Kilimanjaro Moshi Ni sehemu ya adabu kuliko mikoa yote.

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Huwezi kufananisha Moshi na sehemu Kama mwanza.hii Ni kwa sababu Moshi yote ametapakaa mchaga.hakuuzii ardhi yake kizembe.anaweza akawa ana nyumba na asikupangishe akigundua we Ni mtu wa kabila lingine ukienda kichwa kichwa.wanajielewa Sana.si mtoto mdogo SI mtu mkubwa wote Ni wasafi.ukikamatwa umetupa taka faini 50000 na hawana masiara kabisa.ninachowapendea wanakula vizuri maziwa mgando,ndizi,maparachichi,kahawa,kuku.ndo maana wengi wao wanaishi miaka mingi
Pia wahaya wanajitahidi na wanyakusya wanazingatia Sana
 
Sawa tumekusikia,ngoja tusikie na wengine wanasemaje..
 
Uzi wa kikabila huu, haya subiri wachaga wenzio waje wakusapoti.

Tanzania ni moja.
 
Sisi wengine tumezaliwa, tumekua na tunaishi huko ulipo sema na wazee wanamiliki ardhi, nyumba...... japo kwetu ni lake zone. Unapo andika vi_ habari vya namna hii mi nakuona kama mtoto. Grow up boy muwe mnaandika ukweli wacha kujisifu uongo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari ya kutupa taka ni katikati ya mji tu ndio mamlaka hufatilia ambàpo unaweza tembea kwa miguu kwa masaa mawili ukapamaliza kote, hapo majengo watu wanatupa tu uchafu kwa kwenda mbele, maimorial ndio kuchafu balaa. Moshi ina mazuri mengi sana ambayo ndio pekee hutajwa, madhaifu ni mengi mno kwanini mnayaficha? Mimi ntaandika mazuri na mnayo yaficha humu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi home ni Marangu, unaongelea Marangu ipi mzee? Marangu mtoni? Mbona kuchafu ase au sijaelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha mzaha wewe,sasa kama kwako ni Marangu unachobisha watu si wasafi ni nini?
Kwa sababu ukiangalia kwenye barabara za kuelekea majumbani kwa watu(baadhi),kwa njiani wameweka vijidude vya kuwekea taka.maeneo ya Marangu hotel,Marangu hills mpk Marangu stendi unayoijua wewe.Hamna Uchafu

Alafu pili unajua nini maana ya uchafu???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wadanganye ambao hawajawahi kufika ama kukaa moshi.
Hufai kuigwa kabisa kwenye jamii yetu ya kitanzania

[emoji375][emoji375]
 
Peleka uongo kule wewe, ukiona kuna hayo madude ya uchafu Marangu ujue kuna project wazungu wanafanya kwenye eneo hilo au wameweka tu baada ya kutalii kwenye shule na mfano zile dust bin za Kilimanjaro resort zimewekwa na mmiliki wa hiyo hotel kuzunguka hotel yake wala si watu binafsi. Karibu
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Basi kwa muktadha huu.Naomba niwe kimya tusibishane sana
Siku njema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Marangu Hotel ni mahali wazungu wanalala baada ya kufanya utalii wa mlima Kilimanjaro, kuna muda Hotel inakua responsible kuhakikisha usafi wa maeneo ili watu weupe wasiwe discouraged na mazingira ya huduma. Ila wazawa ni wana usafi tu kama wakazi wa dar, Moro, Kigoma. Hakuna tofauti kabisa
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah...Moshi..home sweet home...hata Tigo walifika mapema sana....[emoji41]

Sent using Beretta ARX 160
 
Sasa ngoja waje wale kina Waitu mauweee, inshomireee na igambire uone mapovu ya senene. BTW hivi watu wanajitambulishaje kwa kula wadudu.?
 
Tribalism hii mkuu.. hata hivyo wachaga hawana ukabila kama unavyotaka kuaminisha watu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…