Elections 2010 Kilichonishtua Juu Ya Dr Slaa Pale Mwembetogwa

Elections 2010 Kilichonishtua Juu Ya Dr Slaa Pale Mwembetogwa

Maggid amamuelezea JK kama wale watu wa Cabinda kule Angola walivyokuwa wanamsifia Savimbi. Eleza ukweli bwana. JK mbona ni kama ameshindwa. Anachojaribu kufanya ni kukamilisha ratiba halafu historia ndio itamuhukumu.
 
Kinachomsumbua Mjengwa ni njaa tu.......Ukiwa na njaa huna mawazo huru!
Kama kazi ya kuandika balanced news umeshindwa muombe Muhingo uingie kwenye Team ya Campaign!

Adui yako muombee njaa. Huu ndio wakati ambao hawa waandishi uchwara wanaombea ufike maana kwa maandishi yao haya yasioeleza jinsi hali halisi ya mambo ilivyo ndio wanashiba na kuvimbiwa na watoto kwenda shule. Mjengwa is one of them. Anajaribu kumfanya JK kama ni malaika ambaye amefanya yaliyotukuka tu.
 
Hii nchi ina watu na vitu vya kukera sana.

Kwamba mtu kafanya upuuzi kama huo, halafu apewe state reception? Naamini kama tungekuwa na viongozi 10 tu kama Dr Slaa tungeanza mwendo mdundo kufukuzana na Tigers wa Asia. Sasa kwa umaskini huu na uozo uliojaa kwenye jamii tunataka kuendekeza mila za kuwaficha wahalifu? CHADEMA waendelee hivyo hivyo ili watu waone tofauti yao na majambazi wa CCM
 
Maggid mwenyewe ameondoka si tunabaki kuvutana mashati kama wasio na akili, Hivi ni mara ngapi tukubaliane kama
huyu mtu ni wa kumpuuza?!.
 
sasa kama yeye kapiga makofi kushangilia we inakushusu nini?ni nini kilichokujaza ufunguo ukaona kadhalilishwa ilhali yeye mwenyewe hana tatizo na kallikubali kwa kujipigia makofi..........aagh hembu jiondokee bana.
 
Tatizo la Majjid ni cut and copy attitude aliyokuwa nayo. Ulicopy blog ya Michuzi weee, kidogo tu ujiite "Ankal Majjid", sasa umeona Mithupu anafaidika na system na wewe unasogeze zipu ili CCM waifungue kirahisi-- be real, baada ya tarehe 31 October, wasomaji wa blog watarudi kusoma habari zile zile kabla ya uchaguzi, but kwenye blog tofauti kwa kuwa hizi blog zenu zimeonyesha kutakuwa an ethics za uandishi wa habari. Kama unabisha aungalia blog ya JIACHIE ilivyo juu sasa hivi. Dogo ameamua kuwa fair na it pays off.

Wewe kilichokupeleka Mkutanoni- Mwembetogwa ni nini? wewe ni chadema, au independent voter? Wewe ni CCM hili halina ubishi, sasa ulienda kufanya nini. Na what coincidence kujikuta umekaa karibu na kiongozi huyo wa chadema aliyesemewa ukweli na Dr Slaa. Cha kustaajabisha, wewe ulikuwa umekaa kumuangalia kama atalia au atapiga makofi? Interest yako ilikuwa nini? au ulijau Dr Slaa atalisema hilo? Na kama yeye hakushituka sana akaweza hata kupiga makofi, wewe unachoshituka ni kitu gani, kinakuhusu nini? Mbona unadanganya watu kaka. Tatizo lako ni shule ndogo, na wivu, umaskini wako hautaisha kwa njia hiyo. Kaimarishe blog yako, kwa sababu inabore, is like family album, who cares what you do Majidd. Si uweke huo ujinga wako kwenye face book. Blog lazima ifuate sheria na ethics za uandishi wa habari, la sivyo make it a page kwenye face book au twitter!!

Makala kama hii na ile uliyoandika sijui kuwa CUF watakuwa No 2, ni upuuzi na ya kufikirika. Huwezi ukaandika uchambuzi kama huo ukiwa umelala kitandani na mkeo. Ulinikera pale uliposema kuw CUF wana nguvu Lindi na Mtwara, lakini hukusema kuwa Chadema wana nguvu nchi nzima, na zaidi kaskazini? Just keep opinion zako by yourself, we dont want to hear your crap!! Grow up, mrugaruga !!
 
