Kilimanjaro: Samia Legal Aid Campaign yatatua mgogoro wa ardhi uliodumu miaka zaidi ya 30

Kilimanjaro: Samia Legal Aid Campaign yatatua mgogoro wa ardhi uliodumu miaka zaidi ya 30

Mindyou

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2024
Posts
1,869
Reaction score
4,877
Timu ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) imefanikiwa kutatua mgogoro wa ardhi uliodumu miaka zaidi ya 30 na hatimaye kufikia tamati.

Hayo yalijiri Februari 8,2025 baada ya timu hiyo kumkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu, taarifa ya utendaji kazi ya Huduma ya Msaada wa Kisheria bure kupitia “Mama Samia Legal Aid Campaign”.

Akizungumza na Waandishi wa Habari nje ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Wakili wa Kujitegemea kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Dk. Belinda Chepchumba, alisema kupitia kampeni hiyo waliweza kutatua migogoro miwili ya ardhi Kata ya Mabogini Wilaya ya Moshi Vijijini ambayo imedumu kwa miaka mingi.

“Kupitia kampeni hii ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) tuliweza kufika Kata ya Mabogini iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Moshi Vijijini na tumeweza kutatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa miaka zaidi ya 30, lakini pia tumetatua mgogoro mwingine wa ardhi uliodumu kwa miaka minne.”alisema Dk. Chepchumba.

Aidha Dk. Chepchumba ambaye pia ni Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Shule ya Sheria, alisema kupitia kampeni hiyo waliweza kuzifikia Kata 10 na Vijiji 30 zilizoko Halmashauri hiyo na kufanikiwa kutatua migogoro 105.

“Migogoro ambayo ilijitokeza kwa wingi ni migogoro ya ardhi, ukatili wa kjinsia pamoja na masuala ya ndoa, ipo migogoro ambayo tuliweza kuitatua lakini pia kuna migogoro ambayo hatukuweza kuitatua hivyo itaendelea kutatuliwa na Wanasheria wetu wa TLS kwa kusikilizwa na kuhudumiwa bure kabisa.”alisema.

Snapinst.app_472610063_18487215877057742_7812393324770692030_n_1080.jpg


Source: Millard Ayo
 
Timu ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) imefanikiwa kutatua mgogoro wa ardhi uliodumu miaka zaidi ya 30 na hatimaye kufikia tamati.

Hayo yalijiri Februari 8,2025 baada ya timu hiyo kumkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu, taarifa ya utendaji kazi ya Huduma ya Msaada wa Kisheria bure kupitia “Mama Samia Legal Aid Campaign”.

Akizungumza na Waandishi wa Habari nje ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Wakili wa Kujitegemea kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Dk. Belinda Chepchumba, alisema kupitia kampeni hiyo waliweza kutatua migogoro miwili ya ardhi Kata ya Mabogini Wilaya ya Moshi Vijijini ambayo imedumu kwa miaka mingi.

“Kupitia kampeni hii ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) tuliweza kufika Kata ya Mabogini iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Moshi Vijijini na tumeweza kutatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa miaka zaidi ya 30, lakini pia tumetatua mgogoro mwingine wa ardhi uliodumu kwa miaka minne.”alisema Dk. Chepchumba.

Aidha Dk. Chepchumba ambaye pia ni Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Shule ya Sheria, alisema kupitia kampeni hiyo waliweza kuzifikia Kata 10 na Vijiji 30 zilizoko Halmashauri hiyo na kufanikiwa kutatua migogoro 105.

“Migogoro ambayo ilijitokeza kwa wingi ni migogoro ya ardhi, ukatili wa kjinsia pamoja na masuala ya ndoa, ipo migogoro ambayo tuliweza kuitatua lakini pia kuna migogoro ambayo hatukuweza kuitatua hivyo itaendelea kutatuliwa na Wanasheria wetu wa TLS kwa kusikilizwa na kuhudumiwa bure kabisa.”alisema.



