Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

Kikwete, huu mtandao ni hatari! Be careful, otherwise waweza kuwa historia (Part 1)

Mkuu Ogah, wengi mpaka sasa wameshindwa kunielewa. Tofauti na wengi mimi si mnafiki na sifichi chuki niliyo nayo dhidi ya CCM kwa sababu kama nilivyowahi kusema hapo nyuma naamini adui mkubwa wa taifa letu ni CCM kwa kuwalea na kuwakumbatia mafisadi na wezi wanaoifilisi nchi. Nakataa kata kata kuwa ndani hili genge la mafisadi na wezi yupo au anaweza akatokea kiongozi mwenye dhamira ya kweli ya kuikomboa Tanzania huku hadi leo hii, saa hii, dakika hii bado kajaa humo anashirikiana na kula nao, je anafanya nini humo chumbani ? Kama hadi sasa hana ujasiri wa kuachana nao, hana ujasiri wa kukaa mbali nao na hana ujasiri wa kusema hapana, imetosha, huo ujasiri wa kupambana nao ataupata wapi ? Huyo hatufai !

Mkuu Mkandara naona na yeye humo kwenye kundi la ambao hawanielewi ama hawataki kunielewa kwa sababu sijui Chadema inaingiaje katika hoja yake. Mimi si mwana Chadema na kusema kweli hata hao viongozi wa Chadema nawafahamu tu mtandaoni kulingana na ninayoyasoma kuhusu harakati zao za kisiasa lakini niko pamoja nao kama lengo ni kuwaondoa hawa manyang'au madarakani. Historia mpaka sasa imetufundisha sote jambo moja nalo ni kuwa chama cha siasa kikishachafuka na kuwa kimbilio la wahalifu, kitatumia tu uovu kama silaha yao kuu ya kung'ang'ania kubaki madarakani. Hivyo ndivyo serikali zote za kifashisti zinavyozaliwa, zinavyokomaa na zinavyoendeshwa zikiwaonea, kuwagandamiza na ikibidi kuwaua wananchi wake.

Ni kweli kama wanavyodai wengi, yeyote yule CCM ikimsimamisha kugombea hata akiwa chizi wa kutupwa anaweza kuibuka kidedea iwe kimizengwe au kibabe, hilo halina ubishi kwani tumeshuhudia si mara moja hii ikitokea. Lakini kwa Lowassa mambo ni tofauti kidogo na nitaeleza hili kwa kuuliza swali moja kuu, je ni watu wa aina gani hao ambao hawako tayari hata kulisikia hilo jina likitajwa na je, ikatokea hivyo, watafanya nini ? Je wachangiaji kama wewe Ogah au hata Mkandara wenye msimamo wa kutotaka kusikia hata uvumi tu wa hilo, mko tayari kufanya nini kama, God Forbid, hilo jina hilo litapendekezwa ? Kulingana na michango yenu ninayoyaona humu ndani mnaamini kwamba Raisi atakuwa Lowassa na mambo yataendelea kama kawaida.

Sisi wengine on the other hand tumeenda hatua moja mbele kwa kuitambua the weakest link kwenye hiki kitendawili nacho ni aina ya watu ambao hata leo hii hawapati usingizi jina la Lowassa linapoibuka na ndio hawa tunataka ujumbe uwafikie. Bahati nzuri ni kwamba wapenzi wakubwa wa Lowassa wako ndani ya CCM na maadui wakubwa wa Lowassa nao wako ndani ya CCM na hao wote kwa pamoja bahati ilioje kuwa kiongozi wao mkuu ni Kikwete. Hapo ndipo anapoingia mtu kama Mag3, anajua pande zote zinavyofuatilia mjadala na cheche za moto zinavyoanza kuruka ruka, lahaula, anamwaga petroli ! Jamani, adui mkubwa wa CCM ni CCM na kwa wale wenye wasi wasi naomba niwatoe hofu, turufu ya mabadiliko ni Lowassa !
Mkuu utanisamehe sikupata nafasi ya kukujibu hoja yako...

Mkuu sii swala la kutokukufahamu wewe bali nataka wewe ufikirie nje ya box...Na nilichosema hapo nyuma ni kwamba sisi WATU, Wadanganyika wapiga kura ukiweza kutushawishi kwamba Lowassa ndiye the answer kwa matatizo yetu baso tutachukua maamuzi hayo hadi ktk sanduku la kura. Hivyo kama leo mtaendelea kusema Lowassa is the answer basi ndiye atakuwa hadi kaburini maana tuna asili ya kuamini mizimu na ukitupa dawa ya chaguo la Mungu kiimani basi umetumaliza kabisaaa hata kama ulikuwa unafanya utani.

