Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

aisee kazi kweli inamaana kama asingewekewa viini vya kansa angeishi milele?je alikuwa ana mkataba na mungu

Umejiuliza ukaishia njiani, sikulaumu nu ugonjwa unaowasumbua wengi hou.......
Ungeendelea kujiuliza na JK je angeishi milele kuusubiri uraisi! ungepata jibu la nilichokuwa nakisema.......
Uchovu wa kufikiri ni janga la kitaifa kwani hata JK analo tatizo hili la kwako.
 
  • Thanks
Reactions: UTC
@Pasco +FP hivi kinachowasukuma kumshabikia EL ni hiyo hali yake ya 'usafi' au kuna behind the curtain? Ila hata Hilter kuna waliomhusudu lakini binafsi hata washuke malaika kumpigia kampeni hatapata kura yangu..
 
Siku nikisoma kuhusu mitandao ya kuleta maendeleo nchini na si ya kuingizana madarakani nitafurahi sana! Huwa najiuliza, 'hivi haiwezekani watu kugombea uongozi kila mmoja kwa nguvu na hoja zake mwenyewe bila ya kutumia mitandao?'. Hili suala la mitandao litatufanya hata siku moja tusiweze kupata viongozi wazuri/wenye uwezo wa kuongoza.
 
Lowasa ni MMASAI bwana, nasema yeye ni Mmasai. Wanawake wa Kimasai wana tabia kama ya wale wa Kitutsi ya kurudi kutafuta mimba nyumbani halafu huyo Ndosi anaambiwa mimba ni yake! Juzi nilimwona akitajwa kwa cheo kizito tu cha Kimasai.
Ana Umasai gani EL Lowassa ni Olmekiii sio Mmasai hata kidogo... Kuhusu uLaigwanani ni tamaa za wazee wetu wa kimila walimpa sababu ya njaa zao si unajua zile sherehe za MWEZI wa 12 Monduli zinavyokuwa! Ndo hapa waliuza utu wetu, Mila na desturi zetu ikiwa walimkabizi njipinjipi Batilda Buriani wakati wa kampeni 2010 ilhali ni mwanamke watashindwa kumuuizia Lowassa uLaigwanani? Ndo maana siku zote tunasema EL ni Laigwanani wa Waarusha sio Wamasai na Kama ni Wamasai sio KINA Mollel Bali Laizer..... Ngoja jiwe lifukiwe rika zikibadilika vijana wengine wataingia rika ya wazee na ndo hapo hata chungu itapasuliwa na itawahaunt wote waliovunja Mila
 
hapo nakubaliana na wewe mkuu

Lowasa ni mchapa kazi,tena hana mda wa kusubiri kukumbushwa,yeye na Magufuri hawa jamaa bwana wanafaa

watu wanamwogopa magufuri kwa kuwa yeye hakwepeshi,hapohapo anakupa kitu,lakini ndio watu wanao faa kuiongoza nchi hii

kwa upande wangu nikiwa hai nitapiga kura kama tu
1 Lowasa akiteuliwa ama
2. Magufuri akiteuliwa

waliobaki ni wale wale tu ilimradi naye aongoze.sitapiga kura


Kwa hiyo na wewe ndiyo walewale wa kwamba;

  • kiongozi mwenye uwezo lazima awe au atoke CCM
  • CCM ndiyo chama pekee chanye maslahi kwa watanzania
  • CCM ndiyo chama pekee kitakachowakomboa Watanzania kulika kwenye lindi la umaskini
  • CCM ndiyo chama pekee kinachomjali mtanzania
  • CCM pekee ndiyo kinachojua kuwa ni nini tunataka Watanzania
  • CCM pekee ndiyo wana haki ya kutawala nchi hii
Inaelekea kweli wewe propaganda zimekuingia sawasawa. Ila kitu unachosahau hata walioko upinzani ni watanzania kama walioko CCM
!!!
 
nyie watu wawili nyie sijui vipi? yaani na uelewa wenu wote huo mmetekwa na lowassa?? ...anayway nyie endeleeni lakini nawambia huyu hashiki urais wa nchi hii.....hili nawambia kabisa...we psco nani alikwambia lowasa ni chaguo la Mungu? Mungu yupi wewe unayemzungumzia....hivi lowasa ana tofauti gani na hili juha muliloinstall hapo magogoni?

narudia tena lowasa hatakuwa rais wa nchi hii subirini kwani june mbali?? nyie endeleeni kukunjua viti mlale huko Elairline siku ikifika mtashindwa hata kwenda kutoa heshima za mwisho...

