Elections 2010 Kikwete akumbana na zomeazomea Mbeya

Elections 2010 Kikwete akumbana na zomeazomea Mbeya

mrefu36

Member
Joined
Aug 16, 2010
Posts
72
Reaction score
22
Mjini Mbozi tukio la mgombea ubunge kuzomewa lilimkumba Dk Lucas Siyame baada ya kuitwa jukwaani na Kikwete ili awasalimie wananchi baada ya kumaliza hotuba yake fupi kutokana na kuwa na mkutano mwingine kwenye mji mdogo wa Vwawa wilayani Mbozi ambao, hata hivyo, uliahirishwa hadi leo asubuhi.
"Sipo peke yangu, jamani nawaombea kura pia madiwani, na mbunge,’ alisema Kikwete lakini kauli hiyo ilipokewa na kelele za wananchi waliokuwa wakipiga kelele kusema “maji, maji, maji, hatutamtaki huyo.”
Wananchi hao walipiga mayowe hayo huku wakionyesha ishara ya vidole viwili ambayo ni alama ya Chadema, hali iliyomaanisha kuwa wanamuunga mkono mgombea wa chama hicho cha upinzani.
Upepo wa kisiasa kwenye mji huo haujaikalia vizuri CCM kutokana na hali ilivyojionyesha dhahiri kwenye mkutano huo. Wakati baadhi ya watu walionekana kumkubali Kikwete, wengine walikuwa wakipiga miluzi na baadhi kuonyesha ishara ya vidole viwili.
 
HABARI NDIYO HIYO NA HUKO NDIYO MBEYA wamechoka kudanganyika..............HATUKATAI KUDANGANYWA LAKINI KAMA NI KUDANGANYWA KILA MWAKA HIYO HAIOWEZEKANI..........WANAMBEYA WANAONESHA KWA VITENDO NA HUKO KWINGINE JE...KAzi kwenu.
 
Mjini Mbozi tukio la mgombea ubunge kuzomewa lilimkumba Dk Lucas Siyame baada ya kuitwa jukwaani na Kikwete ili awasalimie wananchi baada ya kumaliza hotuba yake fupi kutokana na kuwa na mkutano mwingine kwenye mji mdogo wa Vwawa wilayani Mbozi ambao, hata hivyo, uliahirishwa hadi leo asubuhi.
"Sipo peke yangu, jamani nawaombea kura pia madiwani, na mbunge,' alisema Kikwete lakini kauli hiyo ilipokewa na kelele za wananchi waliokuwa wakipiga kelele kusema "maji, maji, maji, hatutamtaki huyo."
Wananchi hao walipiga mayowe hayo huku wakionyesha ishara ya vidole viwili ambayo ni alama ya Chadema, hali iliyomaanisha kuwa wanamuunga mkono mgombea wa chama hicho cha upinzani.
Upepo wa kisiasa kwenye mji huo haujaikalia vizuri CCM kutokana na hali ilivyojionyesha dhahiri kwenye mkutano huo. Wakati baadhi ya watu walionekana kumkubali Kikwete, wengine walikuwa wakipiga miluzi na baadhi kuonyesha ishara ya vidole viwili.

Huh!
Yawezekana wameerevuka hawa wananchi!
Huenda hatimaye wameona njia!!

HOngera wajomba na shangazi zangu!..huh!
 
Kikwete kweli hajui kusoma ala nyakati.
Huko Mbeya watu walilala barabarani asipite, wakampiga na mawe.
Bado anajipendekeza ili iweje?
Awaachie CHADEMA wachukue mkoa wao.
Mjini Mbozi tukio la mgombea ubunge kuzomewa lilimkumba Dk Lucas Siyame baada ya kuitwa jukwaani na Kikwete ili awasalimie wananchi baada ya kumaliza hotuba yake fupi kutokana na kuwa na mkutano mwingine kwenye mji mdogo wa Vwawa wilayani Mbozi ambao, hata hivyo, uliahirishwa hadi leo asubuhi.
"Sipo peke yangu, jamani nawaombea kura pia madiwani, na mbunge,' alisema Kikwete lakini kauli hiyo ilipokewa na kelele za wananchi waliokuwa wakipiga kelele kusema "maji, maji, maji, hatutamtaki huyo."
Wananchi hao walipiga mayowe hayo huku wakionyesha ishara ya vidole viwili ambayo ni alama ya Chadema, hali iliyomaanisha kuwa wanamuunga mkono mgombea wa chama hicho cha upinzani.
Upepo wa kisiasa kwenye mji huo haujaikalia vizuri CCM kutokana na hali ilivyojionyesha dhahiri kwenye mkutano huo. Wakati baadhi ya watu walionekana kumkubali Kikwete, wengine walikuwa wakipiga miluzi na baadhi kuonyesha ishara ya vidole viwili.
 
Hayo ni ya kawaida kwenye msongamano. But mi ninavyojua mbozi na vwawa ni jimbo la Godfrey Zambi sa sijui SIyame alikuwa anpigiwa debe kivipi ye ni wa mbozi magharibi unyamwangani.
 
Mbeya wamechoka!!! CCM kwishney!!

Hongereni wana mBeya kwa kustua, na kuchukua tahadhari!! Hawa CCM ni donda ndugu. Haliponi ng'oooo.....

Chagua Slaa, chagueni mbunge wa CHADEMA.
 
Hayo ni ya kawaida kwenye msongamano. But mi ninavyojua mbozi na vwawa ni jimbo la Godfrey Zambi sa sijui SIyame alikuwa anpigiwa debe kivipi ye ni wa mbozi magharibi unyamwangani.

Hili lilitokea katika mji mdogo wa Tunduma kwenye Jimbo la Mbozi Magharibi.
 
Inatakiwa nchi nzima kuwazomea hao mafisadi, kila wanapopita. Juzi Jangwani walijaribu kukatisha matazngazo wakakutana na Peoples Power
 
Naona watu wengi hawajaielewa habari vizuri. Nashauri mnunue gazeti la mwananchi limeiandika vizuri kuliko huu umbeya uliopo hapa, Au ndo kujipa matumaini?
Kama mjuavyo waandishi wetu wa habari wanaandika ili kuuza gazeti, Kichwa cha habari hakisanifu habari kamili ilivyo ndani. Sitaki kusema mengi, badi ni mchana nenda tu kanunue gazate achana na hii habari iliyochakachuliwa.
 
Kikwete amewagawa sana watu wa mkoa wa MBEYA tangu aingie madarakani, na kama Chadema wataitumia vizuri nafasi hii, basi wana uwezo wa kupata kura nyingi sana za urais mkoani Mbeya. kuhusu wabunge, Mbeya wana kawaida ya kuchagua mtu na si chama, kwa mfano si rahisi kumshinda Mwandosya na Mwakyembe kwenye majimbo yao.
CHADEMA wekeni nguvu pale, Mbeya walishamchoka Kikwete siku nyingi.
 
Back
Top Bottom