Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,681
- 8,887
Leo Rais wa Burundi, Evarist Nditiye amewasili nchini kwa ziara ya kiserikali na anapokelewa punde na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.
3:30 Asubuhi: Rais Magufuli ameshaingia uwanjani, kwa sasa wasanii kadhaa wanatoa burudani akisubiriwa Rais wa Burundi, Evarist Ndaishimiye
3:47 Asubuhi: Rais wa Burundi, Evarist Ndaishimiye amewasili uwanja wa Lake Tanganyika na kupokelewa na Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli. Baada ya mapokezi inapigwa mizinga 21.
Rais Magufuli: Tumempata ndugu yetu na rafiki yetu, Rais wa jamhuri ya Burundi ambae kwa mara ya kwanza tangu aapishwe kuwa Rais wa Burundi, ameamua nchi ya kwanza ya kuitembelea iwe Tanzania.
Amekuja kwa shughuli ya mazungumzo ya kiserikali na ndio maana baada ya kukaribishwa rasmi tulitakiwa tuondoke twende kwenye mazungumzo na kabla hatujazungumza tulitakiwa pia twende kwenye sherehe nyingine ya kufungua mahakama, iliyojengwa kubwa ya kanda hii ya Kigoma.
Yale ambayo tutaenda kuyazungumza na kukubaliana tutayatoa baadae lakini nataka kutoa ya utangulizi. Biashara kati ya hizi nchi mbili zimeanza kuongezeka.
Katika suala la madini, leo tutazungumzia kuhusu suala la kuruhusu nchi ya Burundi baadhi ya amdini yake kama dhahabu yawe yanakuja yanauziwa hapa Kigoma kwa sababu bahati nzuri, sisi Tanzania tumeshafungua maduka ya madini badala ya wenzetu Burundi kuhangaikia kupeka mahali pengine tuwaombe walitumie soko la madini hapa Kigoma katika kufanya biashara.
Pia leo tutazungumzia uwezekano wa kujenga mtambo wa kuchenjua madini ya nickel, Tanzania tuna nickel Kabanga lakini pia Burundi wana nickel sehemu yao na mazungumzo yashaanza.
Leo pia tutahusisha kwenye mazungumzo kuhusu ujenzi wa reli ya kutoka Uvinza Msongati hadi Kitega. Tunataka watu wa Kigoma wakitaka kusafiri pia, watumie majini, watumie reli, watumie ndege.
Tunataka kuitengeneza hub ya biashara hapa Kigoma, tunataka tujenge uwanja mkubwa, huu tuupanue uliopo ili ndege inapotoka Dar es Salaam, inatua Kigoma, inaenda Bujumbura.
RAIS NDAISHIMIYE: Zamani Watanzania wakiona Mrundi anakuja hapa walikuwa wanadhani kuna mambo mabaya Burundi lakini sasa hivi mimi nimekuja na salam za warundi wote, wanawasalimia sana kwa niaba yao nataka kwanza mheshimiwa Rais nikupongeze, umeijenga Tanzania, umeibadilisha.
Mimi nilikuwa nakuja hapa Kigoma na familia yangu, umeibadilisha nchi ya Tanzania na Kigoma, mimi nmeshangaa kwa muda mchache tu, nimeona Kigoma imebadilika. Nakupongeza sana.
Nakupa pole, najua mchoko wa kampeni. Nina uhakika kwamba wewe kuwa na wananchi wa Tanzania ni kama baba na watoto, nina uhakika sana kwamba utashinda uchaguzi tena sana.
Na Warundi wote wanasema, nikiwepo ningechagua Dkt. Pombe Magufuli. Burundi tunasema kwamba, Watanzania ni wazazi. Tanzania ni wazazi kwa sababu tangu zamani katika kupambania uhuru, mheshimiwa baba wa Taifa alikuwa anaenda bega bega na Rwagasore wa Burundi, yeye alimsaidia, akamfikisha UN wakaenda pamoja.
Wakati wa machafuko ya Burundi, Tanzania ilikubali kubeba msalaba wa Burundi, walipokea Warundi wengi wakimbizi tangu zamani na Tanzania walituonea huruma wakakubali kwamba wale warundi walikimbilia Tanzania zamani wakapata uenyeji, tunashukuru sana.