Mjengwa,

Naona sasa umeamua kuandika vitu visivyo na vichwa wala miguu. Ni jambo la kusikitisha sana kuona Mwandishi kama wewe unaingia katika ushabiki na kukiuka miiko ya taaluma yako. Kwa hiyo Mjengwa, wewe unaona Dokta kumsema mtu aliyekisubbotage chama ni jambo baya; lakini, Rais kumkumbatia mtuhumiwa wa kesi wa Rushwa aikukushtua kabisa ? Hivi unajua kitendo kile kitakuwa na impact gani kwa hakimu anayetakiwa kutoa maamuzi ya kesi? Na jee kitendo cha Kikwete kumembrace Mwakalebela kinatuma ujumbe gani kwa TAKUKURU ?

Mbaya zaidi matendo haya yalitokea wakati wewe ukiwepo uwanjani na ukusema lolote! Mjengwa, nasikitika kusema ya kuwa kwa muda siku chache hizi umeonyesha unafiki uliokubuhu .

http://www.globalpublishers.info/profiles/blogs/mwakalebela-avunja-kambi-mbele?xg_source=activity


 
Nakupa pole Maggid maana umeshukiwa kama kifaranga cha kuku kinavyoshukiwa na mwewe. Hata hivyo, maoni yalotolewa yamekusaidia (kama kweli umeegemea kambi nyingine dhidi ya Dk Slaa). Hata hivyo bado kuna wachangiaji wengine wamekuwa wakali kama pilipili lakini ukweli Tanzania tunahitaji sana Uongozi mbadala; NAISUBIRI SIKU HIYO CCM ITAKAPOANGUKA, NAISUBIRI SIKU HIYO KAMA MLINZI ANAVYOISUBIRI ASUBUHI IPAMBAZUKE.
 
Maggid,
Wakati mwalimu Nyerere alipoona mzee Malecela haendi vizuri wala hakusita kumtaja hadharani wakati huo Malecela akiwa waziri mkuu na hadharani hapo hapo akamshauri rais amuondoe madarakani na ikafanyika hivyo, ili kulinda heshima ya CHAMA. Na si hivyo tu alimtungia na kitabu na mpaka leo kinasomwa na kila mmoja. Kulinda heshima ya CHAMA.


Hii unayotaka kutuambia ni ubabaishaji uliotufikisha hapa tulipo. Mtu kafanya sabotage eti asisemwe hadharani? Mtu kashusha heshima ya chama sirini eti asisemwe hadharani? Wewe unajua heshima ya Dr Slaa imeletwaje? Kusema hadharani bila kificho. Ukiiba mali ya umma wasemwa hadharani, ebu niambie sasa, mbona yeye kasemwa hadharani kwa kisa cha mchumba? Acha hizo bana!

Na wewe Maggid wajuaje kwamba mpaka anamtaja hadharani bado vikao vya ndani vya chama havijafanyika? Ukifanya ujinga wacha jamii ikufahamu na hata watoto wako na familia yako wakufahamu na upate hukumu ya haki.

Asante Mchukia Ufisadi kwa jibu lako. Mtu utende jambo hadharani na kusaliti maslahi ya umma halafu tuanze kukupeleka chumbani! Kuna mambo ya kufanya kwenye vikao vya ndani na vingine nje ya vikao. fikiria mtu amechukua fomu kwa niaba ya chama na akaacha kurejesha baada ya kuhongwa mnadhani atakuja kwenye vikao vyenu vya ndani?

Mambo ya ndani ni kama yale yanayohusu ndoa ya mtu kwa sababu ni ya binafsi, lakini mengine yamewahi kuletwa humu kama vile yana maslahi ya umma. tuwe macho na hawa watu kama Maggid wanaopima uwezo wa watu kufikiri na kudhalilisha ufahamu wetu.

Maggid anajifanya mshauri wa Chadema ili kuwapotosha wenye uelewa mdogo. Endelea kubuni njia zingine, hiyo uliyoibuni bado haikidhi haja.
 
Maggid,
Wakati mwalimu Nyerere alipoona mzee Malecela haendi vizuri wala hakusita kumtaja hadharani wakati huo Malecela akiwa waziri mkuu na hadharani hapo hapo akamshauri rais amuondoe madarakani na ikafanyika hivyo, ili kulinda heshima ya CHAMA. Na si hivyo tu alimtungia na kitabu na mpaka leo kinasomwa na kila mmoja. Kulinda heshima ya CHAMA.

