Kigwangala aomba radhi kwa matamshi yake. Je, ni baada ya Makamba kushambuliwa vikali mitandaoni?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301
Kaomba radhi i kupitia mtandao wa twitter akimjibu mdau mmoja aliemuhoji kuhusu kauli aliyowahi kuitoa kuwa atamuua mtu yoyote atakaeua twiga.

Tweet yake ya kuomba radhi hii hapa chini:

Niliongea kwa hasira. Nililipuka kutokana na uchungu dhidi ya wahalifu walioenda kuwinda nyara ya serikali ambayo ni alama ya Taifa bila hofu yoyote ile! Nilikosea na huwa najuta mpaka leo. Nilipaswa kuwa makini zaidi, kama Kiongozi ninayeamini utawala wa sheria/haki za binadamu.

Swali ni je, reaction ya watu kwa kauli ya Makamba pamoja na Mama kumuombea radhi Mzee Makamba kiana, ndio vimemfanya leo aone umuhimu wa kuomba radhi?
 
Hakutakiwa aombe radhi sababu hakuwahi kuua japo twiga waliuawa pia katika kipindi chake.
Alichotakiwa kujitetea ni kuwa ile ilikuwa ni kauli tu ya vitisho dhidi ya majangili. Kiuhalisia jangili akikutwa porini anaua wanyama usipomdhibiti atakumaliza wewe.

Kwa hiyo ilikuwa ni kauli katika kutekeleza majukumu ya kazi yake ambapo ni pamoja na kuwalinda hao twiga kupitia jeshi oevu.. Ni kauli na sio action.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…