KIGOMA: Rais wa Burundi, Evariste Ndaishimiye apokelewa na Rais Magufuli uwanja wa Lake Tanganyika, asema ana uhakika Dkt. Magufuli atashinda uchaguzi

KIGOMA: Rais wa Burundi, Evariste Ndaishimiye apokelewa na Rais Magufuli uwanja wa Lake Tanganyika, asema ana uhakika Dkt. Magufuli atashinda uchaguzi

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Leo Rais wa Burundi, Evarist Nditiye amewasili nchini kwa ziara ya kiserikali na anapokelewa punde na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.

3:30 Asubuhi: Rais Magufuli ameshaingia uwanjani, kwa sasa wasanii kadhaa wanatoa burudani akisubiriwa Rais wa Burundi, Evarist Ndaishimiye

3:47 Asubuhi: Rais wa Burundi, Evarist Ndaishimiye amewasili uwanja wa Lake Tanganyika na kupokelewa na Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli. Baada ya mapokezi inapigwa mizinga 21.

Rais Magufuli: Tumempata ndugu yetu na rafiki yetu, Rais wa jamhuri ya Burundi ambae kwa mara ya kwanza tangu aapishwe kuwa Rais wa Burundi, ameamua nchi ya kwanza ya kuitembelea iwe Tanzania.

Amekuja kwa shughuli ya mazungumzo ya kiserikali na ndio maana baada ya kukaribishwa rasmi tulitakiwa tuondoke twende kwenye mazungumzo na kabla hatujazungumza tulitakiwa pia twende kwenye sherehe nyingine ya kufungua mahakama, iliyojengwa kubwa ya kanda hii ya Kigoma.

Yale ambayo tutaenda kuyazungumza na kukubaliana tutayatoa baadae lakini nataka kutoa ya utangulizi. Biashara kati ya hizi nchi mbili zimeanza kuongezeka.

Katika suala la madini, leo tutazungumzia kuhusu suala la kuruhusu nchi ya Burundi baadhi ya amdini yake kama dhahabu yawe yanakuja yanauziwa hapa Kigoma kwa sababu bahati nzuri, sisi Tanzania tumeshafungua maduka ya madini badala ya wenzetu Burundi kuhangaikia kupeka mahali pengine tuwaombe walitumie soko la madini hapa Kigoma katika kufanya biashara.

Pia leo tutazungumzia uwezekano wa kujenga mtambo wa kuchenjua madini ya nickel, Tanzania tuna nickel Kabanga lakini pia Burundi wana nickel sehemu yao na mazungumzo yashaanza.

Leo pia tutahusisha kwenye mazungumzo kuhusu ujenzi wa reli ya kutoka Uvinza Msongati hadi Kitega. Tunataka watu wa Kigoma wakitaka kusafiri pia, watumie majini, watumie reli, watumie ndege.

Tunataka kuitengeneza hub ya biashara hapa Kigoma, tunataka tujenge uwanja mkubwa, huu tuupanue uliopo ili ndege inapotoka Dar es Salaam, inatua Kigoma, inaenda Bujumbura.

RAIS NDAISHIMIYE: Zamani Watanzania wakiona Mrundi anakuja hapa walikuwa wanadhani kuna mambo mabaya Burundi lakini sasa hivi mimi nimekuja na salam za warundi wote, wanawasalimia sana kwa niaba yao nataka kwanza mheshimiwa Rais nikupongeze, umeijenga Tanzania, umeibadilisha.

Mimi nilikuwa nakuja hapa Kigoma na familia yangu, umeibadilisha nchi ya Tanzania na Kigoma, mimi nmeshangaa kwa muda mchache tu, nimeona Kigoma imebadilika. Nakupongeza sana.

Nakupa pole, najua mchoko wa kampeni. Nina uhakika kwamba wewe kuwa na wananchi wa Tanzania ni kama baba na watoto, nina uhakika sana kwamba utashinda uchaguzi tena sana.

Na Warundi wote wanasema, nikiwepo ningechagua Dkt. Pombe Magufuli. Burundi tunasema kwamba, Watanzania ni wazazi. Tanzania ni wazazi kwa sababu tangu zamani katika kupambania uhuru, mheshimiwa baba wa Taifa alikuwa anaenda bega bega na Rwagasore wa Burundi, yeye alimsaidia, akamfikisha UN wakaenda pamoja.

Wakati wa machafuko ya Burundi, Tanzania ilikubali kubeba msalaba wa Burundi, walipokea Warundi wengi wakimbizi tangu zamani na Tanzania walituonea huruma wakakubali kwamba wale warundi walikimbilia Tanzania zamani wakapata uenyeji, tunashukuru sana.