Hii unayotaka kutuambia ni ubabaishaji uliotufikisha hapa tulipo. Mtu kafanya sabotage eti asisemwe hadharani? Mtu kashusha heshima ya chama sirini eti asisemwe hadharani? Wewe unajua heshima ya Dr Slaa imeletwaje? Kusema hadharani bila kificho. Ukiiba mali ya umma wasemwa hadharani, ebu niambie sasa, mbona yeye kasemwa hadharani kwa kisa cha mchumba? Acha hizo bana!

Na wewe Maggid wajuaje kwamba mpaka anamtaja hadharani bado vikao vya ndani vya chama havijafanyika? Ukifanya ujinga wacha jamii ikufahamu na hata watoto wako na familia yako wakufahamu na upate hukumu ya haki.

Kaka natumai Dr Slaa atakuwa tayari kumtaja hadharani yule kiongozi wa CHADEMA kule Kigoma ambako amekuwa mbele kusabotage kampeni za mgombea wao na pia atamtaja aliyemhonga zile milioni kadhaa ili mgombea huyo aanguke.....
 
We mkaka ukiendelea kutuletea tuuchambuzi uchwara hapa tutaanza kukuona mtako.
 
Maggid umeshangazwa tu na kauli ya Dr Slaa alipomuambia Mzee Kapwani kuhusu kutorudisha fomu za kugombea Ubunge jimbo lam Isimani hivyo kumfanya Mzee Lukuvi atangazwe kapita bila kupingwa?

LKN HADI LEO MWANDISHI MJENGWA BADO HAJASHANGAZWA NA KITENDO CHA RASI JK KUWA KARIBU NA MTUHUMIWA WA RUSHWA MWAKALEBELA HATA AKAMUITA JUKWAANI ILI AWASALIMIE WANANCHI WA MANISPAA YA IRINGA KTK ETI KUJARIBU KUSULUHISHA MAKOVU YALIYOACHWA NA KURA ZA MAONI;Kumbukumbu zinaonyesha MAGGID NI MKAZI WA MJI HUO!

Maggid kwa kwa kweli huwa unanishangaza sana na analysis zako;Maggid pengine ni mkereketwa wa CCM hapo Iringa hata zaidi ya Dr Kleruu kama angekuwa hai!
 
Maggid, unalo hilo bwana mdogo. Waliokutuma walidhani una guts kama Malaria Sugu kumbe walikosea. Mwenzio MS hata akianzisha thread iliyojaa upuuzi anaitetea hadi mwisho kama aliyepandwa na malaria kichwani,wewe uwezo huo huna hivyo utapigwa Termination sasa hivi. Unafanya mchezo na hao waliokutuma? Jifunze kaka! unafiki haulipi. Njoo na hoja ambazo hata nafsi yako inaziamini sio hoja mashariki nafsi magharibi. Wewe bado kijana mdogo unahitaji mabadiliko ya kifikra. Pole sana kama nimekukwaza ila habari ndio hiyo.
 
Ndugu yangu Maggid,

Hivi mtu aliyedhalilishwa mbele ya hadhara na yeye mwenyewe akiwepo, angepiga makofi?

Prof. Lipumba akiwa Jimboni kwa Membe alimtuhumu mgombea wa CUF kwamba alihongwa na Membe ili asirudishe fomu na hayo yaliandikwa magazetini.

JK amekuwa akiwakejeli na kuwazushia maneno kibao wale wote waliohamia upinzani baada ya kutoswa kwenye kura za maoni within CCM.

Katika cases hizo mbili za Lipumba na JK sijakusikia ukisema umeshitushwa, ila Dr. Slaa kumtuhumu Mwenyekiti wa CHADEMA (mkoa) imekuwa nongwa?

Hivi Mwenyekiti wa Chama ngazi ya mkoa anaposhindwa kurejesha fomu ya kugombea bila sababu ya kueleweka, what kind of a msg anapeleka kwa wanachama na wagombea wengine ndani ya mkoa? Mwenyekiti wa Mkoa alitakiwa awe mfano kwa wagombea wote wa Ubunge na Udiwani kwenye huo mkoa, arejeshe fomu na kuhakikisha wengine wote wamerejesha kwa muda unaotakiwa zikiwa zimekamilika/bila mapungufu.

