kama haya kwanza ni madharau makubwa kwa mtu mwenye akili timamu


Prof Tibaijuka asalimu amri Kigamboni

Akijibu hoja hizo, Profesa Tibaijuka alisema kuanzia sasa atakuwa karibu na Ndungulile na wakazi wa Kigamboni ili waweze kufahamu kila kitu kinachoendelea.

Naomba kumkumbusha Mhe.Waziri kuwa suala hapa si wnanchi kufahamu kinachoendelea issue hapa ni wewe na Wizara yako kuwasikilizwa kwanza Wananchi wa Kigamboni na hoja zao
Naomba kukumbusha kuwa hoja zao tayari unazo mezani au kafungue makabati ya Wizarani kwako .

Wizara yako inafahamu kuwa zoezi hili la Mjimpya wa Kigamboni haijafuata Sheria ila mmeweka pamba masikioni na ndiyo maana muda wote kelele za Mbunge na wananchi imeonekana wimbo wa Mlevi.


Utasema na hili hukulijua ?
Mpaka Gazeti hili imefungwa na inawezekana ilikuwa inaelekea kugusa masilahi mapana ya wanufaikaji watarajiwa wa mradi huu.


Tibaijuka anatumika kuhalalisha uporaji ardhi Kigamboni | Gazeti la ...


Nakala za barua za kamati zilizotumwa wizarani kuomba kushirikishwa zipo, na majibu ya wizara yaliyotumwa kwa lazima baada ya Rutabanzibwa kuwaamuru watendaji wake wajibu yapo. Sasa huko ndiko kushirikishwa nyumba kwa nyumba, mtaa kwa mtaa na kata kwa kata?

Ni vizuri kwa hadhi yako ukafika mahali usidhalilike zaidi kwa usichoweza kukibadilisha ni vizuri ukafanya maamuzi ya Busara!
 
Kuna haja ya kuendesha maisha kiuhalisi kidogo hata kama tunatamani kuishi kama wenzetu huko Ulaya au Dunia ni nyingine.Tukiende taratibu tutafika salama zaidi.

Tamaa zetu au ndoto binafsi zisichukua nafasi kwenye shughuli ya Jamii maana waathirika wa maamuzi yetu watakuwa wengi na itakuwa vigumu kwao kumsamehe atakaye waumiza katika maisha yao na hiyo haitoshi muda mwingine hatua kama hizo huleta vurugu kwenye jamii

Kuna mambo hayako sawa katika utendaji wa Serikali!

Ebu tujikumbushe na hizi kauli mbili ya watendaji wa Serikali.

Waziri Mkuu analiarifu Bunge kusitisha zoezi husika Miezi Mitatu baadaye Waziri husika anaendelea na zoezi lileli .Sasa sijui kama Serikalini ndiyo namna ya utendaji Kazi na uwajibikaji labda wataalamu au wenye uzoefu watasaidia kufafanua.


Tanzania: Minister Trumps Fairness in Land Allocation in Dar

19 August 2014

Tanzania: Minister Trumps Fairness in Land Allocation in Dar
Summary NEPOTISM will not be entertained in the land allocation programme as the allotment will be carried out in transparency, the Minister for Lands, Housing and Human Settlements, Prof Anna Tibaijuka, has stated. "Yono Auction Mart won the tender to allocate the lands to Kigamboni and Kurasini following the announcement by the ministry," she said adding; "Residents should not listen to propaganda from people who have been discouraging others from buying shares." Prof Tibaijuka said when completed, the Kigamboni project would tremendously benefit people who reside in the area and that the government was seeking the fund for the project.


VS

Govt suspends plans on Kigamboni satellite city - IPP Media
By Felix Andrew

30th May 2014

Kigamboni Satelite city
Prime Minister Mizengo Pinda told the August House here on Wednesday evening that the process will resume after issued that have to do with involvement of the key stakeholders, including the residents in the area and leaders of Temeke Municipality have been solved.

Pinda was contributing to the budget estimate debate for the Ministry of Lands, Housing and Human Settlement Development which was tabled on Tuesday.

The Premier said there was a need to look again into the whole process of establishing Kigamboni satellite city in order to enable it to be implemented well.

