Kigwangalla na Lusinde mnahoji uanachama wa Dkt. Bashiru, mbona hamkuhoji alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM?

Kigwangalla na Lusinde mnahoji uanachama wa Dkt. Bashiru, mbona hamkuhoji alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM?

CCM oyee!

Zidumu fikra za mwenyekiti Magufuli
Bashiru Ally aliteuliwa na mwenyekiti wa CCM, Rais Magufuli, hamkupiga ktk kikao chochote zaidi ya kumpongeza huku KIgwangalah ukijua kuwa Bashiru ni mwanachama wa CUF.

Wapinzani waliteuliwa na kupewa nyadhifa serikalini huku mkijua serikali iliyopo sio ya umoja wa kitaifa lakini hamkupinga zaidi ya kumpongeza mwenyekiti wa CCM Rais Magufuli.

Wapinzani walinunuliwa na kupitishwa kugombea udiwani na ubunge kwa tiketi ya CCM bila kupewa au kusalimisha kadi za uanachama wao huko walikotoka hamkupinga wala kuhoji zaidi ya kumshangilia mwenyekiti wa CCM Rais Magufuli.

Huo ni inafiki wa kisiasa
View attachment 2425602View attachment 2425603
Kigwangala, sidhani kama yupo 100% perfect upstairs.

Ana mashaka na uwanachama wa Bashiru, wakati ameshindwa kuwa na mashaka na yeye kuitwa Kigwangala wakati Baba yake ni Bagalile.

Anamshangaa Bashiru, wakati anashindwa kujishangaa yeye ilikuwaje mwaka ule 2010, apate kura chini ya 500 za wajumbe kwenye kura za maoni, halafu ateuliwe kuwa mgombea wakati wapinzani wake, Bashe alipata kura zaidi ya 3,000 na Seleli zaidi ya kura 2,000.

Wala hashangai yeye mpaka kuwahi kuwa Waziri wakati pale Moolman alipokuwa ameajiriwa kama store keeper alifukuzwa kutokana na yeye kuiba baruti.
 
Mnaacha hoja mnajadili vyama, Mwl. Nyerere alishangaa sana kuona CCM inashindwa kujadili hoja na kupoteza mda mwingi kujadili vihoja na watu. Chama kinasimama na kueimamiwa na "wenye uwezo wa kujenga hoja"
 
Kigwangala, sidhani kama yupo 100% perfect upstairs.

Ana mashaka na uwanachama wa Bashiru, wakati ameshindwa kuwa na mashaka na yeye kuitwa Kigwangala wakati Baba yake ni Bagalile...
Kosa la kufoji vyeti na kuiba majinà ya watu lina laana na ndo maana mwamba hajielewi elewi Hivi. Anabaki kupambana na watu kila mtu yeye anaparamia tu
 
Ninashangaa sana Kibajaji kuhoji uanachama wa BASHIRU wakifanya hivyo wanakibomoa chama chote. Yeye mwenyewe alikuwa CHADEMA,na wako wengi tu wakuu wa wilaya,wabunge wenyeviti km M temvu walikuwa upinzani. Wajibu hoja watu wameelemeki sana itakula kwao 2025.
 
Back
Top Bottom