Kwa hiyo unachosema wewe unatazama udhaifu ndani ya CCM na ili wagombane, basi na achaguliwe Lowassa!.. Lakini umesahau moja tu ya kwamba siku hizi ndani ya CCM hakuna msafi tena na hakuna mtu anayependwa na wengi kama Lowassa isipokuwa kundi dogo sana na wale waliomkataa shetani, hawana tena nguvu wala mamlaka. Kinachotokea leo ndani ya CCM ni Mafia gang tu yaani control ya territory zao - wizara za Uwekezaji. Na Lowassa seems to be fair to all parties zinazoshiriki ktk UTAJIRISHO..wanajua vizuri kwamba ndani ya Lowassa kila mmoja waoa atakula lakini kwa kupimiwa sio Buffet!..

Ni sera ya Lowassa aliyetaka kujenga Mabillionea 100 kufikira mwaka 2010, yeye aliamini kabisa kwamba akiweza jenga mabillionea 100 ndipo tutaweza wekeza wenyewe ktk viwanda na uzalishaji lakini hao mabillionea 100 watatokana na wizi wa fedha za misaada Worldbank na za umma. Na kila kiongozi alijipanga nyuma yake mawaziri wote wa kwanza kila mmoja alijua anashika wapi na ataaachia wapi. Ni Lowassa aliyetuuza kwa mzee wa Loliondo nambie nani hakwenda huko wala kuamini kikombe cha babu?.. Ni wewe na mimi tu ambao tulifikiria inge back fire lakini badala yake akapata umaarufu zaidi hadi serikali nzima ikashjiriki kikamilifu ktk kamba za Lowassa..

Huyu jama hatari kweli kweli mkuu wangu anajua sana jinsi ya kuteka akili za watu utadhani anatumia uchawi (nasikia huenda Nigeria) lakini sii wa kumsabikia hata kidogo.. Ndicho nachosisitiza miye kwani Wadanganyika wataamini hivyo na tayari sasa hivi kisha yakutanisha makundi yote pamoja chini yake..waliobakia ni wachache sana na tatizo lake na JK ni kwamba JK haamini kama Lowassa atakubalika kinyume cha hapo JK na Lowassa hawana ugonvi..Na nimewasema Chadema kutokana na uvumi naoupata mjini kwamba nao wanamshabikia Lowassa kwa mfikra hizo hizo.. Haya ni makosa makubwa sana kum underestimate EL maana ni hatari kuliko wanavyofikiria..

Wee nambie mbali na kundi dogo la watu wanaotegemea JK atawachagua wao kusimama 2015, huyo Lowassa ana maadui gani zaidi ndani ya CCM ya leo? Nijuavyo mimi karibu wajumbe wote wa NEC wanamshabikia yeye!. Na kama chaguo lao ni yeye, fahamu pia RA yupo nyuma yake.. Hapa tunatakiwa kupiga vita bila kuwapa pumzi hata kidogo yasije tokea yale ya JK na sifa za chaguo la Mungu tukidhani kwamba makundi yao ingekuwa rahisi kwa CCM kusambaratika - Haikuwa!
 
Sidhani kama CDM wamekosa kazi hadi waanze kutafuta mtu wa kumnadi huku tayari wagombea wanafahamika. CCM kushinda wanapigana vikumbo kuhusu Urais ni kukosa uwajibikaji kwa wananchi.

we unabisha kitu ambacho kiko wazi,hudhani but ndio hali halisi,unataka kujifanya hujui kwamba wafuasi wa chadema nao wanacheza ngoma ya kumsaka mgombea urais wa tz kwa tikiti ya ccm?hujaona kuna mchangiaji mmoja mashuhuri humu ametengeneza mpaka bango linalosomeka mwishoni mwa kila ujumbe anaochangia humu "EDWARD NGOYAI LOWASSA FOR....."Tafuta huyo mtu utampata humu na ni CHADEMA damu,huo ni mfano hai lakini wapo wengine wa aina hiyo humu,fuatilia utaelewa nasema nini..
 