"Let us take this issue and involve a wider section of the people like the councilors and other stakeholders so that they become aware of the entire process," he said.




Kingine la kushutua zaidi hivi ni Makampuni mangapi yaliomba Tenda hii na lini ilitamngwazwa na je wahusika/wadau walishiriki?





Prof Anna Tibaijuka, has stated. "Yono Auction Mart won the tender to allocate the lands to Kigamboni and Kurasini following the announcement by the ministry," she said adding;



Pengine ni muda muafaka sasa kwa serikali kwenda Angola kujionea namna wenzetu walivyofanya na mikwamo waliyopata kwa miradi kama hii.

Lakini huko nako ni mbali tunaweza kutumia NSSF maana imekuwa na miradi mingi ya ujenzi wa Nyumba na ambazo kumekuwa na malalamiko ya Bei na hii ni kiashiria tosha ya kuhofu uhalisia wa miradi kama hizi.



Nyumba za NHC na NSSF Kigamboni, Dar Es Salaam
"Hivi karibuni kumekuwa na malalamiko toka kwa wananchi kuwa nyumba za bei nafuu (affordable houses) bado si rahisi kwa mwananchi wa kipato cha kati na chini. Bei ya nyumba mpya za NHC hivi karibuni zimekuwa ni zaidi ya TSh 100 millioni kila moja. Bei hii inalalamikiwa kuwa ni kubwa sana kwa mlalahoi".


Naamini hatutofautiani sana na Angola kwa vipato,hivyo suala la wenyeji kutokumudu gharama za nyumba hizo bado ni tatizo halisi na mwisho wa siku ni dhuluma tu ndiyo yenye kuchukua Mkondo wake.

Photos Of A Massive Chinese-Built Ghost Town In Angola ...

But the apartments in the complex cost somewhere between $120,000 and $200,000 according to online advertisements cited by BBC. Other anecdotal reports put the price of 3-bedroom apartment at about $250,000 (2012)




Miaka miwili baadaye hali imebadilika,hivyo ni lazima tufike mahali kipaumbele zetu ziendane na hali halisi ya maendeleo yetu kwa wakati tuliopo na hivyo ndivyo tunavyoweza kujiepusha na Mafisadi wa maendeleo.(Wenye pesa kutumia nafasi ya Umaskini wetu wa Kiuwezo na si Umaskini wa Mali,maana ni wazi kuwa tunazo mali nyingi za kutosha na sizizooza.



Wednesday, April 2, 2014

Chinese-Built Angolan "Ghost Town" Wakes Up?


Until recently. Or so it seems. According to the official Angolan news agency, some 40,000 people moved into Kilamba after their families took advantage of long-term, low-cost mortgages to buy flats with prices ranging from US$70,000 to US$140,000. One account said people are standing in line for days to buy one (photo left).
The news stories on Kilamba, the "ghost town" mainly date from 2012.
 
Haya Kigamboni mjionee usanii wa Wajumbe wa Bunge Maalum ya CCM c/o Chenge na mwenzake Sita.


Katiba pendekezwa;
[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] Fidia
[/TD]
[TD="width: 314"] 25. Bila kuathiri masharti ya Ibara ya 47(2), Serikali itaweka utaratibu wa kisheria kwa ajili ya malipo ya fidia stahiki endapo eneo au sehemu ya ardhi itachukuliwa kwa matumizi ya maendeleo ya kiuchumi na ya kijamii.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Eti fidia stahiki,masihara gani haya?

Nasikitika kuwaona akina mama wengi wanapiga vigelegele kama vile tuko kwenye kuozesha binti,lakini hawachukui kujisomea maeneo muhimu na ya msingi ndani Katiba pendekezwa.

Hakuna nia njema katika Katiba pendekezwa maeneo mengi yamewekwa kihasara hasara kwa faidaa ya wachache.
Nilitegemea maneno yaliyonyooka yaani;

Fidia kulingana na thamani ya soko ya wakati husika
endapo eneo au sehemu ya ardhi itachukuliwa kwa matumizi ya maendeleo ya kiuchumi na ya kijamii.

Dr Ndugulile upo ?
 
Back
Top Bottom