Kila nikichemsha njegere haziivi

Kila nikichemsha njegere haziivi

zipo njegere zisizoive na hizi mara nyingi sana zinalengwa kupikwa zikiwa kavu kama maharage na sio mbichi. siri moja ukitaka kujua njegere zinazoiva angalia punje zake, punje kubwa na zenye rangi ya kijani ilioiva sana, na ambazo ukizimenya hukuti zina wadudu wale funza wanaokula njegere ujue basi hizi haziivi. ukizitafuna mbichi utaona hazina sukari mdomoni so kama zimemenywa toka sokoni jaribu kuuma moja ama kuangalia aina ya punje.

kwa ambazo zinaiva hizi zina punje ndogo na zimepauka fulan hivi pia kama zina maganda utakuta nyingi zimeliwa na funza kwani zinanoga sukari, njegere hizi unapopika usifunike wala kupika na maji mengi sana zitamenyeka.

unapotaka kupika hizo zinazoiva kwa kutolainika basi zichemshe kwa maji kidogo, bila chumvi, yakikaukia ongeza maji tena, pia zifunike ziive kwa mvuke na usichemshe kwa moto mkali sana zitababuka badala ya kuiva.
Asanteje jamani yaani nashukuru sana
 
Mkuu niliugua ugonjwa wa ndui ilibaki kidogo nipoteze maisha,ndiyo maana yamebaki madoa madoa usoni!Huu ugonwa uliua watu wengi sasa hapa kwetu Tanzania.

teh teh teh pole sana
 
Njegere hazichemshwi kama makande jamani!!!
 
Njia ya haraka ya kupika njegere,ukishaziosha ziweke kwenye sufuria unayokaanga washa moto vile vimaji vya kuoshea vikikauka weka mafuta kiasi na chumvi anza kuzikaanga kama DKK 5 weka kitunguu endelea kukaanga mpaka kiive,weka karoti endelea kukaanga weka nyanya zako sasa na spice nyingine upendazo funikia nyanya I've nyanya ikisharojoka weka tui LA Nazi LA pili funika punguza moto vichemke taratibu ukipenda weka na Viaz kidogo lile tui likishakauka weka tui la kwanza korogo vizuri likiiva epua hapo njegere zako zinakuwa tayari kuliwa na ubwabwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom