Kikwete siyo safi! - yes I said it!


Juxtapose with

"Man is conceived in sin and born in corruption and he passeth from the stink of the didie to the stench of the shroud. -- Willie Stark in All the King's Men"
 
Kama hatutawatoa CCM madalakani au kupata upinzani wa nguvu au kuwawajibisha mafisadi Tanzania tusitegemee kwenda popote zaidi ya stories za kujifurahusha hapa JF. Natabiri 2010 hali itakuwa mbaya TZ karibu na ile ya 1980s lakini JK atapata 70 % ya kura na CCM watapata 80 % za wabunge!!!!
 

I am afraid neither kuwatoa CCM madarakani, kupata upinzani wa nguvu wala kuwawajibisha mafisadi tu pia hakutasaidia kumaliza matatizo kwa uhakika.

Tunaweza kuwatoa CCM Madarakani, tukapata upinzani wa nguvu kama alivyokuwa Chiluba Zanzibar na kuwapiga risasi mafisadi wote tunaowajua sasa hivi.

Only to descend further into the depth of the squalor of corruption under wapinzani.

Tunachotakiwa ni kuhakikisha siyo tu tunafanya hayo uliyoyataja, bali tunajenga system itakayokuwa incorrigibly for justice, accountability and rule of law na kuwa na population yenye elimu na muamko wa siasa.

Tusipoweka misingi hii huku juu juu tutakuwa tunacheza tu.
 
Hapa kweli iko ISHU NZITO. Hawa wanangata na kupuliza sidhani kama wana tofauti wakoloni. Mkoloni alijulikana rasmi kuwa ni mnyonyaji, mkoloni wa leo anajiita ndugu, anafanana na sisi, tukilia njaa analia na sisi angali yeye ndio chanzo.
Mmechuma lakini hatutawaacha mle kwa amani. Mafisadi wote watabeba hii nembo 'fisadi' mbale na nyuma yao hadi watakaporudisha walichomnyanganya mwananchi mnyonge. Watoto wao wote watarithi hiin nembo na laana.
 
 

Labda mimi sijakuelewa swali lako vizuri, kama ulikuwepo BCS mimi nilikuwa mtetezi mkubwa wa Mkapa,

Hapa umechanganya mengi mkuu kati ya dataz na ukweli, the dataz ni kwamba baada ya kutoka uwaziri hela za mjukuu wake mwenye umri wa miaka minne, karibu Billion 4 zimezuiliwa na serikali kwa siri,

Ukweli ni kwamba under Mramba, wafanyakazi wa serikali hatukukosa mshahara hata mwezi mmoja kama sasa,

Ukweli zaidi sasa hivi Mramba, ni fisadi kama Mtikila, kipi usiochoelewa hapa nikueleweshe mkuu?
 
Zero kasema mwaka 2010 JK 70% na ccm 80% ubunge, Mimi nasema inawezekana sana kuwa na matokeo mengine. Nadhani wengine wanaogopa maana hili wingu laonekana kuwa zito sana, tukikaza buti, tukawa na malengo na tukafanya kazi kwa haraka inayotakiwa tutafika. Wanaharakati walioko Tanzania kwa sasa wameshaleta presha ya kuwafanya walioko madarakani wapate matumbo ya kuhara wanaposikia issue zao zinatajwa, usiwaone wanapita njiani na magari sasa hivi, asilimia 90% ya mafisadi wanaharisha kwa woga kila siku. Ukitaka kujua ni waoga, wanyang'anye magari sasa hivi uone kama watatoka ndani...? wengine hata kuendesha wenyewe hawawezi ni vile tu wanaendeshwa. Tuombe Mungu washindwe kwa Amani maana wako radhi kufanya lolote kwa sasa, tuliyoyaona bungeni na kwingineko ni juhudi za kujikomboa hizo.
 

sasa nimekuelewa kwamba mramba naye ni FISADI,ulinichanganya uliposema ni mmoja kati ya viongozi wetu walio safi.
mapambano yaendelee mkuu,ushindi wala hauko mbali
 
