Kilichofanywa na Ali Salim dhidi ya Che Malone ni ushamba na ujinga

Kilichofanywa na Ali Salim dhidi ya Che Malone ni ushamba na ujinga

Hivi kama wangekunjana kadi zingehusika?

Naona refa hakuwatilia maanani kisa wako timu moja.
 
Unatetea ujinga wewe TOPOLO. Ule mpira ungeingia nyavuni wa kwanza kulaumiwa angekuwa ni goalkeeper. Alikuwa analinda kuchafuliwa clean sheet yake kutokana na uzembe wa ukuta wa Yeriko.
Kwa hio kumfokea mwenzake kama mtoto ndio ujanja? jana angekua Yondani leo habari zingekua zingine
 
Kama hujawahi kucheza soka unaweza kuona kama ni jambo hatari. Mambo ya kawaida hayo joto la game likipanda
 
Che Malone ni mzito na Kila mechi lazima afanye kosa, Sasa Kuna makosa ya bahati mbaya na makosa ya kusudi.
Beki huwezi kumwacha kipa akutane na mshambuliaji mojakwamoja wakati kipa anatumia mikono.
Che Malone anajiamini kuliko uwezo alionao Sasa ao makipa wamesha msoma na Jana ilikua statement ya wazi.
Yote ni kukumbushana kwaajili ya manufaa ya timu.
Kipa angekua Juma pondamali ndugu Malone ange chezea makofi hdharani.
Ni sahihi, jamaa anafanya uzembe na makosa mengi na ndio maana ni nadra sana Simba kuwa na clean sheet. Ilitakiwa afokewe vile vile.
 
Kama hujawahi kucheza soka unaweza kuona kama ni jambo hatari. Mambo ya kawaida hayo joto la game likipanda
Mara ngapi Ali kafungwa kwa kutema mipira kuna mtu alimfokea? kucheza kama timu maana yake mwenzako anapo kosea una clear mnaelekezana sio kufoka tu ingetosha sio kumsukuma tena mara mbili sio moja hapo unatafta ugomvi
 
Kama hujawahi kucheza soka unaweza kuona kama ni jambo hatari. Mambo ya kawaida hayo joto la game likipanda
Kwani hawakuona wanapongezana mara tu baada ya kuokoa shambulizi hatari Sana.kawaida Sana Ile...ila du nikama kaibu kumsukuma mtu mzima vile
 
Jana kwenye mechi kati ya Simba na Singida tulishuhudia malumbano kati ya mlinda mlango wa Simba Ali Salimu na beki wa simba Che malone baada ya kutokea kosa la kimawasiliano kati yao ambalo kidogo lisababishe goli.

Beki hata kama amekosea kuna namna nzuri ya kumkemea na kumuambia awe makini na sio staili aliyo itumia Ali Salimu jana ule ulikuwa ni udhalilishaji na sio kumkanya beki, cha kushukuriwa ni busara na ustaarabu uliopitiliza wa Che malone tofauti na hapo tungeshudia aibu ya mwaka ya wachezaji wa Simba wakipigana makonde mbele ya hadhara ya mashabiki na wageni rasmi.

Na mbaya zaidi ukijaribu kuangalia kwa umakini lile tukio ambalo kidogo lingesabsbisha goli kosa lilikuwa kwa Ali Salimu mwenyewe kwa kuwa mzito na kuchelewa kuufuata ule mpira aliokuwa ameachiwa na Malone.

Hebu fikiria Alichokifanya Ali Salimu jana angemfanyia mchezaji mwenye akili mbovu kama Kanote, Inonga au Nyoso sasa hivi huyo dogo si angekuwa Muhimbili na mashine za kupumulia akipambania maisha yake?

Huyu dogo inabidi atulize mapepe na ulimbukeni awe ajifunze kuwa na hekima na busara, asidanganywe na kifua chake ipo siku ataingia choo chakike.
Nimekumbuka Onana wa Man u alivoanza na mbwembwe za kumfokea Maguire mara nae akaanza kutoa maboko. Ni ushamba flani wanakuwa nao baadhi ya wachezaji
 
  • Thanks
Reactions: ITR
Kwa tuliopita kwenye shule rasmi za soka tunaweza kufahamu kwamba, kamwe mlinda mlango hatakiwi kuwa mnyonge, au anayebembeleza beki wake.

