Kila nikijaribu kumsamehe/kuwasamehe nashindwa

Kila nikijaribu kumsamehe/kuwasamehe nashindwa

Asante sana, sijawai kujua mimi ni mwandishi mzuri ingawa wakati nikiwa form four zile essay za English sijawai Pata below 18/20. Kuna essay moja niliandikaga Mwalimu akaichukua akaenda kuichapisha Kwenye gazeti. Ila mimi kama mimi sipendi kuandika
Good for you
 
Daaaah wanawa
Msamehe tu uwe huru moyoni mwako hata hivo s ushaamua kuendelea na maisha yako sasa kinachoufanya ushindwe kuwasamehe ni nn??

Acha dunia iwafunze barabara ww lea wanao tu wakikua watamtafta mama yao wakipenda lakini wasamehe
Wanawake wengne hawana akili daaah pole sana mkuu story yako inasisimua nataman ata ingeendelea
 
Kwani wewe uliyepata upendo wa baba Na mama, baba yako akuwa Na mchepuko, mamayako alikukosesha upendo kisa michepuko ya Mzee wako, ? Kwani ujasoma kuwa mwanamke alikuwa kachoka kiuchumi Na jamaa akupenda watoto wake wakae uswahilini,
Unless hujaelewa alichokiandika! Mwanamke akiwa mjamzito alileta manzi kwake akapiga wiki nzima na manzi akataka kukatalia gheto. Utawazaje kutembea na mwanamke mkeo mjamzito? Pili unajua effect inayofata? Mama yake atakapo ondoka duniani atawachukua watoto akakae nao je watakua chini ya mama gani?
 
Asante Mkuu, Mkuu nilifanya kila linalowezekana kumrudisha huyo mwanamke akakataa , nikamwambia mpaka aende alikouza vitu akawaambie ameuza kwa makosa nimtumie hela awarudishie arudishe vitu nyumbani na yeye arudi nyumbani akakataa. Kwa hyo Mkuu ulitaka niwaache Watoto wage kwa utapiamlo, maana hali ya watoto ilikuwa inakaribia na watoto wenye utapiamlo kwa muda mchache ambao huyo mwanamke alikaa nao.?
Kaka nielewe sipingi wewe kuwachukua watoto, ila kutoka moyoni naona mbele kuna drama inakuja na itahusu watoto. Tazama kwa makini maisha baada ya mama yako kuondoka duniani kisha tazama nawe uondoke ghafla! Nini kinafata? Kwakua unawapenda watoto basi vaa uhusika wao kisha chukulia mama yako angekosa hivyo nini kingefanyika.
 
Nimeisoma yote inasikitisha mnoo,punde tu ulipoona tabia ya dada ake hukupaswa kumuona iyo roho anayo peke ake kumbuka ni damu moja hukujihadhari mapema,pili uyo mwanamke anaroho flani ambayo inakisasi kikali ndani yake hawa ata akikusamehe basi atatuñza kisasi ndani yake huwa wanasamehe kwa ulimi,ajabu hukumkuta bikra sasa iweje awake kuona sms kwenye simu yako,

tukiachana na mengine nawe ulikua unamakosa kwanini uchepuke alafu ujisahau,ukiwa mchepukaji kuwa makini simu yako ni yako ya mwenzako ni yake full pasworrd,wewe ulitoboa mtumbwi alafu kuogelea hukujiandaa

cha msingi na ili uwe mshindi katika hili ni kusamehe( kwakua keshazaa nje si lazima mrudiane),msamehe wasamehe na ndugu zake,msapoti,msaidie pale unapoweza,wasiliana nae ukiwa na nafasi,onana nae mara moja moja ukiwa na watoto(mara moja kwa kipindi)

utakuwa huru samehe na kusahau,kikubwa maisha lazima yaendelee,ila ulikutana na mwanamke mwenye roho ya kisasi
 
Unless hujaelewa alichokiandika! Mwanamke akiwa mjamzito alileta manzi kwake akapiga wiki nzima na manzi akataka kukatalia gheto. Utawazaje kutembea na mwanamke mkeo mjamzito? Pili unajua effect inayofata? Mama yake atakapo ondoka duniani atawachukua watoto akakae nao je watakua chini ya mama gani?