...mbona Pasco kafumba kidogo sana, tumuelewe na tumuunge mkono hata mtaani kwa kuwa mioyo yetu inajua nini inatafuta.
 
this is a knowledge to be read by conscious youth to know rotten is the administration! NAOMBA HIZO 'parties' zinzofuata zije faster is tupate kitu kamili taimely
 
Dah! Muda wote huu nilikuwa natafakari kuhusu msimamo huu wa mkuu PASCO. Kumbe anampigia chapuo EL ili CCM wafanye makosa ya kumsimamisha iwe rahisi kupigwa kikumbo na mgombea wa opposition na ndipo ukombozi kamili utakapopatikana! Thank you Pasco. Kama ni hivyo, kweli EL anafaa.

Pasco anaweza kuwa na matakwa hayo lakini akae akijua kuwa hiyo nayo ni risk. Tangu lini mgombea wa CCM akashindwa uchaguzi wa urais.

CCM wana machineries zote za kuweza kumfanya mgombea wao kuwa rais hata kama ni mchafu kama choo cha shimo. Na ikitokea Lowasa amepitishwa, with the money he has and the connections tunaweza kujikuta tumeingia mkenge wa kutisha!!
 
Nashukuru kwa ushauri nasaha,mwisho wa siku tukubali kutokubaliana ili tusonge mbele japo ni muhimu pia kuamini tunavyoviona kuliko kuona vile tu tunavyoviamini


Nimekuelewa kwenye red vizuri sana ungeishia hapo ningejua kweli mdau uliteleza,lakini ulipozidisha manjonjo kwenda kwenye Blue ukawa umetia sukari na chumvi pamoja basi du chakula kizima hakina maana tena basi kama ni mlo hauliki tena.

Ndio maana nikwambia bado unasafari sana ndefu,kwa kuwa wewe unaamini katika kuona,kumbe hauko katika list ya magreat thinker kwa kuwa wewe bado ni tomaso,mpaka ushike ndio uamini watu wa aina yako tunawaita MATERIAL PEOPLE.Wanaamini katika vitu kuliko imani ya usahihi wa mambo,kitu ambacho binadamu yoyote yule tunaemwita FISADI hapa Tanzania ni lazima awe na aina ya roho ambayo imesimama kwenye Material base na kamwe hawana spirtual guide kuamua na kutenda mambo.

Ingekuwa zama za Yesu wewe ni Tomaso,lakini zama zako wewe kwa sasa uko kwenye rank ya aiba ya mafisadi ambao wanaamni katika kukusanya vinavyoonekana ili kupata utukufu,kumbe utukufu utafutwa kwa imani ya nafsi,kuwa nafsi yako ikiwa na furaha moyoni pasipo makovu ya chuki, visasi, hila,giriba, uzandiki, wivu, vijicho, uongo, unafiki, ulafi, ulevi kupindukia,ushirikina, ufisadi na mengineyo mengi basi mwisho wake ni kifo cha aibu.

Nyerere kaondoka dunianai akiwa spirtual well-off leo hii Watanzania tunamkumbuka,lakini waliokuwa mabingwa wa materila [kuona na kushika] kama wakina Mobutu,Ghadafi na Mubarak aliyehukumiwa kuonyongwa jana wote leo hii ndio uzao wa matokeo wapendao kuona materaial pasipo kuamini.

Kama nawe bado ni mfuasi wa kuona basi ukiona vyaelea jua vimeundwa.Je waundaji ni nani?Utajibu swali hilo kama unajua unafiti wapi katika aina hizi tatu za watu.
1: Wale ambao wanafanya mambo yatokee [Those who make Things Happen]
2: Wale wasiojua yaliyotekea [Those who Dont Know what Happen]
3: Wale wanaoshanga yale yaliyotokea [Those who wonder what happen]

Je wewe Mr Romantic uko wapi?
 
