Kikwete alivyoondoka Monduli chuo cha Jeshi kwa misukosuko

Kikwete alivyoondoka Monduli chuo cha Jeshi kwa misukosuko

Jakaya Ana Historia ya kusisimua kuliko Mwanasiasa yoyote hapa Nchini!

Mabonde na Milima yake ya Kisiasa akiamua kuandika bila ya kuficha kitu huenda Kitabu chake kitakuwa reference Muhimu kwa Siasa za ukanda wetu lakin Tatizo la Yule Mkwere ni Mzuri sana wa kuzungumza sio kuandika [emoji12][emoji12]
 
Kipindi hicho mkuu wa chuo alikuwa Gideon Sayore, Kikwete alikuwa ni mmoja wakufunzi wa siasa chuoni hapo.

Sasa ilikuwa hivi,
Mzee Sayore alikuwa anafuga ng'ombewengi pamoja kufanya shughuli za kilimo kwawingi wakati huohuo akiwa mkuu wa chuo cha kijeshi Monduli.

Hivyo basi baada ya kuona ng'ombe wanatoa maziwamengi mno na mazao yametapakaa mashambani,. akaamua kuwa awe analiuzia jeshi mazao kama vile maharage na mahindi pamoja na maziwa na nyama kutoka kwenye mifugo yake.......na pesa anachukua yeye mwenye mazo.

Aliendelea kufanya hivyokwa kipindi kirefu tu.. ikiwa ni kama sehemu yake ya maisha....

Sasa bwana ,,kumbe Kikwette (JK) ilikuwa inamuuma sana sana, yaani mno! sasa haieleweki kama ilikuwa kweli ni kwa uzalendo ua wivu tu....akaandika barua kwa raisi kipindi hicho JK Nyerere.

Katika barua hiyo akaandika lawama nyiingi mno na majungu mengi sana dhidi ya Sayore, akimwita bepari, bwenyenye, mnyonyaji n.k huku akisema hafai kuwa mkuu wachuo hicho kwakuwa navunja miiko ya uongozi na mambo mengine meengi (si mnamjua JK anavyojua kupiga fitna!)...

Basi bwana, akamalizia mwisho kwakujiandika jina lake na sahihi yake huku akijiita mzalendo kamili barua ikapostiwa ikiwa imeadresiwa kwa rais wa nchi wakati huo!......

Mwalimu, aliipata barua ile aliifungua akaisomaaaa kisha akapiga hesabu zake....sijui aliwaza nini mzee yule, akaihifadhi ile barua ikaa sana ofini kwake bila kuchukua uamuzi wowote.

Siku moja alipokuja mkuu wa majeshi wakati huo "General Mtukula" (David Musuguli) ofisini kwa Mwalimu eaisi kipindi hicho, mwalimu akampa ile barua kutoka kwa Kikwete "akisema hayo ni maMbo yenu kayamalizeni hukohuko".

Basi bwana ile barua Mkuu wa majeshi alikaa nayo muda hivi kwenye makabrasha yakee...., sasa siku mija alikuja Mkuu wa chuo cha kijeshi Monduli(Sayore) Dar es salaam kufanya shughuli za kikazi akaenda hadi ofisini kwa Mkuu wa majeshi.

Baada ya shughuli kwisha na Sayore akiwa anajiandaa kwenda Monduli Mkuu wa majeshi alimwita, akampa ile barua ya Kikwete aliyomwandikia rais!!....

Sayore akaisoomaaa we akashangaa mno!! na akafura kwa hasira yule mmasai...., akuliza mwalimu kasemaje? Akaambiwa mwalimu kasema yamalizeni wenyewe!!.... Akasema naam, na akaondoka na ile barua hadi Monduli...

Alipofika tu yule mmasai aliitisha kikao cha wakufunzi wote na wakuu wengine pale chuoni, wakati wanajikusanya kwenda kwenye chumba cha mkutano yeye aliamua kwenda kutoa copy ile barua ya Kikwete, kopi nyingi idadi sawa na wajumbe wa mkutano ule....

