Kilichomnyima nafasi miss Tanzania 2016 shindano la miss world

Kilichomnyima nafasi miss Tanzania 2016 shindano la miss world

Ningeshauri,miss wa mwaka uliopita ndiye awe Miss atakayeliwakilisha taifa kwenye mashindano ya Dunia.

Namaanisha,Miss Tz 2015 awe ndiye mwakilishi kwa mwaka 2016 na Miss Tz 2016 awe maakilishi Miss World 2017.

Kwa sababu inampa muda mwingi wa kujiandaa,yapata mwaka mzima na kuangalia vipaumbele na changamoto za kukabiliana nazo anavyojiandaa kuliwakilisha taifa.

Pia kamati itapata muda wa Kumfunza na kumshauri katika project yake atakayoiandaa na wadau pia watampa ushauri ili aweze kufanya vema.

Nchi nyingi zinafanya hivyo na ndizo hujitahidi kufanya vema. Miss TZ ni ngumu kushinda kwa sababu hukaa karibia wiki moja pekee kisha huhitajika kiufika kambini kujiandaa na Miss World. Mtu huyu atapata muda upi wa kuandaa project yake ili iwe na ushawishi?

Kwa mantiki hiyo,nashauri Tanzania isiwe na Mwakilishi mwaka ujao badala yake MissTz 2017 awe mwakilishi mwaka MW 2018.

Nawasilisha.
tushafanya hvyo tumeshindwa pia!
 
Tuseme zile comments zetu za Tanzania hazikusaidia kitu dadadadeki hizi digisu hizi
 
Atarudi na hasira sasa akahamasishe masai kamata wembe kiswa sawa.
 
Dadaangu ni lini waTz walishindwa kwenye mashindano yoyote wakakosa wakumtupia lawama na kusingizia kafanya figisu.
Outfit za diana nazo very cheap.
yasemekana mavaz yalikua ya kuunga unga pia!
 
Miss Kenya hata nguo zake unaona nzuri unaweza ukasema walitumia mda wakajipanga,Miss wetu wamemtoa kama kinyago hawaja m polish anaongea vijembe kwenye net yani anatakiwa apewe mafunzo yakutosha,mfano ebu angali nguo alorudi nayo ,ametoka Airport nje pale utasem alitoka kijijini au yuko hapa hapa ameingia na local flight jamani,watu wasishindwe nakupika wakasingizia moshi,kamati ya Miss Tanzania wajipange na wajifunze kutokana na makosa full stop.
 
Tanzania hatuna historia ya kujiandaa kwenye mashindano yoyote tunasubiri kukurupuka matokeo ndio kama hayo
Kusema ukweli huyu msichana hana uzuri asilia. Makeup nyingi, lipstick, wanja na nywele za bandia! Imagine ana 18years anasidiwa na uzuri wa dukani si sahihi. Wanaotumia makeup ni wenye makunyanzi ya uzee siyo binti wa 18 wanayesema maji bado yanatembea usoni! Huwezi kumnyima mhindi, mvenezuala mwenye nywele asili ukampa mwenye za bandia! Watanzania tuende kushindana tukiwa halisi kama Flavian Matata. Uzuri fake, bandia haufai. Hebu mchekini Teresia Shayo enzi hiyo ya analogia.
 
Kamati ya miss Tanzania ni ya kiujanja ujanja tu.wababaishaji na ma TP lindanda.
 
Back
Top Bottom