Kikwete afanya mabadiliko makubwa ya Baraza la Mawaziri - Aprili 2012


Aishushe dollar kwanza ndio tumkubali!
Maana nilitaka kuagiza gari lakini nimeshindwa bcoz of this.
 
.....Imekula kwake maana mapambano yake yote ilikuwa anataka apate wizara ya nishati na madini......JK kampiga chenga kampeleka Elimu ya JUU Sayansi na Teknologia ........hana la kufanya alitaka sana sana sana sana Nishati na Madini!!!!!!!!period!!!!anatamani akatae ila hana uwezo!!!!
 
Hili ndio baraza bovu kuwahi kutokea TZ toka Uhuru,

Halitoweza kuleta manufaa yoyote kwa Watz kwa kuwa wengi ya walioteuliwa kuwa mawaziri

wanapokea amri nje ya serikali na sio kwa JK.

JK umedanganywa ukadanganyika.

Soon utagundua haya, tulikushauri hukushaurika.....


Another bad day.
 
Hawa hapa

Sofia simba,Kawambwa,Nagu,Ghasia,Wasira,Maghembe,Malima,Kombani..........!

Nafikiri wao ni lazima wawe mawaziri popote ambapo JK ni rais.
 
Mwenyewe JK anaona amefanya mageuz makubwa kwell? Hapa changa la macho hamna jipya
 
KIKWETOMICS HUAMSHA MASWAHIBA KAMA BINTI SAADA MKUYA TOKA JALALANI KUSIKOJULIKANA NA KURUDI KITANDANI WAKIWA MAMILIONEA NDANI YA MASAA TU KATIKA SIKU NA BADO KAULIMBIU BADO NI ILE ILE YA 'SERIKALI HAINA FEDHA'

Huu ndio uhalisia wa KIKWETOMICS na ujenzi wa uchumi wa maswahiba wake kila mahali kwa maumivu zaidi ya walipakodi kwa furaha ya wateule wachache.

Leo hii Ijumaa, kumetokea ajabu ya mwaka kwamba Bibie Saada Mkuya leo hii ni mwanamama aliyeamka kitandani mwake asubuhi ya leo akiwa ni MAMA WA NYUMBANI na kufika jioni tu anavyovua viatu kurudi kulala akawa amerejea na makontena mawili mazito ajabu iliojaa neema zisizohitajika na familia nyingi zetu hizi za walalahoi.

Mwana mama huyu hatokaa asahau siku hii ya Ijumma Mei 04, 2012 katika maisha yake ambapo aliamka kabwela na kurudi kitandani na funguo zote za U-MILIONEA WA CHAPU CHAPU kama Maige kabla hakujakuchwa kwa serikali ya CCM hii kwa kudondokewa na manemane toka angani kwa maana ya: (1) li-kontena futi 20 la Ubunge viti maalum, na hata kabla hajamaliza kutaharuki juu ya hilo mara mara (2) kukamdondokea tena gukokontena hugo futi 60 la uwaziri tena wa fedha za walalahoi wa nchi hii.

Nguvu mpya, kasi mpya na ari mpya 'kwa kila Mtanzania' kuukwaa uchumi unaopaa angani!!!
 
Huu ni Uvivu wa kufikiri,na kupeana Ulaji!katika karne hii bado tunakuwa na post kama hii?Hivi hata mwenye anajitambulishaje kwa Wageni?am minister of Cross Cutting Issues?wenye kujua kimombo help me plz!
 
The way the cookie crumbles at Tanzania...

Hili ni baraza la lala salama....
 
JK amenifurahisha kuwapiga chini akina Alhaj na Hijjat na kuwaingiza watu wanaomwabudu Mungu aliye hai eg Mkullo out, Mgimwa ndani.
 
Sasa ZITTO KABWE ndio Mwisho? na sasa JANUARY MAKAMBA kaupata Uwaziri pia;
 
Mabadiliko makubwa yako wapi wewe acha ushabiki wa kisiasa sura nyingi ni zilezile
 
Migulu Nchemba nasikia alikua ana vizia vizia .... teh teh teh
 
huyu waziri wa habari na michezo wa sasa, alikua naibu waziri wa habari na mchezo kabla, alivyokua bunge juzi alikua anajibu hoji ya wabunge kuhusu soka ya tanzania, akasimama akasema kua taifa stars imeshawahi kushinda makombe 7, na akataja na timu zingine na vikombe walivyoshinda baada ya kumaliza kuongea akasimama mjumbe mmoja akamsahihisha akamwambia taifa stars haijashinda makombe 7 ila ni matano. Nikawa najiuliza yani huyu amepewa tu report na wasaidizi wake hata hakuifanyia research aone kama kila kitu humu ndani kina ukweli yeye kachukua tu report kaenda bungeni kuisoma...:wacko: sasa huyu naibu waziri wa michezo ambae alikua hata hajui taifa stars imeshashindaga makombe mangapi sasa hivi ndio kapewa uwaziri wa habari na michezo....haki ya naniii..it can only happen in bongo:eek2:
 
Haihitaji kuwa na elimu Kuubwa kufikiri, hebu angalia safu kubwa aliyonayo JK ya wabunge wa chama tawala yaani CCM ambao kikatiba hao ndio haswa waliotakiwa kuteuliwa kuwa mawaziri, namaanisha miongoni mwao. Lakini imembidi raisi ateue wabunge wengine na hapo hapo kuwapa nafasi za uwaziri, nini mtizamo wa hao ambao tayari wamekuwa wakikitumikia chama bungeni lakini ameshindwa ama kuwa na imani nao au pengine amequestion uwezo wao wa kudeliver. Ningekuwa Mbunge kwa tiketi ya CCM kwa kweli wangenisamehe coz ningejiuzulu. Hivi hao waliopata Ubunge wamekwisha kula kiapo? hadi wamepewa uwaziri?
 
Wanajamii, nashindwa kuelewa. Waziri asiye na wizara maalu anateuliwa kufanya shughuli gani? Ofisi yake inakuwapi? Anawajibika kwa nani? Analipwa mshahara kufanya kazi zipi? Naomba ufafanuzi.
 

Mkuu unadhani nyarandu amesomea wanyamapori?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…