Alipoingia mkutanoni akawaona wakuu na wakufunzi wote wameketi wakimsubiri wajue alicho waitia,.. akaanza kwa kuwauliza..jamani kama kuna mtu ana matatizo, au anaona kuna jambo haliendi sawa anyooshe mkono na saemekinacho mkereketa......watu wote wakawa kimya huku wengine wakisema hamna mkuu akiwemo Kikwette!!!

Basi bwana, tumalizie mkasa huu wa mkwere...

Sayore akaanza kuwagawia zile nakala (copies) za ile barua ya Kikwete kwenda kwa rais akawagawia wooote including Kikwete!!! Huku yule mmasasi Sayore akiwa amefura kwa hasira, macho mekunduuu! Akagonga ngumi juu ya meza kwa hasira na kusema someni hiyo barua!! kisha akatoka na kusema anakuja muda si mrefu...

Hapo Kikwete akajua kifo chake kimefika, akikumbuka macho ya yuile mmasai! akatetemeka macho yakamtoka lip! kwa woga!.. na wenzie wakamwanzishia zogo mle ndani......

Alichokifanya ni kuondoka haraka pale kikaoni wenzie wakajua bado yupo chuoni, kumbe safari ya Dar ikawa imeanza...!! Jamaa alitembea uchochoroni kwa muda mrefu sana huku akiogo kabisa kuingia barabara ya kuu...

Mashuhuda wanasema yule bwana akaja kupanda lift ya gari za vyama vya ushirika maeneo ya USA RIVER, hakukumbuka kubeba mzigo wowote!! Just imagine kutoka Monduli hadi hapo jamaa aliteseka sana... lakini yeye hakujali, cha muhimu ilikuwa kusalimisha maisha yake......

Basi huo ndiyo ukawa mwisho wa JK Monduli,........... hukurudi akaja Dar na kupangiwa kazi nyingine na chama... lakini alikuwa anamlaani sana Nyerere eti kwanini alimfanyia vile!!

Hicho ndicho chanzo cha JK kumchukia mwalimu na kugoma katakata kumwita baba wa taifa hadi leo! Yeye humwita mzee Nyrere tu au mwalimu baasi...na mara chache akiwa nje ya nchi humwita 'Father of our Nation', lakini ni pale anapotaka kupigiwa makofi kwa nukuu za Mwalimu....

**Ndugu zangu hiki ni kisa cha ukweli kwa 100%, inawezekana uandishi wangu ukawa na upungufu, lakini niemekipata kutoka watu mbalimbali waliowahi kuwa karibu sana na mkasa huu...
Mkwere alichukia Maofisa Cadet kufanyishwa kazi za kusafisha mabanda ya kuku na nguruwe, wengine wakiwa waislam.
JK kwa fitina noma!!
 
dU...hII NI KALI!
Ingekuwa ni sasa tungepata hiyo barua ikawa scanned na kuwekwa hapa!

Usikute Mkapa alipokuwa anasemea "wivu wa kike" alikuwa kiaina anamng'ong'a jamaa!

Kumbe hakuondoka kwa mema Monduli huyu!...nitafuatilia kisa hiki maana kuna wazee waliokuwa naye enzi hizo Monduli!
Mkuu upo?
Habari ATown.
Manyara ni poa.
 
Jakaya Ana Historia ya kusisimua kuliko Mwanasiasa yoyote hapa Nchini!

Mabonde na Milima yake ya Kisiasa akiamua kuandika bila ya kuficha kitu huenda Kitabu chake kitakuwa reference Muhimu kwa Siasa za ukanda wetu lakin Tatizo la Yule Mkwere ni Mzuri sana wa kuzungumza sio kuandika [emoji12][emoji12]
That is where the difference is...aandike tena aandike ukweli mtupu ili vizazi vyetu vijifunze. Wanaoandika ni wachache sana kama Yule kijana anayeandika harakati za wanaofukuzwa chuo kwa utukutu
 
Kama umezaliwa miaka ya 90 utajuaje unaona miaka ya 70 na 80 kama zamani sana, kopi zilikuwa zinatolewa tangu enzi za uhuru tulikuwa tunatumia carbon paper najua huzijui, nyie watoto wa enzi za photocopy na scanner.
Hawa vijana hata ukiwaambia enzi hzo sisi tunafanya mitihani inaandikwa ubaoni na chaki na kama ubao mdogo mwalimu anasubiri mmalize anafuta tena na tena au ukikuta mwl mwandiko wake wa kitaalamu anabananisha mtihani wote ubaoni. Sidhani kama wataamini
 
Naona mambo ya siasa tushazungumza sana.