Ninaziona juhudi zako za kumchimba Dr. Slaa, lakini naona kuna mengine unaishia kujidhalilisha mwenyewe au kujionyesha wazi zaidi kwamba una malengo hasi kwa mgombea Urais wa CHADEMA. Bora ukae kimya au utoe declaration kwamba wewe ni mmoja wa wapenzi wa CCM na hivyo whatever utakachokisema hakuna ambaye atakichukulia serious.
 
Kaka natumai Dr Slaa atakuwa tayari kumtaja hadharani yule kiongozi wa CHADEMA kule Kigoma ambako amekuwa mbele kusabotage kampeni za mgombea wao na pia atamtaja aliyemhonga zile milioni kadhaa ili mgombea huyo aanguke.....
Omarilyas,
Hii ndio tunapigia kelele hapa. Kama unawafahamu watu hapa na una hakika si taja kwa majina? Huu ndio ujasiri wa hapa JF "dare to talk openly"
Lakini naona unaturudisha kwa Maggid huko huko.
Just talk. Sema ni fulani na fulani!
 
Ndugu yangu Maggid,
Katika cases hizo mbili za Lipumba na JK sijakusikia ukisema umeshitushwa, ila Dr. Slaa kumtuhumu Mwenyekiti wa CHADEMA (mkoa) imekuwa nongwa?
Msameheni maana hao wengine hakuwasikia ila amemsikia Dr Slaa tu maana yeye uishi Iringa tu, na kuripoti mambo ya Iringa tu.
 
Maggid, hiyo habari ya kuogopa kudhalilishana ndiyo iliyoifikisha nchi yetu hapa. Kama wewe umeona kwamba uliyoelezea ni mapungufu basi umekosea. kwa kiasi kikubwa hiyo ni strength ya Dr Slaa kwamba hana muda wa kumwangalia mtu usoni. Anayevurunda anashughulikiwa instantly. Na huyo ndiye kiongozi tunayemtaka. Siyo kiongozi anayesema akikamata mafisadi nchi intatikisika. What a shame. Hongera Dr Slaa kwa kuonyesha ujasiri huo bila unafiki.

Maggid, Dr Slaa alipoongea alikuwa na ushahidi wa kutosha na hakukuwa na muda wa kuunda kamati ya kumchunguza huyo bwana. Kwanza elewa kitendo cha kuaminiwa na Chadema halafu kuwapiga panga la kisogoni ni usaliti usiovumilika. Yaani kuna wananchama maelfu waliitaka nafasi hiyo lakini mjinga unayemtetea akafanya mradi. Huyu bwana angepewa mkataba wa nchi angefanya vivyo hivyo. Mjengwa angalia vitabu vya dini zote uone jinsi wasaliti wanavyo ongelewa,hata kama huamini dini waulize wapagani usaliti maana yake ni nini. Kwa taarifa yako huyo bwana ananafuu yupo Tanzania,ingekuwa nchi zingine za dunia hii pengine haditihi hii ingekuwa tofauti.
Mjengwa,unachotaka kutuambia hapa ni utaratibu wa CCM, wakuficha mambo kwa mgongo wa vikao vya ndani. Hebu nikuulize Richmond imeishia wapi. Chadema wao wanasema kiongozi awe safi, yale ya vikao vya chama yanajulikana,lakini hili la msaliti, hata jeshini hasubiriwi anakula kitu cha shaba.Period. Anachosema mjengwa ni utaratibu wa CCM ambapo mkuu wa kamati ya maadili [mzee wa vijisenti] eti ndiye anamjadili mzee wa Richmondulli!!! Yaani majidi anataka tufuate utartibu wa Nyani, kumjadili tumbili kisa kala mahindi ya binadamu kwa kushirikiana na ngedere. Sikujua mtu kama Maggid angeweza kufikiri kiwango kidogo namna hii. Huyo bwana wa Iringa amekuwa mfano mzuri kwa mkewe na watoto wake,pamoja na wajinga woote waliorubuniwa na kukimbia na fomu. In fact alitakiwa achapwe viboko mbele ya kadamnasi. Kwa umasikini tulionao na jitihada zinazofanyika kutukomboa fidhuli kama huyo bwana hastahili heshima hata inayolingana na tundu la choo. Sijui Maggid anaelewa watu wanaposema Spade is a Spade not a big spoon. Mjengwa kulindana lindana kipuuzi unakokutetea ndio kumelifikisha taifa hapa lilipo. Tena kuwa mtanzania ni Bahati, maana China ni risasi na bili inapelekwa kwa familia yako. Castro aliwahi kuidhinisha rafiki yake mwanamapinduzi alimwe risasi kwa kukiuka maadili tu na wala si usaliti. Mjengwa bado anataka mazungumzo ya uani.
Maggid, si unajua Dr Slaa aliwasilisha mada bungeni kuhusu mafisadi, wakaiteka ili walindane huko kwenye vikao vichafu, alipoipeleka mwembeyanga hata wewe umejua uchafu unaotutia umasikini huu, bado tu Maggid anataka turudi kule tulikotoka.Mungu wangu!
 
