Kila kitu kinachotokea ni uhalisia uliochelewa "Delayed reality"

Kila kitu kinachotokea ni uhalisia uliochelewa "Delayed reality"

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,151
Reaction score
4,277
KILA KITU KINACHOTOKEA NI UHALISIA ULIOCHELEWA "DELAYED REALITY"
Tumekuwa tukihamasishwa mara kadhaa kutokuwa watu wa kuongozwa na matukio( matokeo) na badala yake tumeshauriwa sana kuwa watu wanaoona tukio katika uumbikaji wake kabla halijatokea kwa sababu likishatokea tu linakuwa "uhalisia iliochelewa".

Wapo wanaoshauri juu ya kuwa watu wa kuona zaidi ya kuona kwa kutumia macho.Tunalazimika kuona kwa kutumia akili kabla ya kutumia macho "proactive" kwa sababu kuona kwa kutumia macho ni kuchelewa kuona "reactive" na hapo ndipo linapokuja suala la kuchelewa kuona "delayed reality".

Uhalisia uliochelewa huthibitika kwa wengi na kujenga uhalali mkubwa kuliko uhalisia katika uumbikaji wake. Kuchelewa kuona ni pumbazo na liwazo kwa akili za wengi. Hali hii husabanisha pia madhara makubwa kwa wengi.

Hakuna kitu kinachotokea katika ulimwengu wa vitu kwa kuwahi. Yatokeayo yote ni mambo yaliyochelewa kwa sababu ni mambo yaliyotokea tayari katika mawanda ya uumbaji. Siyo ajabu mtu kuota ndoto na ikatokea kutoka maisha yake kama alivyoiota au kwa ufanano mkubwa kutokana na ukweli kuwa mambo mengi hufanyika kikamilifu kabla hatujayaona katika ulimwengu wa vitu.

Kutokana na uhalisia kuchelewa katika ulimwengu wa vitu wapo wanaofanikiwa kuona mapema   lakini changamoto wanayoipata ni kukiwasilisha kwa ambao hawajaona. Eneo hili la uhalisia uliochelewa limesababisha kuibuka kwa watu wengi chini ya mwamvuli wa unabii.
 
KILA KITU KINACHOTOKEA NI UHALISIA ULIOCHELEWA "DELAYED REALITY"
Tumekuwa tukihamasishwa mara kadhaa kutokuwa watu wa kuongozwa na matukio( matokeo) na badala yake tumeshauriwa sana kuwa watu wanaoona tukio katika uumbikaji wake kabla halijatokea kwa sababu likishatokea tu linakuwa "uhalisia iliochelewa".

Wapo wanaoshauri juu ya kuwa watu wa kuona zaidi ya kuona kwa kutumia macho.Tunalazimika kuona kwa kutumia akili kabla ya kutumia macho "proactive " kwa sababu kuona kwa kutumia macho ni kuchelewa kuona "reactive" na hapo ndipo linapokuja suala la kuchelewa kuona "delayed reality".

Uhalisia uliochelewa huthibitika kwa wengi na kujenga uhalali mkubwa kuliko uhalisia katika uumbikaji wake. Kuchelewa kuona ni pumbazo na liwazo kwa akili za wengi. Hali hii husabanisha pia madhara makubwa kwa wengi.

Hakuna kitu kinachotokea katika ulimwengu wa vitu kwa kuwahi. Yatokeayo yote ni mambo yaliyochelewa kwa sababu ni mambo yaliyotokea tayari katika mawanda ya uumbaji. Siyo ajabu mtu kuota ndoto na ikatokea kutoka maisha yake kama alivyoiota au kwa ufanano mkubwa kutokana na ukweli kuwa mambo mengi hufanyika kikamilifu kabla hatujayaona katika ulimwengu wa vitu.
.........................
"matukio( matokeo)" haya ni mambo mawili tofauti.
 
Hebu dadavua kidogo tupate kuelewa.
Kwa tafsiri rahisi kabisa ishara hutangulia tukio, mathalani ktika jamii upo usemi dalili ya mvua ni mawingu. Mvua hapo ni "delayed reality"na mawingu ni "warning mechanisms"...
........................................................
 
Hata kifo kinaweza kuwa uhalisia uliochelewa kwa mtu kwa sababu katika ulimwengu wa uumbaji wa matukio na vitu, mambo hufanyika mapema sana kabla hayajatokea katika ulimwengu wa vitu. Tunaosubiri kuona Kwa macho huwa tunachelewa sana na ni rahisi sana kuongozwa na matukio.

Siyo jambo la ajabu mtu kufa leo ila akawa alishakufa miaka kadhaa iliyopita katika ulimwengu wa uumbaji kutokana na ukweli kuwa kinachotokea katika ulimwengu wa vitu ni uhalisia uliochelewa "delayed reality". Ulimwengu wa vitu unaweza kuwa na watu wengi wanaotembea ingawa walishakufa.
 
Hata kifo kinaweza kuwa uhalisia uliochelewa kwa mtu kwa sababu katika ulimwengu wa uumbaji wa matukio na vitu, mambo hufanyika mapema sana kabla hayajatokea katika ulimwengu wa vitu. Tunaosubiri kuona Kwa macho huwa tunachelewa sana na ni rahisi sana kuongozwa na matukio.

Siyo jambo la ajabu mtu kufa leo ila akawa alishakufa miaka kadhaa iliyopita katika ulimwengu wa uumbaji kutokana na ukweli kuwa kinachotokea katika ulimwengu wa vitu ni uhalisia uliochelewa "delayed reality". Ulimwengu wa vitu unaweza kuwa na watu wengi wanaotembea ingawa walishakufa.
We call it dead walking alive. Yani ulishakufa lakini bado unaonekana hai kimwili but roho ilishapepea miaka
 
We call it dead walking alive. Yani ulishakufa lakini bado unaonekana hai kimwili but roho ilishapepea miaka
Haswaa....!
Kuna wakati unaweza kusikia watu wakisema jamaa anatembea ila watu walishamaliza yao sisi tunaosubiria kuona katika ulimwengu wa vitu ndiyo wahanga wa delayed reality.

Leo katika baadhi ya imani kuna watu wameweza kuyatawala mawanda haya ya uhalisia uliochelewa na hakika wanawapata wengi kama wafuasi wao ila inawezekana kabisa kila mmoja kutokuwa muhanga wa uhalisia uliochelewa.
 
Back
Top Bottom