Kikwete kavunja katiba??

wambeke

JF-Expert Member
Joined
Aug 30, 2013
Posts
2,655
Reaction score
2,650
WanaJf Salaam??
naomba kujua maana mie sio mtaalamu wa katiba.
Leo rais wa Jamhuri katangaza uteuzi wa mkuu mpya wa Jeshi la Police pamoja na naibu wake.

swali langu ametumia katiba gani kutangaza hicho cheo kipya cha naibu IGP? au atapelekwa Zanzibar? maana kwene rasimu ya pili ya katiba nimeona spika akitoka bara naibu wake zanzibar je na kwene majeshi nako ni hivyo?
kwa hiyo tutegemee naibu mkuu w majeshi tena au>?
 
Kwa mujibu wa Katiba ya JMT Rais ana mamlaka ya kuanzisha au kufuta ofisi yoyote katika Serikali. Hivyo hajavunja Katiba.

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Swala la uteuzi wa mkuu wa jeshi la polisi halizungumziwi kwenye katiba ya sasa. Uteuzi wa
naibu IGP ni swala la kubadilisha tu mfumo wa kiutendaji ndani ya polisi (police force organization structure)
 
Kwa mujibu wa Katiba ya JMT Rais ana mamlaka ya kuanzisha au kufuta ofisi yoyote katika Serikali. Hivyo hajavunja Katiba.

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums


Kweli katiba yetu kiboko, itakuwa ya aina yake dunia. Kama ni hivyo na mshauri rais afute ofisi inayoitwa ikulu. Arudi zake msoga kijijini kwao akaongozee serikali kwa kuanzisha ofisi ya msoga.
 
John brenahan is right.
Na hicho kinachotufanya kupambana usiku na mchana kubadili hali hii ya kuwa imperial president kwamba anaweza kuongeza ukubwa na matumizi ya serikali bila wanachi wala wawakilishi wetu yaani wabunge kuwa na mchango wowote wakati sisi walipa kodi ndiyo tumalipia gharama zote yaani rais ana create expense and stick us with the bill
 
Alikuwa ana balance dini wakamshitua ikabidi amkimbize mwingine Zanzibar. Labda pengine amekubaliana na katiba ya zenj kuwa ni nchi inapaswa kuwa na IGP wake lkn akazuga kwa kumwita naibu IGP. Lisu alisema Zenj ina jeshi lake JKU na sasa wana IGP wao.
 
Kweli katiba yetu kiboko, itakuwa ya aina yake dunia. Kama ni hivyo na mshauri rais afute ofisi inayoitwa ikulu. Arudi zake msoga kijijini kwao akaongozee serikali kwa kuanzisha ofisi ya msoga.

Wewe ni mburura wa karne ya ishirini na moja. Nashindwa kujua kundi gani la kukuweka na laiti ungekuwa enzi zile za Mussa basi wewe ni mfuasi mtiifu wa Firauni.
 
Rais hajavunja Katiba.
Umeleta swali kwa kukiri kuwa wewe sio mtaalamu wa katiba.
Pokea maoni na majibu na utapata cha kujifunza.
ukiwa na majibu yako mwaka utaumaliza vibaya.
 
Hapana hajavunja katiba kwa mfumo huu wa katiba rais ana madaraka makubwa sana ya kufanya mabadiriko anayoyataka.Ndiyo maana tume ya Warioba imeliona hilo na kupendekeza kupunguza madaraka ya rais.Big up sana judge Warioba.
 
Rais kavunja katiba msimtetee vyeo vyote vina muundo wake ndio maana mpaka leo Mrema anadai mafao ya naibu waziri mkuu anashindwa kupata kwani kimuundo cheo hicho hakikuwepo ndio maana katiba mpya inatakiwa kumuondolea kinga rais
 
Kuna vyeo vya kikatiba na visivyo vya kikatibam vyeo vya Kikatiba kwa mujibu wa Katiba ya JMT ya 1977 ni kama Urais wa JMT, Makamu wa Rais, PM, Mawaziri, AG, DAG,DPP, CAG, Makamishna wa Tume ya Haki za Binadamu etc. Vyeo visivyo vya kikatiba mojawapo ni kama uIGP, uCDF etc. Vyeo hivi visivyo vya Kikatiba msingi wake hutokana na sheria inayounda vyombo husika ambayo hutamka aina ya vyeo katika chombo husika. Aidha, vyeo visivyo vya kikatiba mara nyingine msingi wake huwa muundo wa vyombo husika ambao huandaliwa kwa kushirikisha chombo husika na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Kwa mantiki hiyo basi cheo cha Naibu IGP hakipo katika Katiba lakini kimo katika Muundo mpya wa Utumishi wa Jeshi la Polisi. Hivyo, hakuna uvunjaji wowote wa Katiba uliofanyika.

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Hakuvunja katiba ila mapungufu ya katiba ndio inampa fursa kufanya hayo anayoyafanya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…