Kikwete frustrated at the UN?


Uzuri wa Mkapa alikuwa anapitia spichi zake na kusahihisha. Unajua alikuwa mhariri wa Nationalist, na pia Kiingereza chake kilikuwa kinapanda kwelikweli.
Mwinyi alikuwa mwalimu (teacher) na pia hakuwa na makuu kama alivyosema FMES. Ukisikiliza spichi zake za Kiswahili utafurahi mwenyewe. Huyu mwenzetu kwanza anahitaji kutulia. Apitie spichi zake au afanye kama Bush anavyofanya: anapractice mbele ya maafisa wake kabla ya kuisoma hadharani. Public speaking is an art.
 
Public speaking is an art.

Mkuu you got it right, unajua kuna nilipokuwa College, Us tulikuwa tunalazimishwa kuchukua darasa la Speech and Communications,

na part of the class ilikuwa ni kuchagua hotuba ya kiongozi yoyote mashuhuri duniani na kuja kuisoma mbele ya darasa, ndipo nikajifunza hayo maneno yako hapo juu kuwa public speaking ni an art, kwa sababu kuna wanafunzi ambao ilibaikia kidogo waanguke pale mbele ya darasa, kuna waliokuwa wanang'ang'ania ukuta, kuna waliokuwa wanashikilia meza,

yaani hapa fundisho ni hotuba za kuwadaganya wananchi vijijini sio sawa na huko ma-UN!, wawe wanajitayarisha ikibidi basi wawalipe pros huko NY, wawaep mazoezi mbona serikali yetu inalipa kwa mambo mengine ya kijinga sana halafu wanaacha ya muhimu kama haya?
 
Mwandishi wa Ikulu

Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), Rais Jakaya Mrisho Kikwete ameyaonya mataifa ya Bara la Ulaya kuacha mtindo wa kuwadhalilisha viongozi wa Afrika, kupitia mfumo wa mpya wa utawala wa sheria wa kimataifa unaolenga kuwafungulia mashitaka viongozi wa Afrika, na kuwafikisha katika mahakama za kimataifa.

Rais Kikwete pia amesema kuwa Afrika inaunga mkono, moja kwa moja, mageuzi makubwa katika mfumo wa Umoja wa Mataifa (UN), ili mradi Bara hilo lipewe nafasi mbili zenye kura za turufu katika Baraza la Usalama la Umoja huo.

Mwenyekiti huyo wa AU pia ameutaka Umoja wa Mataifa kuongoza jitihada za kupunguza makali ya bei ya mafuta na bei ya chakula duniani, kama njia ya kuzilinda nchi changa zaidi, hasa zile za Afrika, dhidi ya makali ya bei hizo.

Rais Kikwete ametoa msimamo huo wa Afrika wakati anahutubia Mkutano wa 63 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo (Jumanne, Septemba 23, 2008) kwenye makao makuu ya Umoja huo mjini New York, Marekani.

Rais Kikwete alikuwa kiongozi wa 12 kuzungumza katika kikao cha mwaka huu cha UN yenye nchi wanachama 192 na alitoa msimamo wa Afrika baada ya ripoti ya utangulizi ya Katibu Mkuu wa Umoja huo, Ban Ki Moon uliofuatiwa na hotuba za Rais Luiz Inacio Lula da Silva wa Brazil, Rais George W Bush wa Marekani, Rais Nicolas Sarkozy wa Ufaransa, Rais Gloria Macapagal-Arroyo wa Philippines na Sheikh Hamad bin Khalifa Al-Thani wa Qatar.

Wengine waliozungumza kabla ya Mwenyekiti huyo wa AU ni Rais Daniel Ortega Saavedra wa Nicaragua, Rais Ellen Johnson Sirleaf wa Liberia, Rais Abdallah Gul wa Uturuki, Rais Cristina Fernandez de Kirchner wa Argentina, Rais Marc Ravalomanana na Rais Boris Tadic wa Jamhuri ya Serbia.

Katika hotuba yake ya kusisimua, iliyotolewa kwa uchangamfu mkubwa na kupokelewa vizuri, Rais Kikwete ameonya kuwa mtindo wa baadhi ya nchi za Ulaya kuwafungulia mashitaka kwa nia ya kuwakamata viongozi wa Afrika na kuwafikisha kortini kwa sababu mbali mbali ni hatua ya kuwadhalilisha viongozi hao.

“Kabla ya kumalizia, ninayo mambo matatu… Jambo la pili ni kuhusu mfumo mpya wa utawala wa kisheria wa kimataifa unaoendeshwa na nchi za Ulaya. Mfumo huu sasa umekuwa na silaha ya kuwadhalilisha viongozi wa Afrika,” amesema Raia Kikwete na kuongeza:

“Tulilijadili suala hilo katika kikao kilichopita cha Wakuu wa nchi za Umoja wa Afrika, na tunakusudia kuliwasilisha jambo hilo kwenye Umoja wa Mataifa, ili lichukuliwe hatua mwafaka.”

