G7seven
Member
- Mar 25, 2022
- 95
- 251
Wahenga wanasema ukitaka kupata urahisi wa kufanya jambo lako washirikishe wazee, ukubwa dawa. Wiki iliyopita nilikuwa na wazee wetu kijijini, tulikutakana kwenye ndoa ya kijana mwezetu kutoka kwenye ukoo.
Katika kupiga soga za hapa na pale kuna mzee mmoja akawa anasitiza na sisi vijana wengine tufanye mpango tupate majiko kama ilivyo kwa vijana wezetu, tuache woga wa kusingiziazia ugumu wa maisha. Uzuri wa huyu mzee ni mkogwe na anakupa sababu kwanini anashinikiza tufanye mpango wa kuvuta majiko na tuzingatie kitu gani kabla hujafanya maamuzi ya kuvuta jiko.
Moja kati ya kigezo ambacho niliona anatoa msitizo kwa kiwango kikubwa ni umri wa huyo mwanamke unayetaka kufunga naye ndoa, wewe na yeye umepishana naye umri wa miaka mingapi? Mwazoni nilikuwa sifahamu umri wa mwanamke hubeba tafsri nyingi tofauti na tunavyodhani.
Alitoa msitizo kwa jinsi wanawake wa sasa walivyo ikiwezekana hata ukimzidi miaka tisa, nane au kumi haina hasara kwa mujibu wa ushauri wake. Anadai kuoa mwanamke niliyemzidi umri wa miaka miwili/mitatu itakula kwangu.
Akaenda mbali na kusema ikitokea nataka kuoa mwanamke tuliyelingana miaka basi baada ya kipindi fulani kupita, nioe mwanamke mwingine wa umri mdogo ili kuja kufidia la nafasi ya mke mkubwa.
Mzee alienda mbali zaidi, alinipa mualiko nikatembelee nyumbani kwake nikasalimie wake zake, mzee ana wake watatu. Siku ya pili nilipotembelea nyumbani kwake, nilikuta wanakikao cha familia na mimi nikapewa mualiko nijumike nao.
Kwa kigezo cha umri niliona mzee hadanganyi, kila nikiangalia wake zake wawili wa mwanzo wanaonekana wakubwa kuzidi hata yeye, wakati mzee yeye ni mkubwa kuliko wake zake wote. Tena kwa mujibu wa maelezo yake kawazidi umri wa miaka saba kwenda juu, mke mdogo ndiyo anaonekana bado mdogo.
Mzee akaenda mbali zaidi akanambia kwa umri wenu vijana mliozaliwa miaka ya 90's tutafute mabinti waliozaliwa miaka ya 2000 hadi 2004, tofauti na hapo tujiandae kuoa ndoa za mke zaidi ya mmoja au kumchoka mkeo.
Sababu nyingine ambayo mzee alitoa niliona inamashiko makubwa, alisisitiza kutothubutu hata kwa bahati mbaya kuoa mwanamke ambaye awe amewahi kuishi na mwanaume kinyumba kama mke na mume, iwe alizalishwa au hakuzalishwa.
Tena katika kundi ambalo alikandia vibaya ni hili, kumbe vijana mnaoleta mada za kuunga mkono tuoe mabikra mna maono ya mbali. Mzee alinipa sababu za kwa nini mwanamke aliyewahi ishi na mwanaume hapaswi kabisa kuolewa.
Akanipa na umri mzuri wa mwanamke wa kuoa na sababu za kwanini umri huo, kwa mujibu wa maelezo yake anadai umri mzuri ni miaka 18 hadi 22.
Vitu vingi sana alinambia, mfano mfumo wa umiliki mali, mfano yeye ana ng'ombe na mbuzi wa kienyeji, alinambia hata itokee kasafiri miaka kumi hakuna mwanamke atathubutu kuuza ng'ombe au mbuzi bila ya kutoa amri yake yeye na ikitokea imeuzwa ng'ombe au mbuzi hela yote anakaa nayo, yeye ndiyo anatoa maamuzi nani ampe 10, nani ampe 20. Anakwambia ni mwiko mwanamke kukaa na hela.
