kilimbamula
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 1,792
- 853
Wiki hii tutashuhudia wawakilishi wetu kimataifa Simba na Yanga zikijitupa uwanjani kucheza mechi za kimataifa. Yanga leo itacheza na Washelisheli na kesho Simba itacheza na Wadjibuti katika vikombe tofauti.
Msemaji wa Simba Haji Manara alitoa rai kwa wapenzi na mashabiki wa Simba kutoizomea Yanga. Alisema kuwa, hakuna nchi yoyote duniani ambayo mgeni anashangiliwa. Akawaasa wana Simba kuwa kama mtu akiona inamshinda kuishangilia Yanga bora akae kimya kwenye jukwaa kuliko kuipa support Shelisheli. Huo ni mwanzo mzuri kuelekea kwenye ustaarabu.
Kinyume chake, fyatu wa soka Bw. Mkemi ambaye hadi leo anaamini kuwa lazima upinge kila kitu anachosema mpinzani wako kama ilivyo kwenye siasa. Mkemi, sina hakika kama alienda na kichwa chake maana nimesikia sound clip tu, amewataka Yanga kubaki katika ushenzi wa utamaduni mbovu usioleta ushindani na unaotaka upande mmoja kutofurahia mafanikio ya upande mwingine.
Kizazi kile cha kuamini matunguri na wahubiri chuki kimepita, hiki kizazi cha wastaarabu tunataka kuona soka lenye tija na mshikamano.
Mkemi sifa na kiki za kijinga achana nazo, tunaitaka Yanga ya uwanjani na siyo ya mdomoni. Mpira siyo siasa unapinga kila jema. Hata ukikaa kimya mshahara utapata na kundi lako la makomandoo mtasimamia tiketi tu.
Msemaji wa Simba Haji Manara alitoa rai kwa wapenzi na mashabiki wa Simba kutoizomea Yanga. Alisema kuwa, hakuna nchi yoyote duniani ambayo mgeni anashangiliwa. Akawaasa wana Simba kuwa kama mtu akiona inamshinda kuishangilia Yanga bora akae kimya kwenye jukwaa kuliko kuipa support Shelisheli. Huo ni mwanzo mzuri kuelekea kwenye ustaarabu.
Kinyume chake, fyatu wa soka Bw. Mkemi ambaye hadi leo anaamini kuwa lazima upinge kila kitu anachosema mpinzani wako kama ilivyo kwenye siasa. Mkemi, sina hakika kama alienda na kichwa chake maana nimesikia sound clip tu, amewataka Yanga kubaki katika ushenzi wa utamaduni mbovu usioleta ushindani na unaotaka upande mmoja kutofurahia mafanikio ya upande mwingine.
Kizazi kile cha kuamini matunguri na wahubiri chuki kimepita, hiki kizazi cha wastaarabu tunataka kuona soka lenye tija na mshikamano.
Mkemi sifa na kiki za kijinga achana nazo, tunaitaka Yanga ya uwanjani na siyo ya mdomoni. Mpira siyo siasa unapinga kila jema. Hata ukikaa kimya mshahara utapata na kundi lako la makomandoo mtasimamia tiketi tu.