Hapana Mkuu...huyo manzi sikumleta wakati huyo mwanamke akiwa mjamzito. Kama umesoma vzuri nilianza kuishi na huyo mwanamke Mara tu baada ya kupata ujauzito
 
Mkuu mm nikiwa kama mwanakamati mwandamizi Wa roho mbaya nakushauri kabisa usimsamehe mwanamke huyo..
Ulishaachana na pepo usilikaribishe tena litakupoteza mazima... Kila la kheri kaka
 
Stori imejaa kujisifu na uzandiki.
1. Mwanzoni, Ulijivunia vitu badala ya UTU (upendo wa dhati). Ukaibuka na Mtoto wa mjini na genge lake
2. Mchumba/mke uliunganishiwa na ndugu (japo wa mbali) hukumchagua,
3. Mahusiano yako yamejaa washauri kibao (sister, jamaa wa kazini, mamaz, majirani) miluzi mingi humpoteza mbwa.
4. Mpaka mwanamke anakukimbia (na uwezo ulionao) ujue una tatizo.
**Ku-balance story ilipaswa tumsikie mwanamke nae maana wewe unajifagilia mwanzo -mwisho eg. Nilikuwa na kila kitu (nyumba ya kupanga?), Mark II, nilinunua bati 20,nikanunua shamba 1m
Sasa mkuu kama mtu alikua navyo hivyo vitu kwanini asiseme? Hatujasikia kuhusu mwanamke si ajabu ukute huyo mwanamke hajui hata kama kuna JF, pengine ana simu ya tochi, na ulishaambiwa kuna kondakta ameshazaa nae kwaio hapo kuna kua na familia mbili tofauti
 
Kaka nielewe sipingi wewe kuwachukua watoto, ila kutoka moyoni naona mbele kuna drama inakuja na itahusu watoto. Tazama kwa makini maisha baada ya mama yako kuondoka duniani kisha tazama nawe uondoke ghafla! Nini kinafata? Kwakua unawapenda watoto basi vaa uhusika wao kisha chukulia mama yako angekosa hivyo nini kingefanyika.


Mkuu nakuapia nikiamua kurudiana na huyu mwanamke sitamaliza mwaka nitazikwa. Mkuu kuna mambo mengi sana sana sijaongea Kuhusu huyu mwanamke baada ya mimi kumchukua watoto. Mpaka kuanza kuniomba msamaha kuna mambo mengi mno alishafanya au kuongea na kujiapiza Kuhusu mimi.

Nikueleze tu kisa kimoja, kuna wakati nilipata ajili nikaumia sana mgongo, nililalal ndani kama miezi sita hivi. Yule mwanamke aliniandikia sms akaniambia 'Na bado nitaendelea kulia na Mungu na yatakukuta zaidi ya hilo'. Mtu kama huyu nirudiane naye Mkuu, hapana aisee

Najua mama yangu anaweza ondoka muda wowote hata na mimi naweza ondoka muda wowote, uhai wa mtu uko mikononi mwa Mungu, ila hapana boss, Mungu atawalinda wanangu ikitokea mimi na mama yangu tukaondoka wote.

Sorry boss ila hapana.
 
Mkuu nakuapia nikiamua kurudiana na huyu mwanamke sitamaliza mwaka nitazikwa. Mkuu kuna mambo mengi sana sana sijaongea Kuhusu huyu mwanamke baada ya mimi kumchukua watoto. Mpaka kuanza kuniomba msamaha kuna mambo mengi mno alishafanya au kuongea na kujiapiza Kuhusu mimi.

Nikueleze tu kisa kimoja, kuna wakati nilipata ajili nikaumia sana mgongo, nililalal ndani kama miezi sita hivi. Yule mwanamke aliniandikia sms akaniambia 'Na bado nitaendelea kulia na Mungu na yatakukuta zaidi ya hilo'. Mtu kama huyu nirudiane naye Mkuu, hapana aisee

Najua mama yangu anaweza ondoka muda wowote hata na mimi naweza ondoka muda wowote, uhai wa mtu uko mikononi mwa Mungu, ila hapana boss, Mungu atawalinda wanangu ikitokea mimi na mama yangu tukaondoka wote.

