Kigugumizi

Kigugumizi

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Joined
Jan 29, 2021
Posts
577
Reaction score
2,595
Ni tatizo la matamshi linalomfanya mtu asiwe na uwezo wa kutengeneza mpangilio wa moja kwa moja wa maneno na sauti anazotoa.

Watu wenye kigugumizi hufahamu maneno wanayotaka kutamka lakini hupatwa na ugumu katika kutengeneza mtitiriko wa matamshi hayo.

Changamoto hii inaweza kuambatana na tabia za kufumba macho, kukakamaa kwa misuli ya uso pamoja kutetemeka kwa midomo wakati wa kuzungumza. Pia, mambo yafuatayo huonekana-
  • Ugumu wa kuanzisha na kutamka maneno
  • Kuvuta sana neno au sauti kwenye matamshi
  • Kurudia kwa maneno
  • Kuongeza maneno ya ziada mfano “um..” kati ya neno moja na lingine
Hali ya kigugumizi huwa mbaya zaidi wakati wa furaha, uchovu au pindi mhusika anapokuwa na stress kubwa za kimwili na kiakili.

Sababu
Sababu zinazofanya mtu apatwe na kigugumizi huwa hazipo wazi sana, lakini huhusianishwa na uwepo wa changamoto kwenye sehemu ya ubongo inayo ratibu lugha na matamshi, jini za urithi (genetics) pamoja na udumavu wa mtoto kwenye hatua za awali za ukuaji.

Aidha, mtu anaweza kupata kigugumizi baada ya kupitia kiharusi au ajali yoyote kubwa inayohusisha kichwa na ubongo.

Tiba
Tatizo hilo linalomfanya mhusika apunguze kujiamini, akwepe mazungumzo hasa yale yanayohusisha hadhara kubwa, ajihisi mnyonge pamoja na kudhihakiwa na watu wengine huwa halina tiba ya moja kwa moja isipokuwa kwa kila mtu, hutegemea umri wa mhusika, historia pamoja na matarajio yake.

Kwa watoto, kigugumizi mara nyingi huchukuliwa kama sehemu ya hatua ya ukuaji wao na huisha chenyewe baada ya kufikia umri wa walau miaka 6.

Hata hivyo, msaada wa matibabu hulenga kuongeza kujiamini kwa mhusika pamoja na kupunguza ukubwa wa tatizo na madhara yanayoambatana na uwepo wake.

Chanzo: Mayo Clinic/
National Institute on Deafness and Other Communication Disorders (NIDCD)
 
Ni tatizo la matamshi linalomfanya mtu asiwe na mpangilio wa moja kwa moja wa maneno na sauti anazotoa.

Watu wenye kigugumizi hufahamu maneno wanayotaka kutamka lakini hupatwa na ugumu katika kutengeneza mtitiriko wa matamshi hayo.

Changamoto hii inaweza kuambatana na tabia za kufumba macho, kukakamaa kwa misuli ya uso pamoja kutetemeka kwa midomo wakati wa kuzungumza. Pia, mambo yafuatayo huonekana-
  • Ugumu wa kuanzisha na kutamka maneno
  • Kuvuta sana neno au sauti kwenye matamshi
  • Kurudia kwa maneno
  • Kuongeza maneno ya ziada mfano “um..” kati ya neno moja na lingine
Hali ya kigugumizi huwa mbaya zaidi wakati wa furaha, uchovu au pindi mhusika anapokuwa na stress kubwa za kimwili na kiakili.

Sababu zinazofanya mtu apatwe na kigugumizi huwa hazipo wazi sana, lakini huhusianishwa na uwepo wa changamoto kwenye sehemu ya ubongo inayohusisha lugha na matamshi, jini za urithi (genetics) pamoja na udumavu wa mtoto kwenye hatua za awali za ukuaji.

Aidha, mtu anaweza kupata kigugumizi baada ya kupitia kiharusi au ajali yoyote kubwa inayohusisha kichwa na ubongo.

Tatizo hilo linalomfanya mhusika apunguze kujiamini, akwepe mazungumzo hasa yale yanayohusisha hadhara kubwa, ajihisi myonge pamoja na kudhihakiwa na watu wengine huwa halina tiba ya moja kwa moja isipokuwa hutegea umri wa mhusika, historia pamoja na matarajio yake.
Mimi ni mmojawapo wa wenye vigugumizi kiukweli hii Hali ilinitesa zaidi shule ya msingi. Akili zilikuwemo yanaulizwa maswali natamani kujibu lakini kigugumizi kilinisababisha nikose kujiamini.

Nashukuru Mungu sekondari nilimpata mwalimu ambaye naye alikuwa na kigugumizi aligundua tatizo langu kuwa sijiamini,alinijenga na kunibadilisha Sana.

Popote ulipo mwalimu Matonya ulibadilisha Sana maisha yangu.
 
Mimi ni mmojawapo wa wenye vigugumizi kiukweli hii Hali ilinitesa zaidi shule ya msingi. Akili zilikuwemo yanaulizwa maswali natamani kujibu lakini kigugumizi kilinisababisha nikose kujiamini.

Nashukuru Mungu sekondari nilimpata mwalimu ambaye naye alikuwa na kigugumizi aligundua tatizo langu kuwa sijiamini,alinijenga na kunibadilisha Sana.

Popote ulipo mwalimu Matonya ulibadilisha Sana maisha yangu.
Hata mie mmojawapo
 
Back
Top Bottom