Hapa ni kama yale ya Ilala enzi zile. Hii ya leo ni kama vile mtu unatembea kwa miguu peke yako kutoka viwanja vya Jangwani kupandisha kwenda Magomeni Mapipa. Juu mlimani unakutana na umati wa watu wanashuka kwa miguu kutoka Magomeni Mapipa kwenda Viwanja vya Jangwani. Ni lazima utasababisha majadiliano kwa wanaoshuka jangwani. Na hiii ndio staili ninayoitumia hapa katika kuamsha fikra.

Katika Uchaguzi wa mwaka 2005 niliandika makala kwenye Rai kuwakemea wale waliokuwa wakimbagua Dr Salim kutokana na rangi yake. Niliamini na bado naamini kuwa hawakumtendea haki. Dr Salim ni Mtanzania mwenzetu, hakukuwa na sababu za kuja na hoja za uhizbu na mengineyo.

Kuna mwandishi wa habari akaandika makala kwenye gazeti moja la kila wiki kunizushia mambo ya uongo yenye sura ya uchochezi. Aliandika mambo ya kunigombanisha mimi na wenyeji wa Iringa wa kabila la Wahehe. Ilikuwa ni stori ya uongo toka mwanzo hadi mwisho. Na kibaya zaidi mwandishi yule akafikia hata kutoa nukuu ya niliyoyaandika kwenye Rai. Nukuu kutoka kichwani mwake na si kile nilichoandika.

Nikamwandikia mhariri wa gazeti lile kumwomba kiungwana afanye mambo mawili; mosi, aniombe radhi kwa kuchapa taarifa ya kuniomba radhi ukurasa wa mbele wa gazeti lake katika matoleo matano mfululizo. Pili, achapishe makala halisi niliyoiandika katika Rai.

Kwamba asingefanya hivyo, basi, ningefikiria hatua zaidi za kuchukua. Mhariri alinielewa na akatekeleza ombi langu hilo.

Hoja hapa ni kwa nini tunatakiwa kuwa waangalifu katika kuandika na kutamka mambo ambayo kimsingi yanaweza kuwaletea wengine madhara, ya kijamii au hata kiuchumi. Pamoja na mimi kuombwa radhi mara tano na gazeti lile, bado naamini kuwa kuna Wahehe wa Iringa waliosoma makala ile potofu na hawakusoma kingine tena baada ya hapo. Kwao, mimi nabaki kuwa ni yule mchochezi na niliyewadharau Wahehe. Itabaki hivyo daima. Ni hasara kwangu.

Mi nafikiri katika wakati huu mijadala kama hii ina umuhimu. Aliyetuhumiwa na kuhukumiwa pale Mwembetogwa ni mtu mdogo sana katika nchi hii. Amehukumiwa hadharani na mgombea urais bila kupewa nafasi ya kujitetea. Labda habari zake ndio kwanza mnazisoma humu.

Nafikiri ni muhimu hata hao tunaokwenda kuwachagua nao wajue tunafikiri nini juu yao, maana wanakwenda kubeba dhamana kubwa. Kwa kufanya hivyo, tutawapa nafasi ya kutafakari yale ambayo huenda wasingeyatafakari kama si kuibuliwa mijadala kama hii. Mimi sitachoka kuanzisha mada na kuchokoza mijadala, kwa staili hii hii, na ni kuhusu mambo mbali mbali ninayoyatafakari ili tutafakari pamoja.
 