Kuhusu mageuzi ya Umoja wa Mataifa, Rais Kikwete amesema kuwa Afrika inaunga mkono moja kwa moja mageuzi hayo.

Hata hivyo, Rais ameongeza kuwa AU inaamini kuwa mageuzi katika UN hayawezi kuwa yamekamilisha bila kufanya mageuzi katika Baraza la Usalama la UN.

“Kwa upande wa Afrika, tumewaruhusu wawakilishi wetu wa kudumu mjini New York kuanzisha mjadala na pande zote zinazohusika kuhusu mageuzi ya Baraza la Usalama,” amesema Rais Kikwete.

Amesisitiza: “Hapa sasa nataka kusisitiza msimamo wa Afrika wa kuomba nafasi mbili za kudumu na zenye kura ya turufu, na mbili za kudumu bila kura ya turufu kwenye Baraza hilo. Matakwa yetu lazima yatiliwe maanani kwamba ni kweli kuwa Afrika linabakia Bara pekee lisilokuwa na uwakilishi wa kiti cha kudumu katika Baraza la Usalama pamoja na wingi wa nchi wanachama wa UN kutoka Afrika.”

Kuhusu ongezeko la bei za mafuta na chakula duniani, Rais Kikwete amesema kuwa ni kweli kuwa katika wiki za karibuni bei hizo zimeteremka kidogo, lakini bado ziko juu sana.

“Zahama ya bei za mafuta na chakula zikichanganywa na zahama inayokua kila siku katika masoko ya fedha duniani, inatupa kila aina wasiwasi sisi katika Afrika. Hatuwezi kusisitiza kiasi cha kutosha haja ya kusitisha mwelekeo huu. Tunaitaka jumuia ya kimataifa na mataifa makubwa katika uchumi wa dunia kuchukua hatua za haraka kurekebisha jambo hilo. Tunaamini kuwa Umoja wa Mataifa unatakiwa kuongoza mchakati wa hatua dhidi ya zahama hizo.”

Rais pia amezungumzia na kujadili kwa undani hali ya kisiasa na usalama katika Afrika ambako ameelezea jinsi Afrika inavyotatua matatizo yake, hali ya Darfur, hali ya Somalia, hali ya Mashariki kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), hali ya Zimbabwe, mahitaji ya maendeleo ya Afrika, hali ya Sahara Magharibi na mchakato wa Helsinki, ambao uliongozwa na wanachama wenza, Rais Kikwete na Rais wa Finland, Tarja Halonen.
 
Jasusi,FMES,

..sasa sijui hata tufanyeje.

..on paper, Kikwete is supposed to be the most competent and succesful president we have ever had.

..when you compare his background and experience with his predecesors you will definetely agree with me.

..URAISI na hata uwaziri hausomewi, therefore one has to draw frm his/her proffesional and life experiences and grow on the job. sasa Kikwete ni yuleyule wa siku zote tuliyemzoea.

..hata Mkapa alipoanza alikuwa akikandiwa kwa sababu ya kung'ang'ania hotuba za kuandikiwa hata kwenye mikutano ya hadhara kule jangwani. lakini baadaye mabadiliko tuliyaona.
 
Katika hotuba yake ya kusisimua, iliyotolewa kwa uchangamfu mkubwa na kupokelewa vizuri, Rais Kikwete ameonya kuwa mtindo wa baadhi ya nchi za Ulaya kuwafungulia mashitaka kwa nia ya kuwakamata viongozi wa Afrika na kuwafikisha kortini kwa sababu mbali mbali ni hatua ya kuwadhalilisha viongozi hao


Haya Bana!!!!
 

1. Mkuu hapo mwanzoni sina uhakika, ninaamini kwa kiasi kikubwa sana kuwa Kikwete, is doing a fine job kwenye AU, hili nililithibitisha hivi karibuni nilipohudhuria barbecue moja ambapo mabalozi karibu wote wa Africa UN, walikuwepo, karibu wote walikuwa na maneno mazuri sana ya kumsifia Kikwete na AU, ninakubali kwa 75%.

2. Ila nina tatizo sana kwamba he is the most successful na competent ever kwa taifa letu, labda kuna something missing hapo, ukiweke wazi zaidi!

