Kilichozuia kufanyika kwa Sherehe za Uhuru wa Tanganyika kwa miaka mitatu iliyopita kimekwisha ?

Kilichozuia kufanyika kwa Sherehe za Uhuru wa Tanganyika kwa miaka mitatu iliyopita kimekwisha ?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Nchi yeyote inayothamini Uhuru wake huadhimisha siku iliyopata Uhuru huo kutoka kwa wakoloni weupe au weusi kwa shangwe kuu iliyotukuka , hii ni siku ambayo nchi husika husherehekea minyororo ya utumwa kukatwa , nchi zilizopambana kupata uhuru huo kwa vita , huwakumbuka mashujaa wao waliokufa kwenye mapambano ambayo hatimaye yalileta ukombozi wa kweli , kwa kifupi siku kama hii ni siku Tukufu .

Baada ya awamu ya 5 kuingia madarakani ilikuja na mpango tofauti wa kusherehekea siku hii , sherehe na shamrashamra zilizoambatana na gwaride pamoja na halaiki vilizimwa kwa maelezo ya kuokoa pesa ili kujazia maendeleo ya nchi , ikiwemo kujenga barabara kadhaa , hospitali na shule .

Sikuwa na mgogoro wowote na jambo hili kutokana na " uzito " wa sababu zilizoelezwa na wakubwa ili kuhalalisha mpango wao wa kutoadhimisha siku hii kama ilivyozoeleka , bali kilichonishangaza ni kuona mwaka huu yakifanyika maandalizi makubwa ambayo bila shaka yametumia gharama kubwa ili kufanikisha maadhimisho haya Jijini Mwanza , ambako karibu kila kiongozi wa Taasisi kubwa ndani ya nchi hii amehudhuria , tena kwa gharama kubwa mno !

Swali langu ni hili : Je kilichokwamisha sherehe hizi miaka yote hii sasa kimetatuliwa ?

Naomba kuwasilisha .
 
Nimefurahi rais kutupiliambali ombi la mbowe eti maridhiano , mbowe amalize kesi zake na mahakama ndio aje aombe
Amesababisha maafa leo anajifanya mwema akaozee jela


USSR
 
Siku hizi mpaka Jana jiji LA dar lilikua safi, hivyo hatufanyi usafi ndio maana hii sherehe inasherehekewa!
 
Nakumbuka mwaka juzi sherehe za uhuru zilifanyika dodoma

Au nimechanganya madensa?

Kilichofanyika dodoma mwaka juzi kilikuwa kitu gan

Samahan waungwana naomba kujua

Kipindi kile hadi babu seya akaachiwa na dodoma ikatangazwa kuwa jiji

Zilikuwaga sherehe gan zile

Asanten
 
Nakumbuka mwaka juzi sherehe za uhuru zilifanyika dodoma

Au nimechanganya madensa?

Kilichofanyika dodoma mwaka juzi kilikuwa kitu gan

Samahan waungwana naomba kujua

Kipindi kile hadi babu seya akaachiwa na dodoma ikatangazwa kuwa jiji

Zilikuwaga sherehe gan zile

Asanten
Mwaka jana je ?
 
Kwani mada inahusu nini?? Katika miaka minne yake sherehe zimefanywa mara mbili na hazijafanyika kwa magwaride mara mbili!

Wewe ulikua unataka kusemaje?
 
Nchi yeyote inayothamini Uhuru wake huadhimisha siku iliyopata Uhuru huo kutoka kwa wakoloni weupe au weusi kwa shangwe kuu iliyotukuka , hii ni siku ambayo nchi husika husherehekea minyororo ya utumwa kukatwa , nchi zilizopambana kupata uhuru huo kwa vita , huwakumbuka mashujaa wao waliokufa kwenye mapambano ambayo hatimaye yalileta ukombozi wa kweli , kwa kifupi siku kama hii ni siku Tukufu .

Baada ya awamu ya 5 kuingia madarakani ilikuja na mpango tofauti wa kusherehekea siku hii , sherehe na shamrashamra zilizoambatana na gwaride pamoja na halaiki vilizimwa kwa maelezo ya kuokoa pesa ili kujazia maendeleo ya nchi , ikiwemo kujenga barabara kadhaa , hospitali na shule .

Sikuwa na mgogoro wowote na jambo hili kutokana na " uzito " wa sababu zilizoelezwa na wakubwa ili kuhalalisha mpango wao wa kutoadhimisha siku hii kama ilivyozoeleka , bali kilichonishangaza ni kuona mwaka huu yakifanyika maandalizi makubwa ambayo bila shaka yametumia gharama kubwa ili kufanikisha maadhimisho haya Jijini Mwanza , ambako karibu kila kiongozi wa Taasisi kubwa ndani ya nchi hii amehudhuria , tena kwa gharama kubwa mno !

Swali langu ni hili : Je kilichokwamisha sherehe hizi miaka yote hii sasa kimetatuliwa ?

Naomba kuwasilisha .
Kamanda mbowe kanyoosha mikono juu anataka maridhiano.
 
Japo sijamuona kikwete!!LAKINI LEO ulikuwa mpango wa kumsimika jiwe kugombea 2020!LOWASA KAMALIZA KABISA KAMPENI NDANI YA CHAMA!!hakuna sherehe wala nini!!!ile ni kampeni ya kuhalalisha udikteta nchini!!!POLE KIKWETE KWA KUTUINGIZA MKENGE!!!!
 
Japo sijamuona kikwete!!LAKINI LEO ulikuwa mpango wa kumsimika jiwe kugombea 2020!LOWASA KAMALIZA KABISA KAMPENI NDANI YA CHAMA!!hakuna sherehe wala nini!!!ile ni kampeni ya kuhalalisha udikteta nchini!!!POLE KIKWETE KWA KUTUINGIZA MKENGE!!!!
Lowassa ile kichwa nadhani kuna fuse kidogo zina shida sehemu.
 
Back
Top Bottom