Ngoja niingize human touch, light touch story. Memoirs of Al-Watan.

Hii story ilivyomtaja General Sayore imenikumbusha Nancy Sayore enzi za ujana wangu.

Katika pitapita zangu nikawa nakatiza Namanga,mara nikapita Kimicho, watoto wa Oysterbay wanakutana wanakula Ice Cream na mapochopocho, mimi nakatiza tu kuangalia vitu madukani.

Mara namuona Nancy anatoka Kimicho. Wakati huo ndo scandal yao ya email na Heri "DJ Red" Bomani ndo kwanza imetokea. Vijana waliokuwa wanafuatilia mambo ya Dar miakaya mwisho ya tisini watakumbuka.

Mimi Nancy alikuwa kama kichaa wangu kwa sababu kuna mshkaji alipumzika. Ndipo nilipojua kwamba yule mtoto kwa nje anaonekana mpole lakini kichaa kama baba yake. Mimi nilikuwa jioni kisomo flani siku hizo nashika time zangu kwa hiyo sikuwa na mazoea naye sana, ila siku hiyo nilipomuona nikawa namsalimia "Mambo vipi Nancy?" Basi namuona mtoto wa kike anajiumauma, akasema "Poa tu, vipi wewe?". Nikamwambia poa tu.

Yeye anajua kwamba mimi najua scandal yake. Na mimi najua yeye anajua. Ila ikawa kama kuna an wakward moment.

Basi nikaamua kumpoza. Nikamwambia Nancy najua uko katika wakati mgumu sasa, ila wewe usijali sana watu wanavyosema, wewe focus kwenye mambo yako tu, tunaokujali na kukujua hatuwezi kupoteza urafiki wako kwa sababu ya wabongo kukuvunjia faragha yako.

Akafurahi sana akasema "You are so kind, that is the nicest thing I have heard". Akacheka sana.

Na mimi nikafurahi kumtuliza roho baada ya kuona alivyofadhaika.

Basi nikwa namuaga nishike hamsini zangu.

Na yeye akaniaga.

Kuangalia pembeni nikaona Nissan Patrol. Limefungwa vioo.

Halafu ndani kakaa General Sayore kumbe mda wote namchombeza Nancy mshua ananiangalia tu.

Nikasema du, sasa pale ningekuwa na tabia za maneno mbovumbovu kumsema vibaya binti huku sijajua Mzee Mzima ananiangalia sijui ingekuwaje.

Nikajifunza kwamba kuwa na kauli njema ni jambo zuri sana.
 
Na ile ya waitara?aligoma kwenda kumpigia saluti kikwete.
 
Alipokuwa anaondoka ,alikutana na mwanajeshi mwenzie mfupi kuliko wote wakati huu wakimwita Pimbi wa Monduli Abruhaman Shimbo.

Na kwa kuwa walikuwa marafiki kiasi kutokana na uislam wao JK aliamua kumueleza yote yaliyomkuta ndipo hapo Shimbo akamuonea huruma sana na kumuandikia kinot mjomba wake aliyekuwa anakaa Tengeru ili amsaidie.

Basi JK alifikia Tengeru kwa mjomba wake Shimbo na hapo akapumzika siku kadhaa yule mzee alimpa nauli na JK akarudi Bagamoyo moja kwa moja kabla hajapangiwa Lindi kwenda kufanya kazi za chama. Ndio maana JK hasemi kitu kwa Shimbo analipa fadhila
Kumbe maneno yote kuna nukta muhimu ya UDINI ndani yake ee... Haya endeleeni lakini kumbukeni mtavuna mlichopanda.
 
Back
Top Bottom