Pre GE2025 Kijana aliyegonga gari la Mkuu wa Mkoa wa Mwanza anunuliwa pikipiki mpya

Pre GE2025 Kijana aliyegonga gari la Mkuu wa Mkoa wa Mwanza anunuliwa pikipiki mpya

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Wakuu,

Wakati mnaendelea kujadili mchuano kati ya Lissu na Mbowe, viongozi wa CCM wameendelea kutustaajabisha!

=================================================

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda, amemkabidhi pikipiki mpya kijana Kusana Lumambo, aliyegonga gari la mkuu huyo wa mkoa na kuharibu pikipiki yake katika ajali iliyotokea eneo la Mkuyuni, Jijini Mwanza.

Akizungumzia tukio hilo, Mtanda amesema kuwa baada ya ajali hiyo, Lumambo alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando akiwa hajitambui na alikaa katika Chumba cha Uangalizi Maalum (ICU) kwa muda wa wiki tatu.

Pamoja na kueleza kuwa kijana huyo ndiye aliyekuwa na makosa kwenye ajali hiyo, Mtanda amesema alihakikisha anapata matibabu ya kina, akilipa gharama zote za matibabu ambazo zilifikia jumla ya shilingi milioni 12.

 
Angestahili anahakikisha sheria imechukua mkondo wake ili kuzuia ajali ya hivyo isitokee tena. Baada ya hukumu kama amemuenea huruma sana amlipie faini na hayo mengine yafuate.

Vijana wenye bada kuukuu wakajibamize kwa huyo mwamba(kwa tahadhari) ili wapate mpya..
Mtu akiwa wa Siasa ni lazima awe mjinga....siasa bhana.
 
Angestahili anahakikisha sheria imechukua mkondo wake ili kuzuia ajali ya hivyo isitokee tena. Baada ya hukumu kama amemuenea huruma sana amlipie faini na hayo mengine yafuate.

Vijana wenye bada kuukuu wakajibamize(kwa tahadhari) ili wapate mpya..
Mtu akiwa wa Siasa ni lazima awe mjinga....siasa bhana.
Linapofika suala la utu sheria huwa inakaa pembeni kwanza,kumbuka utu ni natural force inayotoka ndani ya moyo ila sheria ni nguvu za nje zilizopangwa na wanadamu....Unaweza kuta hata hajafanya kwa ajili ya siasa ila ana UTU
 
Hata mamba wakati wa kummeza mtu anafanya hivyo huku machozi yakimtoka kuonesha huruma yake feki.
 
Linapofika suala la utu sheria huwa inakaa pembeni kwanza,kumbuka utu ni natural force inayotoka ndani ya moyo ila sheria ni nguvu za nje zilizopangwa na wanadamu....Unaweza kuta hata hajafanya kwa ajili ya siasa ila ana UTU
👏👏Umenikosha sana kwa hizi points. Hivi uko single au uko booked?
 
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Said Mtanda amemkabidhi Pikipiki mpya kijana Kusan Alex Dereva Bodaboda ambaye aliligonga gari la Mkuu wa Mkoa huyo October 31 2024 katika eneo la Chakechake Mkuyuni Jijini Mwanza.

Mtanda amebainisha kuwa kwa mujibu wa sheria za usalama barabarani Bodaboda huyo alikuwa na makosa lakini kama Kiongozi aliamua kumsaidia na kumlipia gharama za matibabu kiasi cha Tsh. milioni 12 katika Hospitali ya Kanda ya Bugando pamoja na kumnunulia pikipiki mpya ili arejee kwenye shughuli zake kama kawaida.
 
Back
Top Bottom