Pathetic!....very unneccessary!JK akoshwa na ziara ya Ivory Coast
*Awaandalia chakula maalumu Golden Tulip
*Amwagia sifa Drogba, amkabidhi uzi wa Stars
*Awaombea watwae taji, aahidi Watz kuwashangilia
Mi ningeshangaa kama asingefanya hili! Kwani si ni mkuu wa kaya tunamzungumzia? Au!
Kuwaandalia chakula cha jiioni n.k ni mambo mema wala hakuna tatizo hapo na hicho alipaswa kufanya.
Hii kazi ya kuandaa chakula na kuwakaribisha ni kazi ya TFF na labda Waziri wa Michezo lakini sio rais wa nchi, amekwenda kwenye mechi inatosha.Wadau, mimi sioni tatizo lolote kuhusu chakula alichowaandalia Ivory Coast maana Kiafrika hilo ni jambo la kawaida kabisa ya kuwa mgeni anakaribishwa na kupewa chakula kizuri kabisa kinachioweza kupatikana kwa mwenyeji wake. Huo ndiyo ukarimu wa Kitanzania.
Unadhani hao wachezaji wanajali?Pili, nampongeza Rais kwa alichofanya, amewaonyesha wageni ukarimu wa Kitanzania hasa ukizingatia wachezaji wengi wa Ivory Coast wanatoka na kuishi Ulaya kwenye maisha ya kibinafsi na kichoyo, tena hata watu wa huko Afrika Magharibi wana tabia za ubinafsi-ubinafsi kwa hiyo hilo ni somo tosha kwa wageni wetu.
Ebo!! sasa kama mambo yenyewe ndio haya kazi ya Taifa Stars ni nini? Hizi nguvu tunazoziwekeza kwenye kutafuta ujiko na kujikomba komba tungewekeza kwenye kuijenga timu yetu ya Taifa basi tungekuwa mbali sana kisoka.Nne Wa-Ivory Coast, kwa kutambua ukarimu wetu wameahidi kuwa iwapo watatwaa kombe la CAN basi watalileta Tanzania. Kwa hiyo, tumeweza kuwa-impact.
Hiyo PR ukiizidisha sana inaonekana kama ni a** kissing.Mwsiho, pamoja na mapungufu yake nimegundua kuwa JK anajua sana PR na ndo maana huwa anapata favor ya ahadi za misaada anapotembelea ughaibuni ingawa kwa kweli misaada haitaweza kutusaidia sana iwapo hatutakaza buti dhidi ya ufisadi na kuhakikisha kinachopatikana kinafanya kazi iliyokusudiwa.
Kaka naona donge limekakaa! Pole sana!Kuwaandalia chakula cha jiioni n.k ni mambo mema wala hakuna tatizo hapo na hicho alipaswa kufanya.
Mimi kwangu nina ujumbe kwa CAG: Usisahau kukagua haya matumizi kama ulivyofanya kwa wale walimu maskini waliokuwa wanadai posho zao
uzi gani huo mpwa?ila....?ule uzi mweusi uko wapi?
MNAMUONEA MKWERE WA WATU!muacheni jamani.
kwenye hili mnamuonea
JK hajui ma star wakiondoka pale tu wameshamsahau na kinchi chake....waanafikiria mambo yao ya kuingiza pesa....baasi,angewaomba waje wawekeze kwenye ball kujenga academy....kama wameona tuna vipaji,,,,,,
Hii nchi kiboko hela za walipa kodi zinaunguzwa ukiuliza unaambiwa tunasaidia kuitangaza nchi. SMH!!!