Kigugumizi cha nini kwenye Uraia Pacha? Shuhudia unavyowakwamisha Watanzania kuwekeza nyumbani. Miradi, mijengo ya maana ingeota kama uyoga

Kigugumizi cha nini kwenye Uraia Pacha? Shuhudia unavyowakwamisha Watanzania kuwekeza nyumbani. Miradi, mijengo ya maana ingeota kama uyoga

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Hii ni makala yangu kwenye gazeti la Mwananchi la leo 20/11/2024.

Uraia Pacha.jpg
Uraia Pacha 1.jpg
Uraia Pacha 2.jpg

Uraia Pacha 3.jpg

Uraia Pacha 4.jpg

Paskali
 
Wanabodi
Hii ni makala yangu kwenye gazeti la Mwananchi la leo 20/11/2024
View attachment 3156601View attachment 3156629
View attachment 3156617View attachment 3156618
Paskali
Ushauri wako ni Mzuri lakini ninacho shangaa Serikali Ya Tanzania kwa nini inaogopa Huo Uraia Pacha? Ungekuwa Uraia Pacha una madhara jirani zetu Wa-Kenya wasingekubali kuruhusu huo Uraia Pacha Bado sisi Wa-Tanzania tuko nyuma kila kitu ingelifaa tuige wenzetu majirani zetu Wa-Kenya walioruhusu Uraia Pacha.
 
Faida ni nyingi kuruhusu Uraia Pacha

Kuna raia wengi Marekani na Ulaya ambao Wana asili ya Tanzania, ambao wangetamani kurudi na kuwekeza nyumbani Tanzania

Hata baadhi ya wana michezo, wengi wangeweza kurudi nyumbani na kuchezea timu yetu ya Taifa

Hilo lingefanyika, huenda nasi baada ya miaka 60 ya Uhuru Tanzania ingeshiriki michuano ya Kombe la Dunia.

Najua hatujachelewa, Viongozi wanaweza kuruhusu hili likafanyika
 
Watanzania (viongozi na watawaliwa) kwa uzoefu na huenda kigenetic ni slow learners, kila kitu huwa tunafanya mwishoni kabisa na tunapigwa tu mara zote. Huwa tunasita na tunaogopa kila kitu hatimaye uoga unapopungua inakua too late na tushapoteza so hii itakujafanywa na generation ijayo kaka. Kwa sasa tuache tufe kwanza, watoto wa watoto wa 2000 watafanya tu haya. Yapo nje sana na ufahamu wetu wa kizazi hiki wa kukariri. Tazama mambo kama DECI, Mr Kuku, UPATU, Q-net nk, hata viongozi walipigwa (nao ni victims tu) ambao tungetegemea watuongoze kutuelimisha na kutahadharisha.

Sheria tu bado tunatumia na mkoloni mwingereza hatujaweza kutunga za kwetu miaka 60 baada ya uhuru, nchi zote zishahuisha katiba zao, sisi slow learners bado, kilimo chetu jembe la mkono, wakati watu wanafanya digital farming sasa, slow learners, kila mwaka tuna njaa chakula hakitoshi, slow learners, kila mwaka kuna mafuriko hadi ikulu, slow learners, kila mwaka watu wanakufa kwa kula mav na kupata kipindupindu, slow learners, shirika la ndege linapata hasara kila mwaka, slow learners tumezubaa tu na kusifia ndege, tunaagiza mafuta ya kula kwa matrilioni kila mwaka, slow learners, maprofesa wanakunywa mitishamba na mivuke kutibu covid, slow learners, maviongozi yana maphD lakini ni kama darasa la saba tu hoja zao, wanaojenga uchumi kwa kukopa na kuongeza makodi wakati uzalishaji ni uleule, slow learners, solution zetu kwa mambo mengi sana ni za kiroho yani ni uchawi na maombi, slow learners ndo maana mapsychopathy ya kidini yanaibuka na kuwalamba pesa na kutajirika wao tu na bado tu hatu-learn.

Hapa ukisema habari ya ardhi huria watasema wakenya wataiba ardhi yetu sijui wataiweka kwenye viroba? slow learners, uwekezaji watasema tunaibiwa wkt wanatuibia kwa kushirikiana nao, tamka diaspora watasema wanatishia usalama wkt sasa hivi hamna uraia pacha na usalama ni wa kufikirika tu! Anyway hamna diaspora atarisk nguvu zake kwa nchi unayoweza kuuwawa bila sababu na hamna hata uchunguzi kufanyika, yani yanaisha kiroho tu, utasikia mungu amlaze pema au mungu atamlipa NO!

Tuandaeni watoto kuwapa life skills wandugu tusirithishe hii slow learning kwa kizazi kijacho, angalau iishe kwetu.
 
Wanabodi
Hii ni makala yangu kwenye gazeti la Mwananchi la leo 20/11/2024
View attachment 3156601View attachment 3156637View attachment 3156638

PaskaliView attachment 3156640
hakuna haja ya kuwa vuguvugu wala kuwa na mawenge na jambo ambalo halina maslahi yoyote kwa taifa ispokua upotoshaji tupu...

kwamba kutokuwapo kwa uraia pacha Tanzania, ndiyo kumemzuia huyo anaishi ughaibuni kuwekeza Tanzania?

Si aende akawekeze Zambia sasa na awaajiri waTanzania huko?

hatuwezi kukubalika kuvuruga nchi yetu kwa kujaza vibaraka wa America na ulaya humu nchini na kuvuruga amani, umoja na mshikamano miongoni mwa waTanzania.