Hapa ni kama yale ya Ilala enzi zile. Hii ya leo ni kama vile mtu unatembea kwa miguu peke yako kutoka viwanja vya Jangwani kupandisha kwenda Magomeni Mapipa. Juu mlimani unakutana na umati wa watu wanashuka kwa miguu kutoka Magomeni Mapipa kwenda Viwanja vya Jangwani. Ni lazima utasababisha majadiliano kwa wanaoshuka jangwani. Na hiii ndio staili ninayoitumia hapa katika kuamsha fikra.

Katika Uchaguzi wa mwaka 2005 niliandika makala kwenye Rai kuwakemea wale waliokuwa wakimbagua Dr Salim kutokana na rangi yake. Niliamini na bado naamini kuwa hawakumtendea haki. Dr Salim ni Mtanzania mwenzetu, hakukuwa na sababu za kuja na hoja za uhizbu na mengineyo.

Kuna mwandishi wa habari akaandika makala kwenye gazeti moja la kila wiki kunizushia mambo ya uongo yenye sura ya uchochezi. Aliandika mambo ya kunigombanisha mimi na wenyeji wa Iringa wa kabila la Wahehe. Ilikuwa ni stori ya uongo toka mwanzo hadi mwisho. Na kibaya zaidi mwandishi yule akafikia hata kutoa nukuu ya niliyoyaandika kwenye Rai. Nukuu kutoka kichwani mwake na si kile nilichoandika.

Nikamwandikia mhariri wa gazeti lile kumwomba kiungwana afanye mambo mawili; mosi, aniombe radhi kwa kuchapa taarifa ya kuniomba radhi ukurasa wa mbele wa gazeti lake katika matoleo matano mfululizo. Pili, achapishe makala halisi niliyoiandika katika Rai.

Kwamba asingefanya hivyo, basi, ningefikiria hatua zaidi za kuchukua. Mhariri alinielewa na akatekeleza ombi langu hilo.

Hoja hapa ni kwa nini tunatakiwa kuwa waangalifu katika kuandika na kutamka mambo ambayo kimsingi yanaweza kuwaletea wengine madhara, ya kijamii au hata kiuchumi. Pamoja na mimi kuombwa radhi mara tano na gazeti lile, bado naamini kuwa kuna Wahehe wa Iringa waliosoma makala ile potofu na hawakusoma kingine tena baada ya hapo. Kwao, mimi nabaki kuwa ni yule mchochezi na niliyewadharau Wahehe. Itabaki hivyo daima. Ni hasara kwangu.

Mi nafikiri katika wakati huu mijadala kama hii ina umuhimu. Aliyetuhumiwa na kuhukumiwa pale Mwembetogwa ni mtu mdogo sana katika nchi hii. Amehukumiwa hadharani na mgombea urais bila kupewa nafasi ya kujitetea. Labda habari zake ndio kwanza mnazisoma humu.

Nafikiri ni muhimu hata hao tunaokwenda kuwachagua nao wajue tunafikiri nini juu yao, maana wanakwenda kubeba dhamana kubwa. Kwa kufanya hivyo, tutawapa nafasi ya kutafakari yale ambayo huenda wasingeyatafakari kama si kuibuliwa mijadala kama hii. Mimi sitachoka kuanzisha mada na kuchokoza mijadala, kwa staili hii hii, na ni kuhusu mambo mbali mbali ninayoyatafakari ili tutafakari pamoja.

Maggid,
Wewe una hakika gani hakupewa nafasi ya kusikilizwa? Mbona hujasema kwa nini alikuwa akipiga makofi pamoja na kushambuliwa? Yaani huu mjadala hakuwa na la maana ndio sababu umeshambuliwa na kila mmoja. Mbona hakuna mahali wewe kama mwandishi umesema ulikwenda kumuhoji Dr Slaa na yule bwana aliyeshambuliwa jukwaani ili uje na uhakika wa alichosema?

Mimi nimekuwa mmoja wa wasomaji wa makala zako kule Rai ya zamani (sio hii ya sasa), na kama unaendelea kuishi kwa matakwa ya Rai ya sasa hivi tutaendelea kukushambulia unapoleta mijadala isiyo na kichwa wala miguu eti kwa sababu wewe ni mwandishi. Hata hayo ya kulishitaki gazeti uliyoandika humu hayana sababu maana ukishaandika vitu vya hovyo bila kufikiri haya ndio matokeo yake. Pole.
 
Back
Top Bottom