Kigwangalla asema kukataza mabegi ya shangazi kaja kwenye treni ya SGR ni ubaguzi wa wazi

Kigwangalla asema kukataza mabegi ya shangazi kaja kwenye treni ya SGR ni ubaguzi wa wazi

Halafu train ikiwa na hasara, serikali iendelee kutoa subsidy.

Wapande usafiri mwingine unaoruhusu kubeba kuku na mifugo mingine.

Culture nayo ina evolve, leo ukivaa katambuga utaonekana wa hovyo. Ukitaka kubeba kuku nenda na usafiri wako.
 
Kigwangalla ni mshamba mshamba anataka mradi uwe wa hovyo apate cha kusema
 
Ndege inajulikana ni usafiri wa bei ghali ila usafiri wa train dunian kote huwa ni cheap kuliko usafiri wa hata basi. And by the way ndege uzito ni jambo la msingi ndio maana ndege wanachaji kwa uzito ila maji wanachaji kwa CBM.
Mimi hoja yangu iko kwenye nauli. Maana mwanzo ilikuwa kama vile hii train inaenda kuwa mbadala wa basi na cheap ila sasa ni kama vile ni usafiri wa tabaka fulani kwa bei zilizopo. Yani nauli ya basi ni cheap sana kuliko train naona kama vile wamehama kwenye wazo la awali sawa na walivyohama kwenye bwawa na Nyerere lilolenga kushusha bei ya umeme.
Wewe unachokosa ni Ustarabu.
 
Sasa shangazi kaja na kuku ni shida? hata kwenye ndege sijawahi kusikia wanakataza shangazkaja!!

Waweke utaratibu wa kulipia gharama za vitu vya ziada
 
Kigwangala aandika haya katika ukurasa wake wa X;

Hii ni aina ya mambo ambayo hatuwezi kunyamaza. Ni aina ya mambo yenye viashiria vya ‘ubaguzi’ wa wazi.

State crafting inataka kulinda tunu zilizoasisi Taifa. Mojawapo muhimu na kubwa ni usawa, na inclusion. Hata siku moja tusithubutu kuruhusu ama kufanya mambo yanayoigawa nchi na kuzishambulia tunu za Taifa letu kama usawa.

Yeyote anayejaribu kuwabagua wananchi wenzetu ambao bado wapo kwenye hali ya chini ya uchumi kwa namna yoyote ile tumkemee. Hatutakii mema.

SGR ni mali ya watanzania wote bila kujali hali zao na shughuli zao wanazofanya, siyo mali ya wasomi na washua tu, hata wauza kuku inawahusu.

Juzi nilitoka na mama yangu mzazi kwenda lunch pale Montana, Millenium towers, mama akanikumbusha story ya utotoni mwangu nikienda kuwasalimu baba zangu kule Goweko Mlimani nikipewa zawadi ya kuku na Shangazi zangu. Hivi leo unategemea mwanangu akienda kule akapewa zawadi ya kuku na babu zake amuache kweli?

Ukisoma autobiography ya Lee Kuan Yew, From Third World to First, The Singapore Story, anaeleza walipojenga flats na watu wakawa wanahamishwa na serikali kutoka kwenye squatters kwenda kwenye hizo flats, walikuwa wanapanda kwenye lift na ng’ombe wao! Hawakuzuiliwa. Washua waligundua ni kazi ngumu sana kukitoa kijiji kichwani, wali-accommodate mahitaji ya warugaruga. They didn’t condemn.

Taifa hujengwa namna hii sasa. Tuendelee lakini tusimuache mtu nyuma. Tujitahidi kuweka mifumo na miundo itakayowezesha kila mmoja wetu kufaidi mema ya nchi kwa urefu wa ukamba wake.

Unajua kwa nini kila anayetoboa kutoka usweken anaanza kujenga ukuta wa fence kabla hata ya nyumba, baadaye akihamia anaongezea electric fencing, CCTV cameras, security company kwa ajili ya rapid response, ananunua silaha zake anaweka chini ya mto, anafuga na German shepherds wakali, na bado kwenye milango na madirisha ameweka vyuma? Equity! Equity! Equity…my countrymen! Tuishi na wengine waishi…ukiwa na maguvu ya kumzaba mtu makofi, muachie haki yake ya kulia. Fairness! Fairness! Fairness! That’s the name of the game.
Nchi ambayo shule hazina vyoo huku wananchi wakijisaidia vichakani eti leo hawataki Shangazi kaja! Natabiri mradi huo kufa soon kutokana na laana ya Mungu
 
Kigwangala aandika haya katika ukurasa wake wa X;

Hii ni aina ya mambo ambayo hatuwezi kunyamaza. Ni aina ya mambo yenye viashiria vya ‘ubaguzi’ wa wazi.

State crafting inataka kulinda tunu zilizoasisi Taifa. Mojawapo muhimu na kubwa ni usawa, na inclusion. Hata siku moja tusithubutu kuruhusu ama kufanya mambo yanayoigawa nchi na kuzishambulia tunu za Taifa letu kama usawa.

Yeyote anayejaribu kuwabagua wananchi wenzetu ambao bado wapo kwenye hali ya chini ya uchumi kwa namna yoyote ile tumkemee. Hatutakii mema.

SGR ni mali ya watanzania wote bila kujali hali zao na shughuli zao wanazofanya, siyo mali ya wasomi na washua tu, hata wauza kuku inawahusu.

Juzi nilitoka na mama yangu mzazi kwenda lunch pale Montana, Millenium towers, mama akanikumbusha story ya utotoni mwangu nikienda kuwasalimu baba zangu kule Goweko Mlimani nikipewa zawadi ya kuku na Shangazi zangu. Hivi leo unategemea mwanangu akienda kule akapewa zawadi ya kuku na babu zake amuache kweli?

Ukisoma autobiography ya Lee Kuan Yew, From Third World to First, The Singapore Story, anaeleza walipojenga flats na watu wakawa wanahamishwa na serikali kutoka kwenye squatters kwenda kwenye hizo flats, walikuwa wanapanda kwenye lift na ng’ombe wao! Hawakuzuiliwa. Washua waligundua ni kazi ngumu sana kukitoa kijiji kichwani, wali-accommodate mahitaji ya warugaruga. They didn’t condemn.

Taifa hujengwa namna hii sasa. Tuendelee lakini tusimuache mtu nyuma. Tujitahidi kuweka mifumo na miundo itakayowezesha kila mmoja wetu kufaidi mema ya nchi kwa urefu wa ukamba wake.

Unajua kwa nini kila anayetoboa kutoka usweken anaanza kujenga ukuta wa fence kabla hata ya nyumba, baadaye akihamia anaongezea electric fencing, CCTV cameras, security company kwa ajili ya rapid response, ananunua silaha zake anaweka chini ya mto, anafuga na German shepherds wakali, na bado kwenye milango na madirisha ameweka vyuma? Equity! Equity! Equity…my countrymen! Tuishi na wengine waishi…ukiwa na maguvu ya kumzaba mtu makofi, muachie haki yake ya kulia. Fairness! Fairness! Fairness! That’s the name of the game.
Ungelipigania kwamba Mbunge Mmasai avae lubega, sime kiunoni na fimbo mkononi awapo ndani ya Bunge mbona ningekuelewa!!!
 
Back
Top Bottom