Source: Millard Ayo
as long as siyo uamuzi wa mahakama kesho ambaye rohoni hajaridhika ataenda mahakamani baada ya samia kuondoka
 
Timu ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) imefanikiwa kutatua mgogoro wa ardhi uliodumu miaka zaidi ya 30 na hatimaye kufikia tamati.

Hayo yalijiri Februari 8,2025 baada ya timu hiyo kumkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu, taarifa ya utendaji kazi ya Huduma ya Msaada wa Kisheria bure kupitia “Mama Samia Legal Aid Campaign”.

Akizungumza na Waandishi wa Habari nje ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Wakili wa Kujitegemea kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Dk. Belinda Chepchumba, alisema kupitia kampeni hiyo waliweza kutatua migogoro miwili ya ardhi Kata ya Mabogini Wilaya ya Moshi Vijijini ambayo imedumu kwa miaka mingi.

“Kupitia kampeni hii ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) tuliweza kufika Kata ya Mabogini iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Moshi Vijijini na tumeweza kutatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa miaka zaidi ya 30, lakini pia tumetatua mgogoro mwingine wa ardhi uliodumu kwa miaka minne.”alisema Dk. Chepchumba.

Aidha Dk. Chepchumba ambaye pia ni Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Shule ya Sheria, alisema kupitia kampeni hiyo waliweza kuzifikia Kata 10 na Vijiji 30 zilizoko Halmashauri hiyo na kufanikiwa kutatua migogoro 105.

“Migogoro ambayo ilijitokeza kwa wingi ni migogoro ya ardhi, ukatili wa kjinsia pamoja na masuala ya ndoa, ipo migogoro ambayo tuliweza kuitatua lakini pia kuna migogoro ambayo hatukuweza kuitatua hivyo itaendelea kutatuliwa na Wanasheria wetu wa TLS kwa kusikilizwa na kuhudumiwa bure kabisa.”alisema.



Source: Millard Ayo
Inakuwaje Rais aunde campaign nje Mfumo wa kawaida uliopo

Kwanini asimamie Mfumo uliopo utende haki kwa haraka au uunde kitengo kitakachojulikana kisheria kusaidia wananchi maskini kuliko kampeni
 
Hii ni mwendeleo ule ule wa kuonyesha mifumo rasmi ya kutoa huduma (Mahakama, Hospitali, Shule, Polisi) imekufa kabisa.
Yaani kwa miaka yote 30 ambayo huo mgogoro umekuwepo, mahakama zilikuwepo na zikashindwa kumaliza mpaka hiyo kampeni yq wiki chache ilipokuja!
 
..kwa miaka yote ambayo mgogoro umedumu CCM imekuwepo mahakamani.

..kama Samia Legal Aid ndio muarubaini basi tuufute mfumo wote wa mahakama nchini.
 
Nyie mnaijua migogoro ya ardhi vizuri?? Mmeandika settlement deed? Au ndio oya oya za mikutano ya hadhara?Sasa hivi mtakuta summons zinaandikwa
 
Hii ni mwendeleo ule ule wa kuonyesha mifumo rasmi ya kutoa huduma (Mahakama, Hospitali, Shule, Polisi) imekufa kabisa.
Yaani kwa miaka yote 30 ambayo huo mgogoro umekuwepo, mahakama zilikuwepo na zikashindwa kumaliza mpaka hiyo kampeni yq wiki chache ilipokuja!

..kama ni hivyo tuondoe mahakama zote tubaki na Samia Legal Aid.🤣
 
Mamlaka zilizopaswa kutatua hilo tatizo ziko wapi? yaani Samia legal Aid Campaign inatatua tatizo la ardhi halafu lililoshindwa kutatuliwa na Taasisi zinazoongozwa na huyohuyo Samia.

Dah aisee, kweli Kuna uyaone.
 
Back
Top Bottom