Pre GE2025 Kijana wewe ni Taifa la leo, kagombeeni nafasi katika chaguzi zinazokuja, muwe na nguvu ya maamuzi

Pre GE2025 Kijana wewe ni Taifa la leo, kagombeeni nafasi katika chaguzi zinazokuja, muwe na nguvu ya maamuzi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

mockers

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2013
Posts
12,843
Reaction score
35,442

kish.PNG

Umeelewa nini kwenye katuni hii?​

Kijana Mtanzania, badili mtazamo

Tuwasihi vijana wetu wagombee nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi wa Serikali za Mtaa kuanzia mwaka huu na hatimaye wagombee uchaguzi mkuu mwakani.

Vijana, kueni na uthubutu. Hapa tunawahitaji vijana wa vyama vyote vya siasa. Nendeni muoneshe makali yenu ya hoja na muweze kuleta mabadiliko kwenye nchi yetu.

Vijana, msikae kulalamika. Msiwaige vijana wa hovyo walioamua kuishi kama wapambe au machawa. Kapambaneni huko, ikishindikana msikate tamaa.

Nchi na hatma yake iko mikononi mwenu. Naamini mkijieleza vizuri mtaaminiwa tu bila tatizo.

Iwe ni nafasi ya mwenyekiti wa mtaa, mwenyekiti wa kijiji, udiwani, ubunge, hata urais. Kagombeeni msiogope.

Vaeni roho za wapigania uhuru na wakataa utumwa kama Mkwawa, Mtemi Isike, Mwami Ntare, Nangwanda. Ingieni kwenye siasa kwa wingi wenu, mtafanya kitu.

Shime shime, nendeni msiogope kitu chochote. Ninyi ni taifa la leo na hazina ya leo na ijayo.
 
We hautaki kugombea kaka?
53 sio kijana tena, tunataka viongozi damu inayochemka wataokimbizana na dunia, mimi tayari niko shambani nachunga vimbuzi vyangu na napata maziwa ya ving'ombe vyangu inatosha kabisa, vijana wakibali mtazamo wao tutasonga mbele waingie kwenye ngazi za maamuzi sasa wasiishie kulalamika, tunawahitaji akina Nyerere, Salim Ahmed salim, Kighoma malima, Samuel Sitta, Warioba, Mzindakaya, Kikwete na kadhalika hao walikua vijana walioingia kwenye uongozi enzi zao wakiwa hawajafika hata miaka 30 , vijana wasiishie kubet tu tuwaunge mkono wao ndio taifa la leo
 
O
Kijana Mtanzania badili mtazamo.
Tuwasihi vijana wetu wakagombee nafasi mbalimbali za uongozi kwenye uchaguzi wa serikali za mtaa kuanzia mwaka huu na hatimaye wagombee uchaguzi mkuu mwakani.
Vijana kueni na uthubutu hapa tunawahitaji vijana wa vyama vyote vya siasa nendeni muoneshe makali yenu ya hoja na muweze kuleta mabadiliko kwenye nchi yetu.
Vijana msikae kulalamika, musiwaige vijana wa hovyo walioamua kuishi kama wapambe au machawa, kapambaneni huko ikishindikana msikate tamaa,
Nchi na hatma yake iko kwenu, naamini mkijieleza vizuri mtaaminiwa tu bila tatizo.
Iwe nafasi ya mwenyekiti wa mtaa, mwenyekiti wa kijiji, udiwani, ubunge hata urais kagombeeni msiogope.
Vaeni roho za wapigania uhuru na wakataa utumwa kama Mkwawa, mtemi isike, mwami ntare, Nangwanda, ingieni kwenye siasa Kwa wingi wenu mtafanya kitu.
Shime shime nendeni msiogope kitu chochote ninyi ni taifa la leo na hazina ya leo na ijayo.
Ongeza vijana wanaojitambua ,sio kila kijana anajitambua hasa machawa zero kabisa
 
53 sio kijana tena, tunataka viongozi damu inayochemka wataokimbizana na dunia, mimi tayari niko shambani nachunga vimbuzi vyangu na napata maziwa ya ving'ombe vyangu inatosha kabisa, vijana wakibali mtazamo wao tutasonga mbele waingie kwenye ngazi za maamuzi sasa wasiishie kulalamika, tunawahitaji akina Nyerere, Salim Ahmed salim, Kighoma malima, Samuel Sitta, Warioba, Mzindakaya, Kikwete na kadhalika hao walikua vijana walioingia kwenye uongozi enzi zao wakiwa hawajafika hata miaka 30 , vijana wasiishie kubet tu tuwaunge mkono wao ndio taifa la leo
Okay shkamoo dingii.....

Hongera kwa maisha yako ya amani, vijana wa sahivi hawana huo uthubutu, uthubutu ni kwenye keyboards tu.
 
Okay shkamoo dingii.....

Hongera kwa maisha yako ya amani, vijana wa sahivi hawana huo uthubutu, uthubutu ni kwenye keyboards tu.
maneno hayo tumezungumza na rafiki yangu, kaka yangu zangira juzi wakati kanitembelea, kua uthubutu Kwa vijana wetu sasa ni tatizo kubwa
 
Kupitia chama gani? Hiii ccm inayowarudisha wazee?

Sehemu pekee ambapo vijana wangepata fursa ya kuonesha uwezo wao ni upinzani, lkn Tume-MTU inapoka ushindi. Acha tuwe watazamaji tu.
 
Naunga mkono hoja Tena msiogope serikali imejaa vikongwe imezeeka ,bunge limejaa vikongwe limezeeka

Sensa inaonyesha vijana ndio wengi serikali ya walio wengi ni pamoja na vijana wengi kuwemo.bungeni
 
"nendeni muoneshe makali yenu ya hoja na muweze kuleta mabadiliko kwenye nchi yetu."

Kwa ushauri kutoka Kwa wazee. Hata CCM ukiwa na uzalendo WA nchi unaweza kuleta mabadiliko... Vyama vingine Ni kama kuhenyeka kujenga chama na nchi Kwa wakati mmoja kitu ambacho ni kujizeesha mapema. Vijana tuangalie penye urahisi kupenya
 
Vijana mbona wapo wengi tuu serikalini kwenye nafasi za maamuzi na ndio taswira ya vijana wengine waliobaki huku mtaani
 
"nendeni muoneshe makali yenu ya hoja na muweze kuleta mabadiliko kwenye nchi yetu."

Kwa ushauri kutoka Kwa wazee. Hata CCM ukiwa na uzalendo WA nchi unaweza kuleta mabadiliko... Vyama vingine Ni kama kuhenyeka kujenga chama na nchi Kwa wakati mmoja kitu ambacho ni kujizeesha mapema. Vijana tuangalie penye urahisi kupenya
Tubadili mtazamo vijana wa SA hawajajifunga na ANC Kwa sasa mabadiliko popote na vyama mbadala sio dhambi wala jinai
 
Vijana hawana mpango wowote na Uchaguzi Mkuu. Nadhani hata baadhi ya sisi wazee, nimewahi kumuuliza Mh. Mbunge wangu hapa nilipo: Je, kuna ugumu gani kutunga na kupitisha Sheria ya Wazee wakati Sera ilitungwa na kupitishwa zaidi ya miaka 20 iliyopita na wewe hapa katikati umeshawahi kuwa Waziri wa Katiba na Sheria? Majibu ni yale yale ya kisiasa zaidi, hakuna TIME FRAME ya utekelezaji!
 
Back
Top Bottom