Sorry boss ila hapana.
Pole ndugu. Huyu mwanamke ulimchukulia wapi? Amelelewa katika mazingira gani? Kabila Gan? Dini? Funguka tuponye vijana wanaopenda kuoa bila kuchunguza tupone
 
Sijawahi kusom la waraka mrefu kama huu huku jamii, ila pole sana na upo so touch. Pole sana
 
Stori imejaa kujisifu na uzandiki.
1. Mwanzoni, Ulijivunia vitu badala ya UTU (upendo wa dhati). Ukaibuka na Mtoto wa mjini na genge lake
2. Mchumba/mke uliunganishiwa na ndugu (japo wa mbali) hukumchagua,
3. Mahusiano yako yamejaa washauri kibao (sister, jamaa wa kazini, mamaz, majirani) miluzi mingi humpoteza mbwa.
4. Mpaka mwanamke anakukimbia (na uwezo ulionao) ujue una tatizo.
**Ku-balance story ilipaswa tumsikie mwanamke nae maana wewe unajifagilia mwanzo -mwisho eg. Nilikuwa na kila kitu (nyumba ya kupanga?), Mark II, nilinunua bati 20,nikanunua shamba 1m
Wabongo bwana ila angeandika yeye ni maskini wa kutupwa ana godoro tu na ndoo moja ya maji ungeridhika?!
 
Kidogo nitakuwa tofauti na kila mtu humu.
Kwanza nianze kwa kukwambia pumbavu! Pumbavu sana! Pumbavu tena!
Ukitembea na mchepuko mkeo alikua kakukosea nini? Umefanya kazi ya kuweka akili kwenye Mali ukasahau watoto wanahitaji malezi ya baba na mama na si ya bibi. Nikweli mkeo alikosea kwa hatua alizochukua baada ya wewe kutenda kosa ila unajua mkeo ni zaidi ya wewe unavyomwona mkeo? Huyo binti unaejivunia mzuri anamwita mkeo mama! Nafikiri unajua maana ya neno mama. No matter what kwa wanao huyo ni mama yao, ukizingatia upendo wako kwa wanao utaanza na kulijua hilo utajua watoto wanahitaji uwepo wa mama kama wanavyohitaji uwepo wa baba pia. Nyote wawili hamjui watoto wanataka nini mnawaza Mali za dunia na starehe zenu, ndio maana yeye alikua bize na biashara kuliko watoto na wewe ulikua busy na kumvua chupi mchepuko pumbavu sana! Ndoa na iheshimiwe nakwambia hili kutoka moyoni pumbavu sana!
Kuna kitu kinaitwa malipizi ya dhambi hivyo ulikua kwenye malipizi ya dhambi na kadhalika mkeo nae kawa kwenye malipizi ya dhambi zake. Hakuna mtu mwenye haki kwenye hii dunia mrudushe mkeo kwako na chukua wanao mkae nao. Kubwa tu siku zote unapohama hama na mkeo shetani yuko mtaani anasaka wafwasi wake. Ndoa ni ndoa na ni above your emotions.
Samahani kama utahisi sielewi uliyopitia. Pumbavu sana.
Ww ndyo mpumbavu tena mpumbavu wa mwisho yani ukute SMS moja kwenye simu yangu ndyo urudi kwenu au uuze vitu alafu c kila aliyezaa anaweza kulea hakuna cha kumlaumu mwanaume apo ata kidogo ukijua nature ya wanaume wala huwezi kulaumu mwanamke ni mpumbavu ndyo maana akakimbia penzi lake na kuona mwanaume hana lolote
 
Kimsingi mzazi ni mzazi hata angekosea. Mtoto hawezi kumwona mzazi anateseka akavumilia. Lakini pia huwezi Pima amani watoto waliokuwa nayo enzi wazazi wako wote na amani walionayo sasa.
Hajatazama vizuri hiko siku bibi yao ataenda mbele ya haki itabidi awachukue watoto wataenda kuishi na nani kama si mama wa kambo? Na baada ya hapo drama ya pili itaanza
Kwani mama wa kambo ni sumu nani kakwambia mama wote wakambo ni wabaya mm sijalelewa na mama yangu lakin nimeishi vizuri tu acha imani za kijinga nani kakwambia nyoka anaweza kuwa samaki si kila uliyezaa naye anafaa kuolewa naye na si kila uliyemuoa mtafika tamati ya kufa na kuzikana kama hupati furaha moyoni na uliyenaye kwanini umuuwe dunia ikakulaumu c bora umuache kwa amani na mbigu itakusifu
 
Back
Top Bottom