3. Kikwete anahitaji kufanya mazoezi ya kuongea mbele ya wageni kwa sababu inachangia sana katika wageni kukuelewa as rais, ukisoma kitabu kimoja cha Kissinger, anasema kwamba aliokuwa waziri wa nje wa US, alikuwa na tabia ya makusudi kutayarishiwa kiti kirefu kuliko viongozi wengine aliokuwa akikutana nao, akidai kisaikolojia ilikuwa inampa an edge ya kumu-intimidate any counterpart wake, lakini anasema ni wa-Russia tu waliomshitukia walikuwa hawakubali hata siku moja huo mchezo wake,

Sasa kwa wazungu how rais wetu anavyoonekana mbele yao ni muhimu sana kwenye kumhukumu, hata kabla ya kuongea naye deal muhimu za taifa ajifunze namna ya kuongea mbele ya mataifa kwa kutumia lugha clear na inayoweza kueleweka kwa urahisi, kuliko sasa.
 
Mwandishi wa Ikulu

Katika hotuba yake ya kusisimua, iliyotolewa kwa uchangamfu mkubwa na kupokelewa vizuri, Rais Kikwete ameonya kuwa...

Mwandishi wa Ikulu ?

Hii ni press release ya Ikulu, au ni ripoti ya correspondent wa gazeti la mchana ambae yuko assigned Ikulu ?

Mwandishi wa Rais akitoa public statement inabidi iwe rasmi, na isiwe cheer leading and jaundiced like this comedy up here.
 
katika waliotoa hotuba jana aliyenifurahisha zaidi ni raisi wa Irani, yule jamaa ni very confident, haogopi kuwapiga nyundo viongozi wa serikali ya marekani kuhusiana na sera zao akiwa kule kule katika ardhi yao. kwa muono wake yule jamaa jembe analiita jembe na si kupindisha pindisha maneno!. jamaa anaipeperusha falsafa ya nchi yake bila woga wala haya!
 
Mnamuonea. Pale mahali panatisha! Halafu msisahau kuwa amefunga. Hawezi kunywa maji hata koo ikikauka.



..anaonewa duh!!,,,,teh teh...duh!!!!

..kikwete huhitaji kumuonea..anatia huruma ..hayupo serious hata siku moja...na bahati mbaya kachukuwa wasaidizi wa aina yake.....

akiwa foregn akifika marekani alikuwa anakesha night club ...sijui siku hizi kama FBI watamkubalia...maana ni head of state ...wao ndio responsible!!!
 

believe yake ni kwamba ukiwa mtoto wa mjini night club ni mahali pake.
Sasa tukirudi kwenye content ya Hotuba yake kuhusu Mataifa makubwa dhidi ya viongozi wa nchi za Afrika/ndogo, mimi naona hao Donors/nchi kubwa waendele tu maana wenyewe wameshindwa kujiheshimu kwa faida ya watu wao.
eg kama sio juhudi zao za kuwabania hela za kifisadi viongozi wetu hali , itakuwaje?
hata kama hizo nchi za magharibi etc wanafanya hivyo kwa maslahi yao atleast na sisi ndio tunapo ponea au kupunguza maafa/machungu.
 
FMES said:
Ila nina tatizo sana kwamba he is the most successful na competent ever kwa taifa letu, labda kuna something missing hapo, ukiweke wazi zaidi!

FMES,

..yah..you missed my point.

..Mwalimu Nyerere hakuwahi hata kuwa mwalimu mkuu msaidizi kabla ya kuwa Raisi.

..Kikwete ameshika nafasi mbalimbali ambazo zimemuandaa kuja kukabiliana na changamoto za Uraisi wa Tanzania. lakini mpaka sasa performance yake ni ZERO.

..nasema Kikwete kila sababu ya ku-succeed lakini ni he is letting himself and the nation down.
 
Sawa mkuu nimekupata, tena hands down sasa mkulu majuzi tu alikuwa DC, lakini anaenda tena DC, halafu atarudi tena NY, yaani this is incredible!

Na I have never seeen this before! I mean never!
 
..on paper, Kikwete is supposed to be the most competent and succesful president we have ever had.

..when you compare his background and experience with his predecesors you will definetely agree with me.


Distortions!

Nyerere aliongoza harakati za uhuru, pamoja na chama cha TANU. Na kabla hajawa Rais mwaka 62 alikuwa chini ya Governor General wa Tanganyika toka apewe uhuru. Kama vile quasi vice president. Experience ya nguvu hiyo kabla ya kuachiwa aendelee na madaraka kivyake mwaka 62.

Mkapa alikuwa foreign minister, balozi wa US, na Waziri sehemu nyingine kwa muda mrefu kuliko Kikwete.

Mwinyi alikuwa Rais wa Zanzibar. Alikuwa Interior minister wa Muungano. Alikuwa foreign envoy miaka kibao. Alikuwa makamu wa Rais.

Sasa utasemaje "on paper Kikwete is the most experienced and successful" ?

