Kilimanjaro: Binti adaiwa kumuua mama yake kisha kumng’oa macho

Kilimanjaro: Binti adaiwa kumuua mama yake kisha kumng’oa macho

tyc

JF-Expert Member
Joined
Feb 25, 2014
Posts
1,179
Reaction score
2,971
1625650432653.png

Mwanafunzi wa kidato cha nne Shule ya Sekondari Kindi Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro anadaiwa kumuua mama yake mzazi, Marietha Mushi (62) kwa kumnyonga na shuka, kisha kumpiga na kitu kizito kichwani na kumng’oa macho.

Habari zinaeleza kuwa mama huyo alikuwa na ulemavu wa mkono jambo linalodaiwa kuchangia ashindwe kujitetea wakati akishambuliwa na binti yake huyo.

Akizungumza na Mwananchi Digital Jumanne Julai 6, 2021 mkuu wa Wilaya ya Moshi, Said Mtanda amesema tukio hilo limetokea Julai 5, 2021 eneo la Kibosho Sambarai.

"Mtoto amemuua mama yake na mtoa taarifa ambaye ni kaka wa marehemu ameeleza kuwa alibaini kuuawa kwa dada yake kwa kunyongwa na shuka kisha kupigwa na kitu kizito kwenye paji la uso. Alisema aling’olewa macho na huyu mwanaye wa kike ambaye anasoma kidato cha nne,” amesema Mtanda.

Amesema mwanafunzi huyo amekamatwa na uchunguzi wa Polisi unaendelea

Source: Mwananchi Newspaper
 
Binti mdogo halafu kamuua mama yake,kamnyonga,halafu baada ya kufa kampiga na kitu kizito,halafu kamtoa na macho,hapa uchunguzi wa kina unahitajika kwanini ampige na kitu kizito baada ya kumnyonga,na hayo macho kwanini kayatoa kama lengo lilikuwa ni kumuua tu...?
 
Acheni hizi hukumu za kimakundi na kikabila.
Unataka kusema hakuna watu wema uchagani au watu wabaya kwenye kabila lako?
NB: Mimi siyo mchagga.
Watu bwana!!!!!....kila kabila lina waovu na wema....kikisikika kitu kibaya (hasa kuhusu wanawake) utasikia wanawake wa kichaga sio wazuri...
 
Uchunguzi ufanyike aisee... Mama ni mlemavu mtoto ni binti tena form four amng'oe mama ake macho it doesn't make sense kuna mtoa kafara hapo maiki za media na camera zao hazijammulika
Taarifa inatolewa na Dc badala ya polisi unategemea itakuwa na details za kueleweka?
 
Back
Top Bottom