Kijana na Mama yake Mzazi

tatanyengo

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2011
Posts
1,133
Reaction score
280
Katika siku za hivi karibuni nimesikia katika vyombo vya habari visa vya kushangaza. Kuna kisa cha huko Songea ambacho mama na kijana wake wa kuzaa wamekuwa wapenzi kwa takribani miaka kumi. Na kingine kimetokea huko kanda ya ziwa, baba alimfumania mke wake akifanya mapenzi na kijana wao. Baba aliwacharanga mapanga na kuwaondolea uhai.

Jamani wana JF tulizoea kusikia akina baba ndo wanatabia ya kufanya mapenzi na mabinti zao. Sasa hili wimbi la akina mama kufanya tendo hilo na vijana wao linashika kasi, ni kitu gani kimetokea katika jamii?
 
mimi nahisi pia imani za kishirikina zinachangia sidhani kama mtu na akili yake timamu anaweza kuwaza hvyo, Mwenyezi Mungu atusamehe
 

Ni habari zinazosikitisha mno kufanywa na mwanadamu mwenye akili timamu! Nafikiri bainadamu sasa tumepoteza utu na kukosa adabu kwa kiasi kikubwa mno. Pia tumekaa mbali na Mungu na hivyo kujikuta tunaenenda kwa kuzifuata tamaa zetu mbaya na kujikuta tukiyatenda yale tusiyopaswa kuyatenda na kujiingiza kwenye imani zisizo sahihi.
Nafikiri inatakiwa ifike wakati kila mtu kwa imani yake, amrudie Muumba wake vinginevyo ipo siku tutakuja kusikia mabaya zaidi au kuangamizwa kabisa kwa hasira ya Mungu kama baadhi ya vitabu vya dini vinavyosema.
Nashauri kila mwenye nia njema na aendelee kukemea vitendo hivi...
 
Hii habari hata mimi imenishangaza sana. nabaki nikijiuliza iwapo huyo kijana na mama yake wana akili timamu kweli!
 
Mh! Inasikitisha sana kwa binadamu ambaye Mungu alimwamini na kumpa utashi na sasa amekuwa yeye ndo anafanya yale mambo ambayo ndo anafanya mnyama, cjui hapa anaemtamani mwenzake na kuamua kuandaa mazingira ni nani?
 
Ushetani unazidi kujiinua, ni Dalili za siku za mwisho, Tumwombe sana Mungu aturehemu, maangamizi haya yasiendelee kati yetu

Bila Reheme ne Neeme zake Mungu Hatuwezi
 
Ni kazi ya shetani tu na maagenti wake.

"when we fight against flesh n blood, we will be fighting the wrong battle" T.B. Joshua
 
Jamani haya ni matatizo ya utandawazi,mimi nimezisikia habari hizi na kusoma kwenye majarida ya wenzetu Ulaya mambo haya miaka ipatayo 20 huko nyuma,ila naona huku kwetu ndio yanaingia,kwa wenzetu wazungu na wahindi jambo hili si la kushangaza sana kwani matukio haya kwao sio mageni.
 
mambo haya yapo tangu siku nyingi, mama na mwanae, baba na bintiye, kaka na dada, mtu na binamu nyama ya hamu, mtu na mamake mdogo hasa wakiwa na umri unaolingana, ndugu kwa ndugu wengi tu wanafanya ngono ila huwa inakuwa siri sana. kuna dada mmoja namfahamu, ana miaka kama zaidi ya thirty, hajaolewa, anatembea na kaka yake mtoto wa babake mdogo hadi leo hii.kaka anaweza kuja geto kwake saa saba usiku, ukiingia kwake unakuta bro amevua shati na amebaki na kaptula tu kifua wazi, ati joto la dar....akimaliza mambo yake anawasha gari anaondoka...hii inatokana na kuanza wakiwa wadogo ile michezo ya mama na baba, akilogwa kufanya wakati anavunja ungo au akambikirii tu, basi watakuwa wanafanya hata wakiwa watu wazima pale wanapopata nafasi....iyo ya wazazi na watoto ni zaidi sana uchawi, anapofanya hivyo nguvu zake za kichawi zinaongezeka.
 
Mbona maofisini watu wanaipindua mijimama umri sana na mama zao huko kijijini..kawaida tu hakuna jipya hapa
 
siku hizi akina mama wanakuja kwa kasi...wanaenda sambamba na waume zao...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…