@Pasco +FP hivi kinachowasukuma kumshabikia EL ni hiyo hali yake ya 'usafi' au kuna behind the curtain? Ila hata Hilter kuna waliomhusudu lakini binafsi hata washuke malaika kumpigia kampeni hatapata kura yangu..
mkuu heshima yako,
pasco amepanda EL airline imfikishe NEC na sio magogoni, akishaona EL kafika NEC atahamia ndege nyingine itakayomfikisha magogoni. hata mimi nimeamua kupanda hiyo ndege kwa mda,
 
...............huyu bwana is ASKING NOT WHAT HE CAN DO FOR HIS COUNTRY, BUT WHAT HIS COUNTRY CAN DO FOR HIM!!!

That is Edward Lowasa's story.

........................



sasa nakubali haya maneno ya sliding roof
 
nyie watu wawili nyie sijui vipi? yaani na uelewa wenu wote huo mmetekwa na lowassa?? ...anayway nyie endeleeni lakini nawambia huyu hashiki urais wa nchi hii.....hili nawambia kabisa...we psco nani alikwambia lowasa ni chaguo la Mungu? Mungu yupi wewe unayemzungumzia....hivi lowasa ana tofauti gani na hili juha muliloinstall hapo magogoni?

narudia tena lowasa hatakuwa rais wa nchi hii subirini kwani june mbali?? nyie endeleeni kukunjua viti mlale huko Elairline siku ikifika mtashindwa hata kwenda kutoa heshima za mwisho...
Mkuu Edson, nabii hatambuliki nyumbani!. Hata Yesu Mnazareti aliyezaliwa Mfalme wa Wayahudi, ni Maayahudi hao hao waliomsulubisha!. Ila pia kwa kuteswa kwake, sisi tuliponywa!

Lowassa ni nabii aliyekataliwa nyumbani. Hili ni " lile jiwe walilolikataa waashi, litafanywa kuwa jiwe kuu la pembeni"!.
 
There are currently... users browsing this thread. (... members and ... guests)...,
mtoahabari...,.


Mkuu mtoa habari, puuzia ule ushauri, endelea kumwaga nondo watu tufaidike!
 
There are currently... users browsing this thread. (... members and ... guests)...,
mtoahabari...,.


Mkuu mtoa habari, puuzia ule ushauri, endelea kumwaga nondo watu tufaidike!

nimemuuliza swali kuhusu Dr.Slaa kwenye huo mtandao naona jamaa kawa kimya, ndo mtu pekee hadi sasa ambaye imani yangu imebaki kidogo kwake.
 
nimemuuliza swali kuhusu Dr.Slaa kwenye huo mtandao naona jamaa kawa kimya, ndo mtu pekee hadi sasa ambaye imani yangu imebaki kidogo kwake.

usiaminishwe kila kitu mkuu,changanya na za kwako..DR Slaa ni jembe usisubili kuaminishwa na mtu.
 
wewe itabidi nikutafutie mda tuonane nikifika huko..sitakualika pale club itabidi tuonanie eneo jingine....halafu ile tabia yako ya kualikwa mahali halafu unajilipia gharama ilumuudhi yule jamaa sana siku ile pale kanda ya kati...ulimuona alivyoshangaa...

uliweza kujilipia bill japo ulialikwa lakini leo ile dhamira huna tena unanunulika kirahisi sana....hivi umetwa na nini? huyu ENL amekuahidi ee!!
Edson, asante kwa nia ya kunitafuta, wanajf huwa tunakutania hapa ukumbini na kama kuna issue nyeti tunaonana kwenye pm, hivyi ukifika wala usijisumbue.

Utetezi wangu kwa Lowassa ni uzalendo tuu kwa nchi yangu wala sio njaa au pesa. Ningeamua kusaka pesa, ningewatumikia wenye pesa za kutakata tena sio hizi za madafu!. Mimi ni masikini jeuri kama "kozi mwana mandanda, kulala njaa kupenda".
 
Back
Top Bottom