Kiki za kijinga za Mkemi

Kiki za kijinga za Mkemi

kilimbamula

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2015
Posts
1,792
Reaction score
853
Wiki hii tutashuhudia wawakilishi wetu kimataifa Simba na Yanga zikijitupa uwanjani kucheza mechi za kimataifa. Yanga leo itacheza na Washelisheli na kesho Simba itacheza na Wadjibuti katika vikombe tofauti.

Msemaji wa Simba Haji Manara alitoa rai kwa wapenzi na mashabiki wa Simba kutoizomea Yanga. Alisema kuwa, hakuna nchi yoyote duniani ambayo mgeni anashangiliwa. Akawaasa wana Simba kuwa kama mtu akiona inamshinda kuishangilia Yanga bora akae kimya kwenye jukwaa kuliko kuipa support Shelisheli. Huo ni mwanzo mzuri kuelekea kwenye ustaarabu.

Kinyume chake, fyatu wa soka Bw. Mkemi ambaye hadi leo anaamini kuwa lazima upinge kila kitu anachosema mpinzani wako kama ilivyo kwenye siasa. Mkemi, sina hakika kama alienda na kichwa chake maana nimesikia sound clip tu, amewataka Yanga kubaki katika ushenzi wa utamaduni mbovu usioleta ushindani na unaotaka upande mmoja kutofurahia mafanikio ya upande mwingine.

Kizazi kile cha kuamini matunguri na wahubiri chuki kimepita, hiki kizazi cha wastaarabu tunataka kuona soka lenye tija na mshikamano.

Mkemi sifa na kiki za kijinga achana nazo, tunaitaka Yanga ya uwanjani na siyo ya mdomoni. Mpira siyo siasa unapinga kila jema. Hata ukikaa kimya mshahara utapata na kundi lako la makomandoo mtasimamia tiketi tu.
 
Umeenda vizur umekosea na wewe ulipoingiza kupinga kila kitu ktk siasa ushamezeshwa jambo zur halipingwi yanayopingwa yote mouvu huna tofauti na mkemi umeongea kwakua halijagusa upande uupendao yote kwa yote mkemi ni mshanba.
 
Ametia aibu sana.

Anataka aonekane na uchungu sana na Yanga.
 
Kwa sababu Haji kasema, basi aungwe mkono tu?
Hivi Kwa nini hawezi kuongelea issue za Simba bila kuingiza Yanga?
Kwa nini asihamasishe wana Simba waende kuipa support timu yao Jumapili akaishia hapo. Mipango ya Yanga inamhusu nini?
 
Wiki hii tutashuhudia wawakilishi wetu kimataifa Simba na Yanga zikijitupa uwanjani kucheza mechi za kimataifa. Yanga leo itacheza na Washelisheli na kesho Simba itacheza na Wadjibuti katika vikombe tofauti.

Msemaji wa Simba Haji Manara alitoa rai kwa wapenzi na mashabiki wa Simba kutoizomea Yanga. Alisema kuwa, hakuna nchi yoyote duniani ambayo mgeni anashangiliwa. Akawaasa wana Simba kuwa kama mtu akiona inamshinda kuishangilia Yanga bora akae kimya kwenye jukwaa kuliko kuipa support Shelisheli. Huo ni mwanzo mzuri kuelekea kwenye ustaarabu.

Kinyume chake, fyatu wa soka Bw. Mkemi ambaye hadi leo anaamini kuwa lazima upinge kila kitu anachosema mpinzani wako kama ilivyo kwenye siasa. Mkemi, sina hakika kama alienda na kichwa chake maana nimesikia sound clip tu, amewataka Yanga kubaki katika ushenzi wa utamaduni mbovu usioleta ushindani na unaotaka upande mmoja kutofurahia mafanikio ya upande mwingine.

Kizazi kile cha kuamini matunguri na wahubiri chuki kimepita, hiki kizazi cha wastaarabu tunataka kuona soka lenye tija na mshikamano.

Mkemi sifa na kiki za kijinga achana nazo, tunaitaka Yanga ya uwanjani na siyo ya mdomoni. Mpira siyo siasa unapinga kila jema. Hata ukikaa kimya mshahara utapata na kundi lako la makomandoo mtasimamia tiketi tu.
Kwa kuwa Haji kasema, basi wengine wote waitikie tawile?
 
Manara ameujua uzalendo baada ya Simba kurudi kwenye michuano ya kimataifa!? mbona hakuyasema hayo miaka mi5 iliyopta wkt mashabiki wa simba walipokua bize kununua jezi za TP Mazembe, Medeama n.k???
 
Hujielew ww ukwer ndohuo sisi haruwezi kushabikiwa na wanafki hata skumoja uzalendo na utaifa kwenu kila mtu atavuna alicho kipanda huezi kusaidia kumulima kwamwenzio halikua kwako kuna majani utakua makuzi!!!
 
Manara aache unafiki uzalendo unaanza lini?

Manara aendelee kujikita kuwajibu waandishi wa habari tu na kudai point FiFA.

Mbumbumbu hovyo sana.
 
Kwnn haya maneno yamekuja mwaka huu na hayakuwepo kabla?

Ww na manara huna tofauti ulopokaji tu
 
Kwa sababu Haji kasema, basi aungwe mkono tu?
Hivi Kwa nini hawezi kuongelea issue za Simba bila kuingiza Yanga?
Kwa nini asihamasishe wana Simba waende kuipa support timu yao Jumapili akaishia hapo. Mipango ya Yanga inamhusu nini?
Kwani huyo Mkemi hakuzungumzia ya Yanga bila kutaja Simba? Kweli Nyani haoni Kundule
 
Kwani huyo Mkemi hakuzungumzia ya Yanga bila kutaja Simba? Kweli Nyani haoni Kundule
Alilazimika kumjibu huyo mpuuzi wenu. Huwa unasikia press conference ya Yanga wakiongelea Simba katika hali ya kawaida?
 
Mwaka huu mikia ndo mnakumbuka uzarendo mhuuu mikia wote mkapimwe mkojo
Uzalendo na mikia itakuwa laana kubwa. Waende uwanjani kuizomea Yanga wakipenda lakini wasiipangie Yanga nini cha kufanya.
 
Manara ameujua uzalendo baada ya Simba kurudi kwenye michuano ya kimataifa!? mbona hakuyasema hayo miaka mi5 iliyopta wkt mashabiki wa simba walipokua bize kununua jezi za TP Mazembe, Medeama n.k???
Better late than never. Inawezekana kwamba kiini cha kauli ya Manara ni kuikinga Simba dhidi ya kuzomewa na Yanga ilivyokuwa Simba ndiyo inacheza mwisho. Inawezekana bado nyoyo za Manara na baadhi kubwa ya Wanasimba hazifurahii kutoizomea Yanga. Lakini si vibaya heri kuzaliwa kutoka ndani ya tumbo la shari. There is nothing wrong in doing the right thing.
 
Sisi Yanga tumetumia mara moja tu uwanja wa taifa, ila Simba wameutumia mara mbili, Nyambafuu mkemi.
Simba wameutumia mara mbili kwa siku moja ama siku tofauti, leo mkienda pale tayari mtakuwa mmetimiza Siku mbili.
Nyamafuuu mkemi, Simba walivumilia sana.
 
Sijawahi ona timu, iliyolegea kama Saint Louis. Hii Yanga nayo itatolewa mapema tu, timu mmeizidi umiliki wa mpira kwa %72 halafu hukuna goli, hii timu inafungwa na hata timu ya daraja la pili,
nashangaa Yanga wanapata shida kuwafunga hawa.
 
Back
Top Bottom