Yaan kupata fursa ya kuishi ughaibuni tu mtu anajiona kama malaika. Na inashangaza anaeishi Tanzania yuko rahisi tu kurubuniwa kusema jambo ambalo halina maslahi kabisaa kwa mwananchi wa kawaida.🐒

Mungu Ibariki Tanzania
 
hakuna haja ya kuwa vuguvugu wala kuwa na mawenge na jambo ambalo halina maslahi yoyote kwa taifa ispokua upotoshaji tupu...

kwamba kutokuwapo kwa uraia pacha Tanzania, ndiyo kumemzuia huyo anaishi ughaibuni kuwekeza Tanzania?

Si aende akawekeze Zambia sasa na awaajiri waTanzania huko?

hatuwezi kukubalika kuvuruga nchi yetu kwa kujaza vibaraka wa America na ulaya humu nchini na kuvuruga amani, umoja na mshikamano miongoni mwa waTanzania.

Yaan kupata fursa ya kuishi ughaibuni tu mtu anajiona kama malaika. Na inashangaza anaeishi Tanzania yuko rahisi tu kurubuniwa kusema jambo ambalo halina maslahi kabisaa kwa mwananchi wa kawaida.🐒

Mungu Ibariki Tanzania

Probably ni mbunge huyu mgonga meza na mawazo yake! 😛 😛 😛
 
Wabongo jolowe kila kitu waoga
Ila huenda kuna sababu ya kusema watatoa Hadhi maalum badala ya Dual
Labda tunaogopa dual citizenship kwa jirani watapewa na wenye tamaa ili wapore ardhi yote
Maana uchu unawatoka wakiona mapori yapo yapo tu
Kama wanaleta hela zao za wizi bongo na kuzizungusha huku money laundering sasa watashindwa kuhonga wapate Dual?
Serikali inalinda mali za masikini wasioona haya
Nilipaza sauti ya uraia pacha ila walipokuja na hii ya Hadhi maalum nikawaza vingine
 
Wabongo jolowe kila kitu waoga
Ila huenda kuna sababu ya kusema watatoa Hadhi maalum badala ya Dual
Labda tunaogopa dual citizenship kwa jirani watapewa na wenye tamaa ili wapore ardhi yote
Maana uchu unawatoka wakiona mapori yapo yapo tu
Kama wanaleta hela zao za wizi bongo na kuzizungusha huku money laundering sasa watashindwa kuhonga wapate Dual?
Serikali inalinda mali za masikini wasioona haya
Nilipaza sauti ya uraia pacha ila walipokuja na hii ya Hadhi maalum nikawaza vingine

Hata hiyo hadhi maalum si imekwama? Au mwenzangu umeisikia tena na mbwembwe zake?
 
umefikia kiwango chako cha mwisho sio cha fikra mpya na mawazo mbadala gentleman dah 🤣

mbona mapema sana aise 🤣

Bahati mbaya sana sikaririshwi na binadamu yeyote nipo huru sana! Haya mambo ya vibaraka wa Ulaya na Marekani nimenza kuyasikia nikiwa chipukizi wa ccm miaka ya mwisho ya 70 na 80, bado yapo kumbe! Vibaraka wa Uarabuni kama Oman, UAE, Saudia, nk hawapo? Mbn wabongo ni vibaraka tu wa levels zote na wapo tu hapo ndani? Hiyo amani unayoongelea itaharibiwa na Duality ni ipi? Una justification yoyote au ni yaleyale ya kuombea matajiri waishi kama shetani?
 
DIASPORA ni watu wanaojitambua na serikali yetu ya ccm huwa inataka kuwatawala wajinga ili itawale kwa mda mrefu
diaspora gani wanaojitambua? nadhani kama tunasolve issue ya uraia tuongee ukweli na tuwathamini tu kwa sababu ni watoto wetu na hakuna madhara wakiwa na uraia pacha, ila ni diaspora gani anajitambua, tutajie hata mmoja tu. mange? is that the real picture?

Tanzania ina over protectionism isiyo na umuhimiu wowote na hii inatokana na sera za nyerere za ujamaa, nenda hata urusi au china uone kama kuna uraia pacha, wanaogopa kuliko chochote, sababu yao kuu ati mtu hatakuwa royal kwa serikali yake, wengine wanafikiri mtu akiwa na allegiance kwa nchi mbili atatoa siri za nchi. siri zipi sasa kama Tanzania au Africa hii ambayo Marekani akitaka kukujua hahitaji mtu wa ndani, atatumia mitandao tu anakufahamu hadi chooni kwako? ni kitu gani tunacholinda hasa hadi tuwakatae watoto wetu kaka zetu na dada zetu walioenda kutafuta maisha nje? tujifunze basi, nchi zenye uraia pacha zimepata madhara gani? mfano Kenya, Rwanda, Nigeria, Ghana, South Africa, Congo DR etc wamepata madhara gani? ati watu watakuja kuchukua ardhi, kwani wakichukua wakaiendeleza pakawa pazuri utaathirika nini? wanaondoka na ardhi? Dubai mbona kuna kila mtu na maendeleo yanaonekana ni ya wadubai? kwani mtu akija na pesa yake akaspend hapa si ameongeza mzunguko, uchumi na ajira? akili za wanaopinga uraia pacha ni finyu sana.
 
Faida ni nyingi kuruhusu Uraia Pacha

Kuna raia wengi Marekani na Ulaya ambao Wana asili ya Tanzania, ambao wangetamani kurudi na kuwekeza nyumbani Tanzania

Hata baadhi ya wana michezo, wengi wangeweza kurudi nyumbani na kuchezea timu yetu ya Taifa

Hilo lingefanyika, huenda nasi baada ya miaka 60 ya Uhuru Tanzania ingeshiriki michuano ya Kombe la Dunia.

Najua hatujachelewa, Viongozi wanaweza kuruhusu hili likafanyika

Na hasara ni zipi?

-Kaveli-
 
Back
Top Bottom