4.jpg
3.jpg
2.jpg
1.jpg
5.jpg
 
Leo Rais wa Burundi, Evarist Nditiye amewasili nchini kwa ziara ya kiserikali na anapokelewa punde na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.
Pinga pinga wanaumia roho najua.

Na kama kawaida yao watakua wanafuatilia TBC1 japo ndo vinara wakuitukana.
 
Leo Rais wa Burundi, Evarist Nditiye amewasili nchini kwa ziara ya kiserikali na anapokelewa punde na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.

3:30 Asubuhi: Marais wote wameshaingia uwanjani, kwa sasa wasanii kadhaa wanatoa burudani kabla ya shughuli Rasmi.
Aaaaah uwanja umeshindwa kujaaa pamoja n fiesta kuwepo.
 
Hatimaye Rais wa Burundi amewasili na kupokelewa na Rais Magufuli mkoani Kigoma. Rais huyo wa Burundi Mheshimiwa Everiste Ndayishimiye aliwasili na mkewe ambaye ni first lady wa Burundi na kumtambulisha kwa mheshimiwa Rais wa Tanzania Mheshimiwa Magufuli ambaye alimtambulisha kwa Mheshimiwa Ndalichako ambaye alimpa kampani na kuondoka nae kuelekea jukwaa kuu.
 
"Uzi ko sogokuru yavuye aho. Noneho uri umuvandimwe wanjye wamaraso reka tubane." Sisi ni ndugu wa damu. Amesika bwana yule katika mapokezi.
 
Hongera sana Rais Magufuli kwa kudumisha ushirikiano na mataifa jirani, Burudi ni ndugu zetu kabisaa. Hongera kwa Rais wa Burundi. Ushirikiano huu utakuza uchumi wa nchi hizi mbili lkn haswa kwa mkoa wa Kigoma.
 
Leo Rais wa Burundi, Evarist Nditiye amewasili nchini kwa ziara ya kiserikali na anapokelewa punde na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.

3:30 Asubuhi: Rais Magufuli ameshaingia uwanjani, kwa sasa wasanii kadhaa wanatoa burudani akisubiriwa Rais wa Burundi, Evarist Ndaishimiye

3:47 Asubuhi: Rais wa Burundi, Evarist Ndaishimiye amewasili uwanja wa Lake Tanganyika na kupokelewa na Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli. Baada ya mapokezi inapigwa mizinga 21.
Nashangaa TBC bado wana kamera za kizamani za kutumia waya. Dunia ya leo wanashindwa kuwa na camera wireless! Hata matangazo wanarusha kishamba picha zinachanganywa kishamba.
 
Leo Rais wa Burundi, Evarist Nditiye amewasili nchini kwa ziara ya kiserikali na anapokelewa punde na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.

3:30 Asubuhi: Rais Magufuli ameshaingia uwanjani, kwa sasa wasanii kadhaa wanatoa burudani akisubiriwa Rais wa Burundi, Evarist Ndaishimiye

3:47 Asubuhi: Rais wa Burundi, Evarist Ndaishimiye amewasili uwanja wa Lake Tanganyika na kupokelewa na Rais wa Tanzania, Dkt. John Magufuli. Baada ya mapokezi inapigwa mizinga 21.
Believe this (amini usiamini):
bao la mkono la kwanza - Chato - Museveni kaleta maboksi ya kura
Goli la mkono la pili - kigoma- Rais wa Burundi kaingiza maboksi ya kura

Next?

hiki ndicho kilifanyika 2005 uchaguzi wa Kikwete Vs Slaa mwaka 2010 Rais wa Botswana alileta maboksi ya kura Mtwara.

CCM !!!!!!!!
 
Samahani kwa kifaransa changu, ivi BURUNDI ni kijiji chenye Rais? Kipo nchi ipi vile?
 
Kabudi naona kaanza kuvuruga Protocols, Karibu sana mheshimiwa Evariste.
 
Ziara ya hii ni kumsaidia Jiwe kwenye kampeni zake. Mbaya zaidi wanaoalikwa ni madikteta!
 
Pinga pinga wanaumia roho najua

Na kama kawaida yao watakua wanafuatilia TBC1 japo ndo vinara wakuitukana
Nilikuwa naangalia "tunavyojiaibisha kwa kukataa mawazo mbadala na kukosolewa hata tukatweka bendera kwenye mlunda!"
 
Back
Top Bottom