3:30 Asubuhi: Rais Magufuli ameshaingia uwanjani, kwa sasa wasanii kadhaa wanatoa burudani akisubiriwa Rais wa Burundi, Evarist Ndaishimiye
3:47 Asubuhi: Rais wa Burundi, Evarist Ndaishimiye amewasili uwanja wa Lake Tanganyika na kupokelewa na Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli. Baada ya mapokezi inapigwa mizinga 21.
Rais Magufuli: Tumempata ndugu yetu na rafiki yetu, Rais wa jamhuri ya Burundi ambae kwa mara ya kwanza tangu aapishwe kuwa Rais wa Burundi, ameamua nchi ya kwanza ya kuitembelea iwe Tanzania.
Amekuja kwa shughuli ya mazungumzo ya kiserikali na ndio maana baada ya kukaribishwa rasmi tulitakiwa tuondoke twende kwenye mazungumzo na kabla hatujazungumza tulitakiwa pia twende kwenye sherehe nyingine ya kufungua mahakama, iliyojengwa kubwa ya kanda hii ya Kigoma.
Yale ambayo tutaenda kuyazungumza na kukubaliana tutayatoa baadae lakini nataka kutoa ya utangulizi. Biashara kati ya hizi nchi mbili zimeanza kuongezeka.
Katika suala la madini, leo tutazungumzia kuhusu suala la kuruhusu nchi ya Burundi baadhi ya amdini yake kama dhahabu yawe yanakuja yanauziwa hapa Kigoma kwa sababu bahati nzuri, sisi Tanzania tumeshafungua maduka ya madini badala ya wenzetu Burundi kuhangaikia kupeka mahali pengine tuwaombe walitumie soko la madini hapa Kigoma katika kufanya biashara.
Pia leo tutazungumzia uwezekano wa kujenga mtambo wa kuchenjua madini ya nickel, Tanzania tuna nickel Kabanga lakini pia Burundi wana nickel sehemu yao na mazungumzo yashaanza.
Leo pia tutahusisha kwenye mazungumzo kuhusu ujenzi wa reli ya kutoka Uvinza Msongati hadi Kitega. Tunataka watu wa Kigoma wakitaka kusafiri pia, watumie majini, watumie reli, watumie ndege.
Tunataka kuitengeneza hub ya biashara hapa Kigoma, tunataka tujenge uwanja mkubwa, huu tuupanue uliopo ili ndege inapotoka Dar es Salaam, inatua Kigoma, inaenda Bujumbura.
RAIS NDAISHIMIYE: Zamani Watanzania wakiona Mrundi anakuja hapa walikuwa wanadhani kuna mambo mabaya Burundi lakini sasa hivi mimi nimekuja na salam za warundi wote, wanawasalimia sana kwa niaba yao nataka kwanza mheshimiwa Rais nikupongeze, umeijenga Tanzania, umeibadilisha.
Mimi nilikuwa nakuja hapa Kigoma na familia yangu, umeibadilisha nchi ya Tanzania na Kigoma, mimi nmeshangaa kwa muda mchache tu, nimeona Kigoma imebadilika. Nakupongeza sana.
Nakupa pole, najua mchoko wa kampeni. Nina uhakika kwamba wewe kuwa na wananchi wa Tanzania ni kama baba na watoto, nina uhakika sana kwamba utashinda uchaguzi tena sana.
Na Warundi wote wanasema, nikiwepo ningechagua Dkt. Pombe Magufuli. Burundi tunasema kwamba, Watanzania ni wazazi. Tanzania ni wazazi kwa sababu tangu zamani katika kupambania uhuru, mheshimiwa baba wa Taifa alikuwa anaenda bega bega na Rwagasore wa Burundi, yeye alimsaidia, akamfikisha UN wakaenda pamoja.
Wakati wa machafuko ya Burundi, Tanzania ilikubali kubeba msalaba wa Burundi, walipokea Warundi wengi wakimbizi tangu zamani na Tanzania walituonea huruma wakakubali kwamba wale warundi walikimbilia Tanzania zamani wakapata uenyeji, tunashukuru sana.