Mr President,

Ningekuwa na muda ningekueleza mengi sana. Muda wangu ni kidogo sana ndiyo maana nashindwa hata kupost mambo mengi kuhusu taifa hili hapa JF. Ninatuma post hii si kwa lengo la kukutisha. Lengo ni kukukumbusha uwe makini ili usijefanya uamuzi wa hovyo na kuliingiza taifa katika machafuko na kuharibu timetable za watanzania. Machafuko ndiyo tunayoyakwepa lakini si wewe (I have to tell you the truth because you are not my breadwinner at all).

Mtandao

Ninachozungumzia hapa ni kundi kubwa na hatari linaloaminika kuongozwa na Edward, Rostam, Othman, Apson, Karume na Shein na Mkapa. Ninakufahamu vizuri sana na ungekuwa uwezo wako, hawa wote ungeweza kufanya uwezalo ili kumweka madarakani mtu unayemtaka kwa maana ya Asha au Nahodha. Huu ni mtandao unaofanya kazi kwa umakini wa hali ya juu sana. Ukitaka kuamini, jiulize swali la kipuuzi sana kuwa kwanini kila plans unazofanya (zisizo na faida) kwa kundi hili zote zimefail?

1. Shein ni nani?

Nataka nikukumbushe ''issue'' ya Omar Juma. Huyu alikuwa threat kubwa kwa kundi lenu kwa ajili ya 2005. Mtandao wake ukibebwa na Mkapa ulikuwa ni hatari sana. The only way ilikuwa ni ''kumwondoa'' na hilo liliwezekana. Siku nikiwa na muda nitaeleza mchezo wote ulivyofanyika. Wakati jina limeletwa tukiwa hotel moja maarufu hapa Dar, nakumbuka hukuweza kumfahamu Shein wala kulitamka jina lake vizuri. Ulikosea mara tatu kulitamka. Tukacheka wote. Hatimaye Shein akawa makamu wa rais.

Baada ya wenzako kukuweka madarakani (mgombea ndani ya CCM), kosa ambalo Shein hataweza kukusamehe katika maisha yake (Mimi sio Mungu, kwani anaweza kukusamehe vilevile) ni pale ulipo-attempt kumfanya Zakhia kuwa makamu wa rais. Asingekuwa Edward, Rostam, Mkapa na Karume, leo hii Shein angekuwa mwenyekiti wa TPDC au TANAPA!. Kitendo cha Shein kuletwa na kundi hili, kutetewa na kundi hili achilia mbali kushawishiwa na kundi hili agombee urais wa Zanzibar ili kummaliza nguvu Nahodha chaguo lako kinamfanya awe mtiifu kwao kuliko hata kwa Mwanamwema!. Unafahamu vizuri Shein alivyoshinda urais Zanzibar, rafiki zako walikuchezea akili wakikuambia kuwa wamemleta Shein ili kupunguza kura za Bilal na ulipomkubali Shein wao wakaenda kumpigia Bilal kampeni wakijua kazi ya kumweka Shein imekamilika. Baada ya hapo uliendelea kumng'ang'ania Zakhia kuwa makamu. Mkapa akishirikiana na Rostam (ambaye alikuwa akim-install Bilal kuwa makamu huku yeye akiwa South Africa kuangalia World Cup) walimweka Bilal hapo alipo.

Shein hakushinda uchaguzi Zanzibar. Kilichofanyika ni Mkapa, Rostam, Karume kumhonga pesa za kutosha sana Maalim kupitia kwa kijana wao hatari sana Jussa (kumbuka huyu aliletwa na Rosatm ili umteue awe mbunge). Today, umeshindwa kumweka mtu wako Zanzibar na makamu wa rais Muungano. Walichoweza kufanikisha ni kuiteka Zanzibar yote (Bilal na Shein). Nakukumbusha ya kwamba, ili uwe mgombea kupitia CCM, unahitaji Zanzibar na 'Lake Zone'. Kule 'Lake Zone' wamekushinda. Hilo unalifahamu vizuri. Hii ndiyo maana Wanzanzibar wamekutesa sana ndani ya CC iliyopita. Ili kukuonyesha kwamba hufai, Shein kampa udaktari wa heshima ''Baba yake'' mdogo Karume. Ninafahamu jinsi unavyojikosha kwa Anne kwa kumpa nishani ili kusiwe na vote of no confidence mwakani hasa kwa sakata la Richmond na Twiga. Napenda kumhakikishia Anne ya kwamba that's a strategy anayoitumia Mugabe ya kuwamaliza watu. JK ameiiga huko. Naomba Anne uwe makini sana. Waweza kufa kwa ''presha'' usipoangalia.

