Kila nkifanya ubunifu mshindani wangu anaiga ,wote tuko na aina moja ya biashara vinywaji na vyakula

Kila nkifanya ubunifu mshindani wangu anaiga ,wote tuko na aina moja ya biashara vinywaji na vyakula

Kwamba huo ubunifu is out of this world ? Kwamba haujawahi kufanyika popote au na wewe uliiga sehemu ? Kama ndivyo basi maybe you are in the wrong business anza biashara ya ubunifu na kuwauzia watu ideas...

Anyway issue sio ideas issue ni implementation...
 
Buni bidhaa yenye kuleta hasara halafu lete kwa idadi ambayo kwako iko ndani ya uhimilivu wa hasara halafu mshirikishe kwamba hiyo bidhaa ndiyo inayokupa faida kubwa kwa sasa halafu tuone ikikopi na kupesti.
 
Nimetengeneza bidhaa Bora kwanamna navojua kwenye kiwanda wamehangaika kwa miaka2 Hadi wakakipata kiwanda nao wakaenda omba special oder kama yangu
Kama hiyo bidhaa Ina ubora huo unaousema na mwenzio katoka oda kama hiyo sioni tatizo.
Kwanza hiyo inaonyesha bidhaa ni bora na inapendwa na Ina faida mpka wengine kuiga.... Faida ya mwenzio kuiga ni kwamba wateja wataongezeka kwani kwenda tu kutoa oda kama yako kiwandani kwanza kaipa promotion bidhaa husika na kaongeza wingi wa bidhaa na wateja.
Sasa wewe kwa upande wako hakikisha bidhaa yako inakua na ubora ule ule na weka misngi na msimamo wako katika kazi mwisho wa siku mtumiaji ndio muamuzi wa kuchagua kilicho bora kwa upande wake.
 
Kuna brother wangu mmoja mwaka 2014 alishusha chanja zima la sulphur ya kupulizia mikorosho kijiji cha mdimba Sudi baada ya siku 2 kuna mchaga nae akashusha nae chanja zima...brother alishusha bei akawa anauza bei ambayo hapati faida zaidi ya kurudisha tu hela yake yule mchaga alimfuata akawa anamwambia asifanye hivyo ila brother aligoma akadai yeye kwake anaona faida na isitoshe wale ni ndugu zake...baada ya wiki mchaga alihama na baada ya siku ya pili tangu mchaga ahame bei ikapandishwa.NB biashara ni mtaji
 
Kama hiyo bidhaa Ina ubora huo unaousema na mwenzio katoka oda kama hiyo sioni tatizo.
Kwanza hiyo inaonyesha bidhaa ni bora na inapendwa na Ina faida mpka wengine kuiga.... Faida ya mwenzio kuiga ni kwamba wateja wataongezeka kwani kwenda tu kutoa oda kama yako kiwandani kwanza kaipa promotion bidhaa husika na kaongeza wingi wa bidhaa na wateja.
Sasa wewe kwa upande wako hakikisha bidhaa yako inakua na ubora ule ule na weka misngi na msimamo wako katika kazi mwisho wa siku mtumiaji ndio muamuzi wa kuchagua kilicho bora kwa upande wake.
Shida hapo inakuja anaipunguza Bei hiyo bidhaa ili avute wateja nawateja nao wanahamia kwake kufuata Bei ndogo
 
Shida hapo inakuja anaipunguza Bei hiyo bidhaa ili avute wateja nawateja nao wanahamia kwake kufuata Bei ndogo
Kama anapunguza Bei Ina maana hiyo bidhaa kaipunguza bei na kiwandani kaipunguza ubora...
Wewe tulia uza bidhaa yako bila papara na uhakikishe ubora wa bidhaa yako uko pale pale!!!! Unaona energy ya Azam iko juu kwa bei na ubora kwa hapa Tanzania na hana mpinzani kwa soko la ndani japo mie sio mtaalamu lakini sababu kuu mojawapo itakua ni ubora!!!!
Hapo unateseka na ushindani na inaonekana wewe ni mtu yule unaumizwa kwenye harakati za ushindani,,, buni mbinu mbalimbali za kuuza hiyo bidhaa yako hakikisha sehemu uliyopo unafatilia harusi zote na misiba ukisikia harusi jiingize kwenye kamati ikifika muda wa vinywaji lazima utapata tenda,, siku hizi misiba iko tofauti watu wanalia na vinywaji na hela zao ukisikia vilio unasogea unasoma mazingira ukielewa beba vinywaji vyako,, viwanja vya mpira tafuta taarifa na habari kuhusu ligi kuanzia ligi kuu ,,ligi daraja la kwanza huko watu wanakula Bata na kina vibe wanajiachia mechi za basketball ball huko kote unaweza uza huku ukiendelea na biashara yako maana huko hayazidi masaa mawili...
Hakikisha upande wa masoko uwe na alternative Tena upande wa vinywaji hautesi unaweza kuuza hata kwenye mikutano ya hadhara....

Nikupe mfano wangu labda utakusaidia.
Nilianza kuuza solar ,tv , radio, sabufa pamoja na spare zake sokoni nilikutana na ushindani mkali wa bei, kujuana, kuchongeana tra, na uchawi juu yake. Tanzania hii nimeizinguka kidogo nikawaza uhitaji ni mkubwa vijijini na wanafika Bei kuliko mjini!!! Nilianza kupeleka bidhaa zangu maporini na vijijini huko nilisambaza mfulilizo miaka minne matokeo yake niliyopata mwaka wa sita ninavyoongea hapa huko maporini Nina jina na napokea oda inayokuja na hela cash ikifika msimu wa mauzo kwangu unakuta foleni kama ya bank wale washindani wananiita mtoto mchawi sana yule.... Na duka langu sasa hivi limekua la kuuza kwa oda zaidi yanii mwendo wa kutuma mizigo..
Kaa chini tafakari kama hiyo biashara unaipenda usiikatie tamaa Wala usimuwaze mpinzani wako!!! Tengeneza njia zako za kupata wateja na jipe muda utatoboa.
 
Tumi
Habar wakuu leteni uzoefu wenu,Niko katika biashara ya vinywaji na chakula kwamiaka Sasa ,mshidani wangu yuko mita50 tuko ofisi yangu, Sasa Kila nkifanya ubunifu wakibiashara basi ataiga,nkiigiza product mpya sokoni basi nae ataiga na ataipunguza Bei
Nini chakufanya biashara imekua pasua kichwa Kila ubunifu utakao uweka washindani wote wataiga
A akili ...hakuna watu wapumba kwenye biashara kama wauza vyakula... uchafu uchafu na kutokutumia akili
 
Back
Top Bottom