Kili Marathon kugawa barakoa kwenye Mbio zitakazofanyika mwaka huu

Kili Marathon kugawa barakoa kwenye Mbio zitakazofanyika mwaka huu

Kampuni ya Kilimanjaro Marathon inayoendesha Mbio maarufu za kila mwaka za “Kili Marathon” zinazofanyika Mkoani Kilimanjaro imetangaza kuwa kutakuwa na zoezi la ugawaji wa barakoa kabla na baada ya mbio kwa wakimbiaji wote wa mbio fupi na ndefu.

Vilevile wameeleza kuwa kutakuwa na kamati maalumu itakayokuwa inagawa vitakasa mikono kwa washiriki kwenye vituo maalumu, njiani mpaka mwisho wa mbio, na uwanjani kwa siku nzima ya mashindano. Watoa huduma wote katika vituo vya maji pamoja na uwanjani watavaa barakoa, gloves, aprons na watahakikisha wanatakasa mikono mara kwa mara muda wote wa mashindano

Wamesema hatua hiyo ni kutokana na wingi wa watu watakaoshiriki katika tukio hilo litakalofanyika Februari 28, 2021 Mjini Moshi. Mbio hizi zinafanyika huku kukiwa na madai ya COVID19 kuenea mkoani Kilimanjaro.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro amekanusha madai hayo na kusema mkoa uko salama na magari ya maiti yanayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ni kutoka mikoa mingine.

Pia soma



Kili Marathoni huhusisha ukimbiaji wa mbio fupi/nusu (half marathon) kwa umbali wa Kilomita 21.1 na ndefu/kamili kwa urefu wa Kilomita 42.2.
Kili marathon kwa Hali ilivyo isimamishwe haraka iwezekanavyo.
 
Kampuni ya Kilimanjaro Marathon inayoendesha Mbio maarufu za kila mwaka za “Kili Marathon” zinazofanyika Mkoani Kilimanjaro imetangaza kuwa kutakuwa na zoezi la ugawaji wa barakoa kabla na baada ya mbio kwa wakimbiaji wote wa mbio fupi na ndefu.

Vilevile wameeleza kuwa kutakuwa na kamati maalumu itakayokuwa inagawa vitakasa mikono kwa washiriki kwenye vituo maalumu, njiani mpaka mwisho wa mbio, na uwanjani kwa siku nzima ya mashindano. Watoa huduma wote katika vituo vya maji pamoja na uwanjani watavaa barakoa, gloves, aprons na watahakikisha wanatakasa mikono mara kwa mara muda wote wa mashindano

Wamesema hatua hiyo ni kutokana na wingi wa watu watakaoshiriki katika tukio hilo litakalofanyika Februari 28, 2021 Mjini Moshi. Mbio hizi zinafanyika huku kukiwa na madai ya COVID19 kuenea mkoani Kilimanjaro.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro amekanusha madai hayo na kusema mkoa uko salama na magari ya maiti yanayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ni kutoka mikoa mingine.

Pia soma



Kili Marathoni huhusisha ukimbiaji wa mbio fupi/nusu (half marathon) kwa umbali wa Kilomita 21.1 na ndefu/kamili kwa urefu wa Kilomita 42.2.
Hawaogopi kugawa hizo barakoa,maana mwenye nchi yake anasema kuvaa barakoa ni kuwatia hofu wananchi.
 
Waachwe ujinga, Kuna mtu anaweza kukimbia na barakoa??? Waachwe tamaa waahirishe marathon
 
Kampuni ya Kilimanjaro Marathon inayoendesha Mbio maarufu za kila mwaka za “Kili Marathon” zinazofanyika Mkoani Kilimanjaro imetangaza kuwa kutakuwa na zoezi la ugawaji wa barakoa kabla na baada ya mbio kwa wakimbiaji wote wa mbio fupi na ndefu.

Vilevile wameeleza kuwa kutakuwa na kamati maalumu itakayokuwa inagawa vitakasa mikono kwa washiriki kwenye vituo maalumu, njiani mpaka mwisho wa mbio, na uwanjani kwa siku nzima ya mashindano. Watoa huduma wote katika vituo vya maji pamoja na uwanjani watavaa barakoa, gloves, aprons na watahakikisha wanatakasa mikono mara kwa mara muda wote wa mashindano

Wamesema hatua hiyo ni kutokana na wingi wa watu watakaoshiriki katika tukio hilo litakalofanyika Februari 28, 2021 Mjini Moshi. Mbio hizi zinafanyika huku kukiwa na madai ya COVID19 kuenea mkoani Kilimanjaro.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro amekanusha madai hayo na kusema mkoa uko salama na magari ya maiti yanayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ni kutoka mikoa mingine.

Pia soma



Kili Marathoni huhusisha ukimbiaji wa mbio fupi/nusu (half marathon) kwa umbali wa Kilomita 21.1 na ndefu/kamili kwa urefu wa Kilomita 42.2.
Watanzania wengi wameshagundua Covid-19 ipo sana nchini na wanachukua tahadhari kwa kufuata ushauri wa kisayansi wa wataalam wa nchi za nje na kuachana na ushauri wa vilaza wetu wenye PhD feki. Yule Jaji wa Mahakama Kuu wa Shinyanga alifariki lakini hakuna taarifa iliyotolewa juu ya ugonjwa wake wala kifo chake bali walionyesha kwenye luninga maziko yake Kagera, cha kushangaza wengi waliohudhuria walivaa Barakoa. Mwingine ni yule Jenerali Mbena mstaafu wa Jeshi Dar es Salaam hawakutangaza kuugua kwake lakini wakaonyesha shughuli za maziko lakini washiriki karibu wote ikiwa ni pamoja na Wanajeshi waliokuwa wanabeba Jeneza walivaa Barakoa licha ya Amiri Jeshi Mkuu kuagiza kuwa hakuna Covid-19 nchi nzimà. Meya wa Moshi aliwafukuza mkutanoni wote waliovaa Barakoa kujilinda na kumlinda Mstahiki Meya, lakini kwa agizo toka juu Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro anasisitiza hakuna Covid-19. Miji mingi wakazi waliokuwa wanajifukiza na kula malimao na tangawizi wamegundua haisaidii kitu wamerudia kuvaa Barakoa na kufuata tahadhari zote za kujikinga ambazo walikuwa wamezitupilia mbali kwa agizo toka juu. Civil disobedience inaanza.
 
Back
Top Bottom