Kila nikiifikiria hii kodi nashindwa kuwaelewa TRA, naona kama naibiwa

Mimi nimeanza biashara mwezi wa 4 mwaka huu,
1. Nilitakiwa nilipe na kodi ya quarter ya kwanza kama mleta mada anavyolalamika.
2. Tax officer kanikadiria kodi ila bosi wake kasema hii haimtoshi muongezee. Nikalalamika akasema utake utalipa usitake utalipa.
Chakushangazaa yule alienihoji kujusu hako kabiashara kangu kapya kanielewa ila yule bosi wake kagoma kunielewa.
3. Nikalipa instalmnt 1 kisha nikaandika barua kuomba nifanyiwe assesment upya kutokana na hali ya biashara kuwa ngumu. Meneja akagoma akasema lipia installment zilizobaki kisha ndio tunaweza kukubadilishia.
4. Nimeamua wiki hii napeleka barua ya kusitisha TIN yangu kuwa nafunga biashara. Tuone hata kile kidogo ambacho nilikua na uwezo nacho wa kulipia hawatakipata.

Nadhani watu wa TRA na serikali wanapita humu wataona malalamiko yetu.
Kama jiwe ndii kawalazikisha wafanye kazi kwa staili hii basi analazimisha watu wote tukalime na tuachane na biashara na kujiajiri.
 

Hiyo ndio njia sahihi (ya kuwaambia unafunga). Na yaliyokukuta ndio yanayowakuta walipa kodi karibia wote na ni kwa sababu moja tu: watu wanaamini kuwa ni jukumu la TRA kukadiria watu kodi wakati sheria inakutaka WEWE mlipakodi ndio ujikadirie (ila TRA wafuatlie kujiridhisha kuwa makadirio yako yalikuwa ni sahihi). Kila mlipa kodi angekuwa anajua hili na kulisimamia kubambikia kodi watu kungeisha.
 
Wazungu walisemaga mazingira ya kodi Tanzania yanafanya uwekezaji kuwa mgumu
Itakuwa na wao ndio wanafanyiwa hivyo hivyo wanaanza uwekezaji mwezi wa 8 wanadaiwa kodi kuanzia January wakati hiyo January hata mitambo yao ilikuwa haijafika

Mambo mengi ya nchi hi yapo katika maajabu ya dunia kama tusingekuwa na bandari tungekuwa masikini sana vichwa vyetu vimelala sana
 
!
!
Ndio Ukome. Kuchukua Kadi Ya Sisiemu Pamoja Na Kitambulisho Cha Mjasiliamali Ulishindwa Nini? Ni 20000 Tu
 
Kwani ile sheria waliyosema wanaipitisha mfanyabiashara anaeanza biashara halipi kodi mpaka afikishe miezi sita tangu aanze biashara haifanyi kazi bado au zilikuwa porojo tu?
Hilo ni deni tayari linasoma katika tin namba yangu na natakiwa nililipe kabla ya tarehe 31 December
Nisipo lipa ikifika 2020 nitapigwa penati kwa kweli najuta kwa nini nilienda TRA
 
Je utaratibu huu unaleta mantiki? Ndicho anacholalamikia mleta mada. Au ni lazima kila biashara ianze shughuli zake mwanzo wa mwaka?
hilo ndio swali la maana hapana huu utaratibu sio kabisa hata kabla hatujafika hapo utaratibu wa kukata kodi kwenye mauzo na sio faida ni unyanganyi kwa mfanyabiashara..., makadirio yote ni mauzo na sio faida..,
 
Hii ni kwa mujibu wa sheria iliyopitishwa na Bunge kuwa kwa biashara mpya mtafanya makisio kama kawaida ila utapewa muda wa miezi sita kuanza kulipa hiyo kodi; kipengele kingine ambacho ndicho kinachokuumiza ni kuwa kodi yote inatakiwa kulipwa mwisho wa mwaka wako wa fedha yaani 31/12

Endapo ungekuwa umesajili biashara yako January, ungeanza kulipa hayo makisio July ila yote yawe yamelipwa ifikapo 31 December

www.vabusiness.co.tz
 
Vp akianza January?

Tatizo Kesha kadiriwa tayari,TIN yake tayari inasoma hayo makadirio,sasa hata akianza january, Deni litasoma, cha Muhimu aende akaonane na meneja, Mara nyingi mameneja huwa waelewa
 
Right. Lakini pia kodi nyingi sio user friendly kabisa. Kama uko kwenye biashara nadhani unanielewa
Nimegundua kwa nini watanzania wengi hawalipi kodi tatizo ni maofisa wa TRA eidha wana mapungufu kutokana na tatizo la elimu yetu tunayoipata darasani au wanafanya kusudi ili kutengeneza mazingira ya rushuwa
 
huu upuuzi mwenyewe nilijuta sana...Siji kurudia kufuatilia leseni ya kuanzisha biashara ikishapita January, nitakimbizana nao tu hadi mwaka ujao...Halafu walivyo wa ajabu wanakuambia System ndivyo ilivyo-setiwa utadhani hiyo system haiwezi kufanyiwa maintainance ikarekebishwa kuondoa wizi huu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…