On paper Kikwete ame succeed nini ? Nitajie alicho succeed Kikwete "on paper" ?
 

tatizo they don't count watu kama sisi kuiweka hotuba hiyo yote na kuona jinsi ilivyotolewa badala ya kuripotiwa.
 

Kuhani,
Mbali tu ya kuwa Foreign Minister, Kikwete alikuwa ana miaka kumi ya kujiandaa kuwa rais. I would think huo ni muda tosha kabisa kujiandaa kwenye art ya speaking in public, no?
 
Kuhani,
Mbali tu ya kuwa Foreign Minister, Kikwete alikuwa ana miaka kumi ya kujiandaa kuwa rais. I would think huo ni muda tosha kabisa kujiandaa kwenye art ya speaking in public, no?

Ni kweli. Lakini kusema Kikwete ndie the "most experienced and succesful on paper" sio sahihi.


Mkapa aliwahi kuwa balozi UN? When was that? Na ni UN ipi hiyo?

Nilimaanisha US, sio UN.

Ahsante.
 
Matatizo ya Speech za Rais hayakuanza leo...Mwaka jana licha ya kuchelewa kwenye kikao cha UN pia alitoa Speech Nyepesi kupindukia..Hii Speech ya Juzi ilizungumzia mambo mengi,kilichotokea ni kubabaika na lafudhi ya kiswahili katika maneno ya kiingereza,Kuzungumza mambo mengi juu juu kwa wakati (muda) mdogo (dk 45).

Hotuba inayotolewa UN inatakiwa iwe nzito na inayofanana na Hadhi ya hapo mahali,Hiyo sio Hotuba yakuomba kura kule Tarime,au Hotuba ya Ufunguzi wa Daraja huko Songea,Hotuba hizi ndio zina hadhi ya akina Januari,lakini sio Hotuba zinazotolewa kwa watu waliobobea kwenye siasa Nzito.......zinataka watu waliopevuka kwenye Diplomasia na uwezo wa Lugha nyepesi ya kistaarabu na inayoeleweka.

Kwa Mtazamo wangu naona kuwa kuna matatizo makubwa katika Kitengo cha Mwasiliano Ofisi ya Rais.Ama kwa makusudi wanamfanya Mh.Rais Mpuuzi ama watu hawa hawajui vizuri kazi zao.Haiingii akilini kusikia kuwa Januari Makamba ndio yupo kwenye list ya Waandaaji Hotuba za Rais,sina uhakika kama kijana huyu alimaliza shule yake,kwa sabau alikwenda State House kwenye Intern tu,na sio kama ndio ilikuwa ajira.Kuna Magwiji wa uandishi wa Hotuba kama Balozi Daraja,Balozi Sanga,Balozi Sefue,Balozi Chokala na hata Chabaka Kilumanga,kwa nini watu hawa na wengine ambao hatujawataja wasijenge Timu imara ya kunoa Hotuba za Mkuu wa Nchi?.

Huyu Salva alikwishaambiwa matatizo ya Hapo Ikulu,nae aliingia kwa kuibadilisha sura ya Kitengo cha mawasiliano kwa kuwapangua akina Dada waliojazana hapo,lakini leo nae anaonekana kama mwanasiasa zaidi,hakuna lolote linaloendelea hapo,hali imekuwa mbaya kuliko kipindi cha Balozi Kalaghe.Waungwana.....Imefika kipindi cha kuwahoji hawa watendaji.Tanzania ni yetu sote,Aibu inayozungumzwa inatugusa sote...Inatia aibu kuona kwamba jina Tanzania linadidimia kwa sababu ya Uongozi Dhaifu...Mnaokutana na hawa wahusika fikisheni messages zetu,tusichoke kuwaamsha hawa Watendaji!!!
 
1.
Aliwahi kuwa permanent Rep of Tanzania to the UN - New York in the 1980s nadhani

2.
3.
Nilimaanisha US sio UN.


Mkapa, alikuwa mkurugenzi wa Daily news/Uhuru na Mzalendo, akawa Mwandishi wa rais, akawa balozi Nigeria, Canada, DC, Waziri Habari, Waziri Nje, Waziri Elimu Ya Juu, rais,

Hajawahi kuwa balozi wetu UN, Case closed!
 
Mwawado, ukiniuliza mimi nitakuambia Januari hatakiwi kuwa mwandishi wa hotuba za Rais; anatakiwa kuwa mshauri wake katika mambo ya kimataifa au maeneo ya Afrika. Mtu wa hotuba siyo lazima awe mwandishi wa habari lakini lazima awe mtu anayeweza kuzungumza na kuandika vizuri kwa kiingereza au kwa Kiswahili. Ni lazima awe mtu mwenye kipaji cha kushawishi na kucheza na maneno.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…