Anatakiwa kuwa mbabe kwa kiasi cha kutosha. kama ana sauti ya kutosha afoke mpaka uwanja mzima usikie. Ahimize timu kushambulia na kurudi kulinda.

Hata Ayoub naye aliwahi kumfokea Kennedy Juma kwa namna ileile, akimkumbusha anakopaswa kuwa akiwa kwenye nafasi ya kuanzisha mpira golini.

Alimweleza kwa kufoka na ishara za mikono, wakati akitaka kuanzisha Kennedy anapaswa kuwa kwenye boksi la golini kama ilivyokuwa kwa mwenzake Che Malone.

Ova
Mkuu Che malone ni mtu mzima sio unaweza kumuonesha ukali bila kumsukuma na akakuelewa ,kwa kilicho tokea jana kama sio uvumilivu ulio pitiliza wa Che malone tungeshudia maafa.
 
Na ni mbaya sana kum provoque mtu mzima maana hajui jamaa akiwa na hasira huwa anafanya Nini.

Binafs nilipoona clip nilistuka mana jamaa kama angerusha ngumi pale : ukweli wangepigana na ni aibu.

Kuna namna dogo afundishwe nidham na awe responsibile. Wajifunze kwa ayub jamaa ni mstaarabu sna

Jamaa yule dogo kafanya makosa 2

1. Kumfokea mchezaji mwenzie hadharani as yeye ni father

2. Kumshika, that was a turning point afundishwe asifanye hivo Tena maana next time anaweza kuvunjwa shingo na kisheria yeye ndio anashida.

Kuna msemo unasema ongea but usiniguse….. maana ukinigusa you are provoking me and I will act and defend

Mfikishieni huu ujumbe, asioneshe Kama yeye yupo serious kuliko wengine.

Binafsi nimemdharau sana na nilikuwa namuona ni kijana mwenye career path Nzuri kumbe ni uharo kama uharo mwingine

respect to malone, such a gentleman. Kama sio busara zake , jana SSC ingeingia kwenye aibu ya mwaka.

Ongea but don’t touch me , hiyo ni principle hata Mahakaman ; ukianza kunigusa means unahitaji vita na nitakulipua.

Guys kufoka hakukufanyi uonekana upo serious na kazi . Just know how to deliver message in a respect way na utaheshimika



Huyu dogo ni MMAKONDE au yaani ni pure Baribarian( uncivilized society)
Tena bora hata ange msukuma mara moja tu tumgesema labda ni bahati mbaya lakini ali msukuma zaidi ya mara 3 licha ya juhudi za Che malone kujaribu kumuepuka lakini dogo alikuwa anazidi kumfuata huku akimusukuma pamoja na hilo mshikaji alichukulia poa na hilo tukio hali kumtoa mchezoni.
 
Hivi kama wangekunjana kadi zingehusika?

Naona refa hakuwatilia maanani kisa wako timu moja.
Kupigana ndani ya pich ni haramu haijalishi mnatoka timu moja.
 
Kwa tuliopita kwenye shule rasmi za soka tunaweza kufahamu kwamba, kamwe mlinda mlango hatakiwi kuwa mnyonge, au anayebembeleza beki wake.

Anatakiwa kuwa mbabe kwa kiasi cha kutosha. kama ana sauti ya kutosha afoke mpaka uwanja mzima usikie. Ahimize timu kushambulia na kurudi kulinda.

Hata Ayoub naye aliwahi kumfokea Kennedy Juma kwa namna ileile, akimkumbusha anakopaswa kuwa akiwa kwenye nafasi ya kuanzisha mpira golini.

Alimweleza kwa kufoka na ishara za mikono, wakati akitaka kuanzisha Kennedy anapaswa kuwa kwenye boksi la golini kama ilivyokuwa kwa mwenzake Che Malone.

Ova
Anamuiga Diarra, mwenzake huwa hafanyi hivyo b…
Mfundisheni kijana wenu kabla hajakutana na ngoma ngumu akachakaa.
 
  • Thanks
Reactions: ITR
Back
Top Bottom