Kigoma: Nyumba 10 zimebomoka kutokana na mvua Kasulu

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Zaidi ya nyumba 10 katika mtaa wa mkombozi kata ya murusi halmashauri ya Mji Kasulu Mkoani Kigoma zimebomoka na nyingine kuezuliwa na mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali kunyesha oktoba 29 mwaka huu.
Baadhi ya wananchi wa mtaa wa mkombozi wakieleza namna walivyoshuhudia upepo mkali na kuasababisha madhara hayo ambayo yamesababisha baadhi ya wananchi hao kukosa makazi yakuishi. Timotheo Maliatabu, Selina Kahendabia , Josephati Leonard na Zelda James ni baadhi ya wahanga wa mvua hiyo.
Afisa mtendaji wa kata ya Murusi Omary Sebabili amezulu katika maeneo yaliyoathiriwa na mvua hizo ili kuona uwezokano wa kutoa msaada wa awali kwa wahanga waliokubwa na kadhia hiyo.
Mbali na nyumba hizo kubomoka pia baadhi ya nyumba zilizojaa maji ambapo afisa afya, mazingira na mkuu wa kitengo cha udhibiti wa taka halmashauri ya Mji Kasulu Msafiri Charles ameeleza madhara ya kiafya yanayoweza kujitokeza.
 

Attachments

  • 1733119428362.png
    1.2 MB · Views: 12
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…