2. Karume ni nani?

Huyu alipigiwa kampeni kubwa sana na Edward na Rostam mwaka 2000 licha ya CCM Zanzibar kumkata jina lake. Kwa hili Karume hawezi kuwasahau hawa jamaa mpaka anakufa. Karume alikupinga Butiama. Yeye, Edward na Rostam wakaenda ku-design ''mwafaka'' wao wanaoujua ambao leo hii unafanya kazi Zanzibar. Nataka nikukumbushe mara ya pili kuwa Jussa aliletwa kwako na Rostam ili umpe ubunge. Think twice! Karume ndiye rais aliyeleta maendeleo makubwa Zanzibar. Shein will do more than what Karume did. Usishangae ukisikia Karume kuwa makamu wa Lowassa 2015!. Karume ana msimamo. Hayumbi na bahati mbaya sana hakuogopi.


NITAENDELA SIKU NYINGINE WAPENDWA WANA JF
Riwaya zile zile za alinacha...miaka nenda miaka rudi kila mtu anakuja na tamthilia yake ya kufikirika. Hakika wabonge kwa ngano wapo mbele kwani kila mmoja ni mjuvi wa kila fani..km unabisha hudhuria mechi yeyote ya kimataifa uwanja wa taifa ili uone kila shabiki jukwaaani anashindana na mwenzie kuhusu mchezaji yupi afanye nini! Na bado tutasikia mengi kabla ya 2015 lakini lililowazi EL hawezi kuwa our next presidaa!!
 
Riwaya zile zile za alinacha...miaka nenda miaka rudi kila mtu anakuja na tamthilia yake ya kufikirika. Hakika wabonge kwa ngano wapo mbele kwani kila mmoja ni mjuvi wa kila fani..km unabisha hudhuria mechi yeyote ya kimataifa uwanja wa taifa ili uone kila shabiki jukwaaani anashindana na mwenzie kuhusu mchezaji yupi afanye nini! Na bado tutasikia mengi kabla ya 2015 lakini lililowazi EL hawezi kuwa our next presidaa!!
Naona K una hasira na HH kwa kuchelewa kwake vuta subira mambo mazuri hayataki haraka vinginevyo kuna kila dalili kuwa upande wa pili wanataka kujua nini kinachojili.Wenye akili zao walioyaona haya ya bwana HH wakayafanyia kazi na hatua wakachukua na vipengere vikarekebishwa wasiojua wanatahamaki wakiuliza wanaambiwa mbona basi lilishapita ikizu lianelekea msoma mjini zamani hivyo.Uzuri uko upande ule ule wa wanawachezesha wenzao filamu ndio inaendelea tunasubilia part two ya safari kutoka musoma mjini kwenda suguti.
 
Duh! Mkubwa nakuwa kama nafunguka macho hivi, hebu endelea kutujuza maana mambo ya Jussa sio kidogo, huwa anatoa miropoko ambayo mtu wa kawaida hawezi kuifunguka! Tafadhari endele akutujuza
 
End will justfy the meaning..., My God may you grant me more days of living....
 
Lowasa ataliingiza taifa kwenye mzigo mkubwa wa madeni

Katika hili napingana nawe mkuu,
Huyu EL hawezi kukopa hovyo, yeye anatafuta kupitia uchumi wa ndani na kuiimarisha shilingi. Tazama jinsi alivyofanya hatua za kilimo cha mvua za kutengeneza na umwagiliaji alipokwenda Thailand ili ahamishie ujuzi huo uje hapa Tanzania. Si mtalii au muombaji au muhudhuriaji wa makongamano kama tuambiavyo sasa 'mikutano isiyoisha anayohudhuria mkulu ughaibuni'
 
Katika hili napingana nawe mkuu,
Huyu EL hawezi kukopa hovyo, yeye anatafuta kupitia uchumi wa ndani na kuiimarisha shilingi. Tazama jinsi alivyofanya hatua za kilimo cha mvua za kutengeneza na umwagiliaji alipokwenda Thailand ili ahamishie ujuzi huo uje hapa Tanzania. Si mtalii au muombaji au muhudhuriaji wa makongamano kama tuambiavyo sasa 'mikutano isiyoisha anayohudhuria mkulu ughaibuni'
kila shabiki wa Lowassa na kikwete ni muhalifu maana anashabikia waliopoteza maisha ya nyerere! ni upunguani kuamini hawa wauaji watafufua uchumi. kama watapata madaraka kwa sumu watatumia sumu hiyohiyo ya bone marrows kuyalinda. haya mashabiki wote jiandaeni kuuliwa mkikengeuka!
 
