safuher
JF-Expert Member
- Feb 11, 2019
- 11,837
- 17,412
Sasa hivi ili uwe mwana CCM wa kweli na mzalendo basi ni lazima ukitetee chama chako cha CCM dhidi ya Wapinzani na kuwapinga katika hoja zao.
Jambo hili linafanya wapinzani wahangaike katika kukosoa mambo ya maendeleo kweli wakati huo chama tawala wanahangaika katika kusifia tu na kuwajibu wapinzani.
Itakapofikia hatua ya chama kuwa kimoja hapo sasa hakutakuwa na mpinzani wa kunyooshewa vidole ili wewe mnyoosha vidole uonekane unajali maslahi ya chama na taifa.
Hapo sasa ndipo watu wa chama hiko watatafuta nafasi ama cha kusema ili waonekane wazalendo wa kweli katika nchi ama katika chama.
Hapo sasa ndipo ukosoaji wa ndani ya chama utaanza na watu wataanza kukosoa ili waonekane wanapenda maendeleo ya kweli.
Kila mmoja atataka kuongea aonekane kaongea na mtaka maendeleo, jambo hili litafanya mambo mawili yatokee.
1. Ikiwa rais aliyeko atakuwa ni dikteta na mgumu atawafukuza uwanachama hawa watu kwa sababu ni kikwazo katika tawala yake.
Na hii inaweza kupelekea kuundwa kwa chama kingine tena cha upinzani ambacho kitakuwa na vikwazo vingi sana kutokana na asili yake ile ilikotoka.
2. Ikiwa ni raisi poa atamuacha aendelee huyu mtu na atazidi kukubalika na wanachi na hapo wengine wataona kuwa kumbe hii ni njia ya kukubalika kwa wanachi na chama changu hakichukui hatua yeyote,na hapo wengine wataanza kujitokeza kuanza kukosoa zaidi na zaidi.
Jambo hili linafanya wapinzani wahangaike katika kukosoa mambo ya maendeleo kweli wakati huo chama tawala wanahangaika katika kusifia tu na kuwajibu wapinzani.
Itakapofikia hatua ya chama kuwa kimoja hapo sasa hakutakuwa na mpinzani wa kunyooshewa vidole ili wewe mnyoosha vidole uonekane unajali maslahi ya chama na taifa.
Hapo sasa ndipo watu wa chama hiko watatafuta nafasi ama cha kusema ili waonekane wazalendo wa kweli katika nchi ama katika chama.
Hapo sasa ndipo ukosoaji wa ndani ya chama utaanza na watu wataanza kukosoa ili waonekane wanapenda maendeleo ya kweli.
Kila mmoja atataka kuongea aonekane kaongea na mtaka maendeleo, jambo hili litafanya mambo mawili yatokee.
1. Ikiwa rais aliyeko atakuwa ni dikteta na mgumu atawafukuza uwanachama hawa watu kwa sababu ni kikwazo katika tawala yake.
Na hii inaweza kupelekea kuundwa kwa chama kingine tena cha upinzani ambacho kitakuwa na vikwazo vingi sana kutokana na asili yake ile ilikotoka.
2. Ikiwa ni raisi poa atamuacha aendelee huyu mtu na atazidi kukubalika na wanachi na hapo wengine wataona kuwa kumbe hii ni njia ya kukubalika kwa wanachi na chama changu hakichukui hatua yeyote,na hapo wengine wataanza kujitokeza kuanza kukosoa zaidi na zaidi.