Kikwete hawezi kuwa safi kama alizaliwa kwenye familia chafu, kwa ujumla kama angekuwa safi angeshafukuzwa kwenye familia yao siku nyingi zilizopita. Yaani ccm ni uchafu mtupu, tusitegemee aliyezaliwa na kukuzwa na ccm awe msafi. Lingine ni kwamba tusijidanganye kwamba eti Kikwete ni mgeni wa mambo yaliyoko katika nchi hii, naomba tukumbuke kwamba JK hadi afike hapo alipo amepitia idara zote na wizara zote nyeti kwa nyakati tofauti. Tusidanganyike anapounda tume kujidai kuchunguza maasi ya baba zake, ni danganya toto isiyo na mwisho kwa upande wake. Tuambiane ukweli labda kama mimi nimepitwa na wakati, ni ripoti gani kikwete aliyoifanyia kazi hadi sasa katika ripoti zote alizopewa na tume alizozituma kufanyia kazi zozote...? Ni juzi tu hapa tumekumbwa na balaa la mwanamasumbwi pekee aliyekuwa anaenda olimpiki kukutwa na madawa ya kulevya. Cha ajabu aliyehusika ni jamaa ambaye alitakiwa kuwa mfungwa kwa wakati huu, JK anasema anapambana na madawa ya kulevya...? Kwahiyo wana-JF mtaniambia JK hamjuia huyu jamaa? sasa hadi inafikia kuwatumia wanamichezo ambao hata kujitayarisha kwao na kuondoka kwao kwenda olimpiki ilikuwa bahati nasibu? kama sio dharau ya pekee ni nini maana ya haya yote? KIKWETE NI MCHAFU, NA HUU NI UCHAWI ALIORITHI KWA BABA ZAKE (CCM). Akiwa msafi na awakatae baba zake.
 
CCM inapokuwa chafu, basi wananchi wote tunaowapigia kura for the last 45 years tunakuwa wachafu kuliko CCM wenyewe, au?

CCM in baadhi ya viongozi wachafu sio siri, hata upinzani pia kuna baadhi ya viongozi wachaceh wachafu kama Mtikila,

Kikwete ana mapungufu mengi ya uongozi, lakini wizi huwa sio one of them, maaana angeiba nyingi sana toka alipoanzaia nishati, Fedha na nje,

Mnyonge Mnyongeni, lakini kama kawaida ya JF huwa tunatoa haki, alizaliwa na baba kiongozi alyekuwa mjumbe wa NEC, baadaye akalelewa na kusomeshwa na Mwalimu, sidhani kuwa mikono ya Mwalimu ilikuwa michafu!
 
Asante Mkuu, nakuunga mkono kwamba wanaona sawa kuchuma na kula lakini tuendako tukijaaliwa kuwa salama tutaona matokeo. Hizi laana za watanzania hazitawaacha watoto wao wakue hivihivi, sitasema lolote kuhusu hili lakini Mola atujalie uzima tuone matokeo. Waswahili walisema dua la kuku halimfikii mwewe na mafisadi watajitia moyo kwa hili, mimi nina hakika hili litafika. Kwa akili yangu mtindi, nina ushahidi mkubwa kisaikolojia kuhusu hili.
 
Mkulu FM ES nakubali kwamba JK anaweza kuwa sio mwizi maana angeiba siku nyingi, lakini anapoona wenzake wanaiba akanyamaza tumweleweje? Baba zake namaanisha ccm maana ndio familia yenyewe, kama anawajua wanaoiba na kunyang'anya mali za watu, hatutaki na wakati mwingine (protocol) sio lazima awataje, ila ni kwanini awang'ang'anie hadi madhara yatokee wazi tukayajua? naamini angekuwa mwelewa angezima hizi issue kimya kimya na sisi wadanganyika tukaendelea kuamini ccm ni safi. Kama hadi uingereza waseme Chenge ni mwizi, unataka kuniambia JK hakujua mkuu ama uingereza wanatusingizia? Kama JK alijua kwanini hakumtafutia post nyingine akatulia ili sisi tuendelee kuamini kwamba wao ni safi?
 


Mkuu nimekusikia, tatizo maneno yako ya juu hayafanani na ya chini, tizama mwenyewe! Kwa sababu in one quote Kikwete ni mchafu na hafai, ya pili ni kwa nini anawaone haya wezi, hivi Mwalimu alikuwa mwizi? Under utawala wake ni viongozi wangapi walifikishwa kwenye mikono ya sheria? Je hakukuwa na viongozi wezi under his rule?

