Kijana wa kiherero alivyowatembezea mkono Vasco Da Gama kwenye pwani ya Namibia karne ya 14

Kijana wa kiherero alivyowatembezea mkono Vasco Da Gama kwenye pwani ya Namibia karne ya 14

Maghayo

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2014
Posts
20,307
Reaction score
47,210
Mzuka wanajamvi!

Kati ya makabila yanayopenda na kuthamini Ng'ombe kupindukia ni Herero Namibia, Fulani (Nigeria, Niger, Guinea, Mali, CAR na western Sudan, Maasai, Sukuma na Tutsi.

Vasco Da Gama aliandika walipokaribia pwani ya Namibia wakitokea Goa India baada ya kutafuta trade route ya spices walitia Nanga Namibia.

Vasco anasema hali ya hewa ya southern Atlantic ilikuwa nzuri. Yeye na crew yake walichoka kukaa majini safarini muda mrefu. Wakitokea Cape of good hope (cape town).

Walipokuwa ufukweni na kutafuta maji salama fresh water. Kwa mbali wakaona kundi la mifugo Ng'ombe .

Kwa shauku wakasogea walishangaa kumuona kijana mmoja mwembamba mrefu sana akiwachunga.

Kijana huyu mrefu sana na mwembamba alikuwa kutoka kabila la Herero.

Naye pia alishangaa kuona kundi hili la wazungu weupee na meli akawasogelea.

Vasco Da Gama wakajaribu kuwasiliana naye kwa ishara ni wapi karibu watapata maji ikawa vigumu kwasababu ya lugha gongana.

Sasa Kina Vasco walipendezwa na muonekano wa huyu dogo urefu wake nauwembamba haukuwa wa wakawaida.

Wakapanga mpango ovu wa kumteka na kumuingiza kwenye meli yao na kumpeleka Ureno ili wamtumie kupata hela kwenye manesho.

Ila dogo machale yakamcheza akawashtukizia. Kitendo kile cha kumzingira na kutaka kumkamata na kumfunga kamba. Dogo akamngata mmoja na kutoa ukunga wa hatari.

Dogo akapiga summersaults za mfulululizo wakamfuata. Akamuasha beberu mmoja ngumi ya taya. Akaangukia huko kwenye korongo.

Na akaendelea kutembeza dozi za maana kwa hawa mabeberu wa kireno. Ngumi za tumbo na buti za kaynday aliwatembezea kweli.

Ilikuwa mnyukano wa aina yake kati ya wareno ka 20 na dogo mmoja mwafrika.

Vasco anaelezea dogo alikuwa anarusha ngumi mfululizo za uhakika anaweza kubwaka na kujirusha kima cha thabeet akirudi chini kima cha tulia na joti saba chini.

Baada ya kupambana dogo alifanikiwa kuponyoka na kutokomea na kuacha ng'ombe nyuma.

Vasco na crew yake wakachinja Ng'ombe mmoja haraka haraka kumchoma na kirudi faster kwenye meli wakijua dogo kaenda kuwashtua wenzake.

My take (lugha ya JF)

Hapo kwenye mkono dogo anapotembeza dozi nimeogezea chumvi na chai. Ila Vasco da gama aliandika mkono dogo aliutembezakweli tena wa uhakika.

Pia katika simulizi za kiherero kisa hiki kinasimuliwa sana kizazi na kizazi.


Senior JF accredited Historian and anthropologist
 
Kabila la Herero ni wa Bantu ambao wanaishi kusini mwa Africa kwa wingi Namibia. Japo Herero wengi wako namibia lakini kuna baadhi wachache wanaishi Botswana na Angola.

Lugha yao wanayoongea ni otjiherero.
Ni warefu kwa kina na wanapenda kufuga ng'ombe karne na karne.

Ujerumani ilipokuwa wakoloni Namibia waliwaua sana kwenye vita ya kimbari. Na kupelekea Ujerumani karibuni kuwaomba msamaha na kuwafidia.

Herero ni kabila wanaijiopenda na kujivunia.
 
Huenda hapa ndio dogo wa kiherero alivyowatembezea mkono Vasco da gama na wenzake. Picha hii ni pwani ya Namibia south Atlantic.
istockphoto-156278254-612x612.jpg
 
Binafsi niko vizuri sana kupigana, karataker wa black belt. ila kuna siku nilimwona masai mmoja akiwa amepandwa na mori, kidogo alinistua kuwa huyu ukienda vibaya anaweza kukusumbua though at the end utampiga pamoja na kwamba yeye hana skills.

Alikuwa anaruka na haogopi kufa hata nukta, alijigongesha kwenye kuta damu zinamtoka lakini ni kama amepagawa na mashetani. tusiwadharau hao watu wa vijijini. nahisi dodo mori ilipanda akawatembezea kichapo kweli.
 
Namibia ni nchi nzuri sana, lakini sijui wizara yao ya utali inafeli wapi katika kutangaza vivutio vilivyopo nchini mwao.
 
Back
Top Bottom