Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
WanaJF,
Mada hii itakuwa na 'Updates' za Matukio kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Urais, Ubunge na Udiwani 2025 kama yanavyotujia kutoka kwenu kutoka mkoa wa Kigoma. Ukiwa na taarifa yoyote ambayo ni ya eneo hili tafadhali usisite kuweka.Kigoma ni mkoa uliopo magharibi mwa Tanzania, ukipakana na nchi za Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kwa upande wa magharibi na kaskazini. Mkoa huu unajulikana kwa ziwa la Tanganyika, ambalo ni moja ya maziwa marefu zaidi duniani.
MUHTASARI WA MAENEO YA UTAWALA, MKOA WA KIGOMA
Katika muhtasari wa maeneo ya utawala, mkoa huu una halmashauri ambazo zimegawanyika katika mamlaka za miji na wilaya.
Idadi ya Watu
Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022 yanaonesha kuwa idadi ya watu katika Mkoa wa Kigoma ni 2,470,967; wanaume 1,186,833 na wanawake 1,284,134, ikiwa na wilaya 5.
Idadi ya Majimbo ya Mkoa wa Kigoma
Mkoa wa Kigoma una majimbo Nane ya uchaguzi
- Jimbo la Buyungu
- Jimbo la Kasulu Mjini
- Jimbo la Kasulu Vijijini
- Jimbo la Kigoma Kaskazini
- Jimbo la Kigoma Kusini
- Jimbo la Kigoma Mjini
- Jimbo la Buhigwe
- Jimbo la Muhambwe
Katika uchaguzi mkuu wa 2020 mkoani Kigoma, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilishinda kwa kiwango kikubwa katika ngazi zote.
Kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Hayati John Magufuli alipata kura nyingi katika mkoa huu kwenye nafasi ya urais, akipata zaidi ya asilimia 80 ya kura zilizopigwa.
Katika nafasi za ubunge, wagombea wa CCM walishinda viti vyote vya majimbo, huku ACT Wazalendo ikipoteza ngome jimbo la Kigoma mjini.
Aidha, kwenye udiwani, CCM ilijinyakulia kata takriban zote kutokana na upinzani kukumbwa na changamoto nyingi, zikiwemo wagombea wao kuenguliwa kutokana na matatizo ya kisheria au kutokidhi vigezo
Updates
January
- Pre GE2025 - Waziri Kivuli wa ACT Wazalendo Ndolezi Petro atangaza nia ya kugombea Ubunge jimbo la Kigoma Kusini
- Pre GE2025 - Waziri Kivuli wa ACT Wazalendo Ndolezi Petro atangaza nia ya kugombea Ubunge jimbo la Kigoma Kusini
- Pre GE2025 - Baba Levo: Nikipewa kadi ya CCM kwenye mkutano mkuu, nitamrudishia Zitto Kabwe kadi yake ya ACT
- Pre GE2025 - Zitto: Serikali inaweka vizingiti katika Kesi za Uchaguzi
- LGE2024 - Matokeo ya uchaguzi mtaa wa Geza Ulole, Kigoma yabatilishwa
- Pre GE2025 - Madiwani Kigoma ujiji walalama miradi ya maendeleo kukwama hivyo kuonekana hawajatimiza wajibu wao, waishutumu TAMISEMI wakitaka uchunguzi ufanyike
- Pre GE2025 - Tunataka uchunguzi haraka kutekwa kwa raia wawili Kigoma na Dar es salaam na uzembe wa jeshi la polisi
- Pre GE2025 - Mbunge Samizi na kamati ya siasa yaendelea na ziara kata kwa kata
- Pre GE2025 - Kigoma: Wana CCM kwenye jimbo la Muhambwe wafurahishwa na kitendo cha Rais Samia kupitishwa kama Mgombea Urais
- Pre GE2025 - Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango amewataka wananchi mkoani Kigoma kuutambua na kuuthamini mchango wa Serikali katika maendeleo ya huduma za kijamii
- Pre GE2025 - Kigoma kuuziwa majiko banifu ya ruzuku kwa Tsh. 10,000