Mapungufu ya uongozi kwa Rais, hayahusiani ni tabia ya wizi ya viongozi wachache walioko ndani ya CCM, that is my point!
 

...and a very good one.

Let's stretch it a little further, if you will.

Mtu "msafi," kiongozi, ama Nyerere, ama Kikwete, ama mja wa mtaani, anaeashudia jambazi linavunja benki kuu, au linaficha hela chimbo, na hapigi kelele "mwizi mwizi..." ana integrity?
 
Kuhani... we can even go a little bit further...

Inakuwaje mtu ambaye siyo tu anashuhudia uvunjaji bali anafungua mlango, ili wasivunje..?
 
Mkulu FM ES, mwisho wa majibu yangu yote ni kama kuhani alivyokuuliza. Ukimwona mwivi anavunja benki usiseme lolote tukuite wewe msafi? Hapana...wewe ni mchafu. Sasa hapa JK ni mchafu kwasababu hafanyi lolote kuhusu wachafu anaowajua. Kingine ni kwamba mimi sisemei viongozi kuwa ndio wazazi wa JK, mimi nasema ccm ndio imemkuza JK. Na ccm ni familia ambayo inaimarisha umoja wake ikijua kabisa sisi ni wezi lakini ni marufuku kijana yeyote wa nyumba kusema sisi ni wezi, kwahiyo familia inakubaliana ikiwemo hao unaosema wewe kwamba ni wasafi. Kwa msingi huo, hatuwezi kumchagua aliyejichanganya huko sisi tukamtoa kwa nguvu na kusema huyu ni msafi, Hapana Mkulu. Kama alikubaliana na uchafu wa familia, na akakubali kuuficha, naye ni mchafu.
 
Labda we can go futher.......zaidi.... na sisi wananchi tunaoendelea kuwachagua hawa viongozi wezi na wavunja majumba na sisi ni wezi pia, au?

Maana tunawaona majabzi wanavunja kwa maneno yenu, lakini bado tunawachagua hii inatuweka wapi sisi wananchi on this logic of yours?
 

CCM ni chama cha siasa, sio kitengo cha Police katika jamii yetu ya Tanzania, nia na madhumuni yao kama chama cha siasa ni kushinda uchaguzi na kutawala, sasa kama wemeweza kufanikiwa hilo kwa miaka 45 mfululizo,

tena wakiwa wachafu unasema wa kulaumiwa na Rais wa sasa? Aliyechaguliwa only miaka miwili tu iliyopita? au?

Hatukatai kuwa serikali yetu ya sasa ina matatizo tena mengi sana, lakini tuyaelekeze yanapotakiwa sio kila mahali, na pia tuwe specific!
 
Mkulu FM ES watu ni hawakujua kwamba JK ni mchafu, walidhani labda angekuwa mteule. Sitawalaumu sana hata maaskofu waliosema Mola ametuletea mkombozi ambaye ataigeuza hii nchi kuwa paradiso, wamevumilia sana na wameshaona matokeo maana miaka ya JK imekwenda haraka sana. Subira yavuta heri imeumiza matumbo na wengi sasa wanajuta chinichini, point ni kwamba JK sio msafi na wananchi wameshagundua Mkulu.
 
Mkulu ili mwili uende popote ni kichwa kwanza kinaweka utaratibu wa wapi pa kwenda na kwa wakati gani, sasa hapa wewe unatushauri tulipe tumbo kazi ya kufikiria mwili uende wapi. Kimsingi tumbo litatuelekeza jikoni Mkulu, kama hakuna chakula tumbo litashauri mwili usiende popote hadi chakula kiletwe ama kipikwe. Mwili ukishakula tumbo litashauri mwili upumzike hapo hapo jikoni ili chakula kingine kikiletwa mwili uwahi kupata share yake. Hata kama ana washauri na mengineyo mengi Mkulu, mhusika ni yeye na sisi hatuwajui wengine, unataka kuniambia washauri wa Prezidaa wakimwambia avae pensi na kandambili kwenye hotuba ya sherehe za muungano atavaa...? Hapana... kwanini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…