Kijana akoswakoswa kuchomwa kisu na mwenzie kisa mwanamke

MR.NOMA

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2014
Posts
339
Reaction score
505
Katika Hali ya kustajabisha tar 31 Dec 2021, mitaa ya Kimara Mavurunza, kijana mwenye genge la nyanya, tikiti,nanasi etc. Alivamiwa kijana mwingine mwenye hasira huku akifoka na kumwambia mara ngapi nimekuonya hutaki kusikia, basi jamaa akachukua kisu cha palepale gengeni akamwambia Leo nakumaliza, Ile amepiga cha kwanza akamkosa jamaa mwenye genge alikimbia mbio mithili ya Filbert Bayi kuelekea kusikojulikana.

Mwamba alipasua matikiti,viazi,nanasi na nk. Na kuondoka simu ya jamaa. Taarifa za awali zinasema kuwa mwenye genge alishaonywa mara kadhaa aache mazoea na kuchart na binti fulani ambaye mbabe emezaa naye ila hawaishi pamoja
 
Akamatwe mara Moja Mhalifu Huyo.
Mashitaka SABA Naam Nane yafunguliwe dhidi yake

1. Kufanya mapenzi bila ndoa - ushahidi mwanamke aliyezaa naye.
2. Kutishia Kuua
3. Kudhamiria Kuua
4. Kuharibu Mali - matunda
5. Kuiba Mali - simu
6. Kuleta taharuki katika Jamii.
7. Ugaidi
8. Uhujumu Uchumi
 
9. Kutakatisha mbuchuchu (hana uhakika mtoto wa huyo demu ni wake kweli)
 
9. Kumzuia mjasiliamali kutimiza wajibu wake
 
huyo kijana ni mshamba wa mapenzi. Ni dizaini ya wale watu ambao wakipewa busu na demu wanaona dunia yote ipo mfukoni mwao.

siku akijamfuma huyo anayezani ni demu lake pekeake akiliwa kiboga na wahuni na kukanwa hadharani ndo huishia kujiuwa au kuleta sintofahamu
 
Huyo mhalifu siyo wa kuacha aendelee kuhatarisha maisha ta eatu

Atafutwe na afungwe tu
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚, hapo hakuna ushahidi wa hata moja, na hilo la kwanza si kosa kisheria
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…