Katika kupiga soga za hapa na pale kuna mzee mmoja akawa anasitiza na sisi vijana wengine tufanye mpango tupate majiko kama ilivyo kwa vijana wezetu, tuache woga wa kusingiziazia ugumu wa maisha. Uzuri wa huyu mzee ni mkogwe na anakupa sababu kwanini anashinikiza tufanye mpango wa kuvuta majiko na tuzingatie kitu gani kabla hujafanya maamuzi ya kuvuta jiko.
Moja kati ya kigezo ambacho niliona anatoa msitizo kwa kiwango kikubwa ni umri wa huyo mwanamke unayetaka kufunga naye ndoa, wewe na yeye umepishana naye umri wa miaka mingapi? Mwazoni nilikuwa sifahamu umri wa mwanamke hubeba tafsri nyingi tofauti na tunavyodhani.
Alitoa msitizo kwa jinsi wanawake wa sasa walivyo ikiwezekana hata ukimzidi miaka tisa, nane au kumi haina hasara kwa mujibu wa ushauri wake. Anadai kuoa mwanamke niliyemzidi umri wa miaka miwili/mitatu itakula kwangu.
Akaenda mbali na kusema ikitokea nataka kuoa mwanamke tuliyelingana miaka basi baada ya kipindi fulani kupita, nioe mwanamke mwingine wa umri mdogo ili kuja kufidia la nafasi ya mke mkubwa.
Mzee alienda mbali zaidi, alinipa mualiko nikatembelee nyumbani kwake nikasalimie wake zake, mzee ana wake watatu. Siku ya pili nilipotembelea nyumbani kwake, nilikuta wanakikao cha familia na mimi nikapewa mualiko nijumike nao.
Kwa kigezo cha umri niliona mzee hadanganyi, kila nikiangalia wake zake wawili wa mwanzo wanaonekana wakubwa kuzidi hata yeye, wakati mzee yeye ni mkubwa kuliko wake zake wote. Tena kwa mujibu wa maelezo yake kawazidi umri wa miaka saba kwenda juu, mke mdogo ndiyo anaonekana bado mdogo.
Mzee akaenda mbali zaidi akanambia kwa umri wenu vijana mliozaliwa miaka ya 90's tutafute mabinti waliozaliwa miaka ya 2000 hadi 2004, tofauti na hapo tujiandae kuoa ndoa za mke zaidi ya mmoja au kumchoka mkeo.
Sababu nyingine ambayo mzee alitoa niliona inamashiko makubwa, alisisitiza kutothubutu hata kwa bahati mbaya kuoa mwanamke ambaye awe amewahi kuishi na mwanaume kinyumba kama mke na mume, iwe alizalishwa au hakuzalishwa.
Tena katika kundi ambalo alikandia vibaya ni hili, kumbe vijana mnaoleta mada za kuunga mkono tuoe mabikra mna maono ya mbali. Mzee alinipa sababu za kwa nini mwanamke aliyewahi ishi na mwanaume hapaswi kabisa kuolewa.
Akanipa na umri mzuri wa mwanamke wa kuoa na sababu za kwanini umri huo, kwa mujibu wa maelezo yake anadai umri mzuri ni miaka 18 hadi 22.
Vitu vingi sana alinambia, mfano mfumo wa umiliki mali, mfano yeye ana ng'ombe na mbuzi wa kienyeji, alinambia hata itokee kasafiri miaka kumi hakuna mwanamke atathubutu kuuza ng'ombe au mbuzi bila ya kutoa amri yake yeye na ikitokea imeuzwa ng'ombe au mbuzi hela yote anakaa nayo, yeye ndiyo anatoa maamuzi nani ampe 10, nani ampe 20. Anakwambia ni mwiko mwanamke kukaa na hela.