Huyo rais wenu mtarajiwa (el) siku hizi amekooondaa, ana matatizo gani au anaumwa nini, uso umemkongoroka! hatuwezi weka picha yake kwenye ofisi zetu

Wafuasi wa el naomba mnijuze baba yenu anagonjeka nini
 
Nchi hii watu wana nyeti kwelikweli, nadhani jamaa kaanika vitu vya maana, lakini yote na yote heri haizidi kudra
 
Katika hili napingana nawe mkuu,
Huyu EL hawezi kukopa hovyo, yeye anatafuta kupitia uchumi wa ndani na kuiimarisha shilingi. Tazama jinsi alivyofanya hatua za kilimo cha mvua za kutengeneza na umwagiliaji alipokwenda Thailand ili ahamishie ujuzi huo uje hapa Tanzania. Si mtalii au muombaji au muhudhuriaji wa makongamano kama tuambiavyo sasa 'mikutano isiyoisha anayohudhuria mkulu ughaibuni'
Mvua ya Thailand ulikuwa utapeli mwingine. Tanzania ilishapoteza zaidi ya dola millioni kumi katika kile walichokiita utafiti wa mvua hiyo. Na tushukuru kama yule waziri mkuu wa Thailand asingepinduliwa leo ingekuwa imekula kwetu tena na fisadi Lowassa akijiongezea pesa nyingine mfukoni.
 
Hivi tapeli kaishia wapi,tulitaka aje aelezee kilichotokea kwenye kikao cha NEC dodoma hivi karibuni ambako jk anaonekana kukidhibiti chama kwa kuwaondoa wazee wote kwenye vikao vya maamuzi na kuwaundia chombo chao kwa ajili ya ushauri tu..na pia hakuna mbunge kugomea ujumbe wa nec tena,hapa huyu atatuletea tetesi gani tena...
 
Huyo rais wenu mtarajiwa (el) siku hizi amekooondaa, ana matatizo gani au anaumwa nini, uso umemkongoroka! hatuwezi weka picha yake kwenye ofisi zetu

Wafuasi wa el naomba mnijuze baba yenu anagonjeka nini

Umeona eh, jana nimemuliza jamaa mmoja aliye karibu na familia hiyo akaniambia anadalili za stroke upande mmoja ingawa haijadhibitishwa kama ni kweli au la.
 
Watanzania,

Hivi kweli mnapenda story za udaku namna hii?.

Kila siku huwa nasema na kusisitiza anzeni kufikiri kwa kutumia ubongo wenu acheni magazeti na mitandao kuwafikiria.

Ndio maana mnalialia kila kukicha maisha magumu, hayawezi kuwa raisi kama mnaamini story ya kutunga kama hiyo hapo juu.
Hatupendi udaku, kwa nini wewe usimpinge kwa hoja kwamba anachosema kiko vipi? Ye kampa JK ushauri, na kwa manufaa yake na Taifa, nina uhakika atauzingatia. Mtoa maada anaonekana sio mtu wa kada ya chini, anaufahamu vizuri huu mtandao. Na huwa anahudhuria vikao vyao! Siwezi kumbishia bila sababu, part two itatupa mwanga zaidi. Unashindwa kuelewa, hii ni sehemu ndogo tu ya kilichotolewa. Subiri amalizie kisha ndo tuanze kumwaga maoni yetu. Be patient, its just a trailer, there is so much here. Hold and wait!!!
 
Nanukuu gazeti la mwanahalisi toleo na 276 la jumatano tar.11-7 2012 lilikuwa na habari maalim seif alishinda fuatilia kipengele kisemacho kama maalim alimsamehe salimin,pia alimsamehe karume akatangazwa mshindi ihali hata wewe jusa unajua seif alishinda urais zanzibar..................kwa mantiki hiyo basi hapa jf sio kila kitu cha kubeza hapa mtu anatoa dukuduku lake lililopo moyoni asikilizwe .
 
Back
Top Bottom