the guardian 17
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 395
- 570
KIGOMA: MAMA lishe na walengwa wa kusaidia kaya masikini Manispaa ya Kigoma Ujiji wanatarajia kunufaika na ugawaji wa majiko banifu yaliyogaiwa na Mamlaka ya Nishati Vijijini (REA) kuhamasisha matumizi ya nishati safi na utunzaji mazingira
Makundi hayo yatanufaika na ruzuku ya 80% ya majiko banifu 200,000 ambapo badala ya kununua jiko moja Sh 55,000 watapata ruzuku ya serikali kwa kununua jiko moja 10,000.
Joseph Sambali mtaalam wa nishati na masuala ya jinsia kutoka Wakala wa Nishati Vijiji (REA) anaeleza.
Akizungumza leo Machi 7, 2025, katika hafla ya kugawa bure majiko 400 kwa mama lishe na walengwa wa kusaidia kaya masikini (TASAF), Joseph Sambali amesema hatua hiyo ni uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi katika kutekeleza mpango wa serikali wa asilimia 90 ya watanzania kutumia nishati safi ifikapo 2034.
Ametaja vipaumbele wa wanufaika kuwa ni makundi maalum hasa vijijini ambako matumizi ya kuni na mkaa ni makubwa.
Makundi hayo yatanufaika na ruzuku ya 80% ya majiko banifu 200,000 ambapo badala ya kununua jiko moja Sh 55,000 watapata ruzuku ya serikali kwa kununua jiko moja 10,000.
Joseph Sambali mtaalam wa nishati na masuala ya jinsia kutoka Wakala wa Nishati Vijiji (REA) anaeleza.
Akizungumza leo Machi 7, 2025, katika hafla ya kugawa bure majiko 400 kwa mama lishe na walengwa wa kusaidia kaya masikini (TASAF), Joseph Sambali amesema hatua hiyo ni uhamasishaji wa matumizi ya nishati safi katika kutekeleza mpango wa serikali wa asilimia 90 ya watanzania kutumia nishati safi ifikapo 2034.
Ametaja vipaumbele wa wanufaika kuwa ni makundi maalum hasa vijijini ambako matumizi ya kuni na mkaa ni makubwa.