Ndugu zangu awali nilileta uzi uliokuwa unasema Kilimo ni biashara pekee inayolipa 100%, wapo waliopinga na wapo walikubaliana nami, lengo la uzi nilikuwa nimewalenga hasa vijana waliomaliza vyuo vikuu wanaozunguka na bahasha huku wakikidharau kilimo ambacho kinaweza kuwatoa na kupata mitaji. Wapo watu walihoji kwamba kama kilimo kinalipa mbona wazee wamejihusisha na kilimo kwa muda mrefu ni maskini? Wao wana hoja ya msingi ila wakumbuke watu wengi wanafanya kilimo cha kienyeji sana, hawatumii mbolea, hawapandi kwa vipimo matokeo yake huvuna mazao duni, lakini ukilima kisasa utakifurahia kilimo.
Awamu ya pili nimelima ila nikaongeza ukubwa wa shamba kidogo toka ekari mbili mpaka tatu, nilitumia takribani laki tisa kuandaa mashamba hayo mpaka kuvuna, kwa mchanganuo ufuatao.
Mbolea mifuko 4@61,000/=
Mbegu mifuko 16@10000/=
Kulima nilitumia ng'ombe zangu, ingawaje kama nisingetumia ng'ombe hizo gharama yake ingelikuwa 200,000/=
Kupanda mashamba yote 75,000/=
Palizi awamu ya kwanza na ya pili jumla 210,000/= awamu ya kwanza 105,000/= @ekari 35,000/=
Mpaka sasa nimevuna ekari 2 nilizivuna mwishoni mwa mwezi wa tano, nilitumia Tsh50,000/=
Mifuko 40@10000=40,000/=
Kupukuchua 1@2000 nilivuna gunia 38@2000=76,000/=
Huo ndio mchanganuo ninaoukumbuka katika awamu ya pili ya mahindi niliyolima.
Katika ekari mbili nilizo vuna nimepata gunia 38, ambazo niliziuza 3,465,000/=
Hivyo mtaji wangu wa kilimo misimu miwili una jumla ya milioni tano.
Katika kukuza mtaji nimechukua milioni mbili iliyobaki mwaka jana baada ya kutoa gharama za kilimo awamu ya pili nimeongeza za sasa hivi nimeanza kununua mahindi maana bei kwa sasa imeshuka gunia la mahindi linauzwa Tsh 50,000/=ila nina uhakika kwa hali ya chakula iliyopo nchini kufikia mwezi wa tisa gunia litakuwa linauzwa laki,maana nimetembelea mikoa ya Geita, Tabora, Mwanza, baadhi ya maeneo mkoa wa Mara na simiyu, katika mikoa hiyo hali ya chakula ni tete.
Ekari ya tatu ambayo sijavuna nategemea kupata gunia 17~20 haya nitayachanganya na ambayo nanunua sasa hivi ili niyauze bei ikipanda.
Faida nyingine niliyoiona kwenye kilimo ni kwamba ni biashara pekee ambayo usimamizi wake ni mdogo mimi nipo Mwanza lakini nafanya kilimo Tarime na mambo yanasonga tu, katika mashamba yote nilienda kuvuna tu wakati mwingine wote nilikuwa natuma pesa..
Nawaasa vijana wenzangu ambao hamjapata ajira msikae kuzunguka na bahasha tuu, geukieni kilimo kinalipa, sisemi kwamba muwe wakulima, hapana, ila kilimo ni njia nzuri ya kupata mtaji kwa haraka kama nilivyo fanya mimi.
Rejea,
Kilimo ni biashara pekee inayolipa kwa 100%
Awamu ya pili nimelima ila nikaongeza ukubwa wa shamba kidogo toka ekari mbili mpaka tatu, nilitumia takribani laki tisa kuandaa mashamba hayo mpaka kuvuna, kwa mchanganuo ufuatao.
Mbolea mifuko 4@61,000/=
Mbegu mifuko 16@10000/=
Kulima nilitumia ng'ombe zangu, ingawaje kama nisingetumia ng'ombe hizo gharama yake ingelikuwa 200,000/=
Kupanda mashamba yote 75,000/=
Palizi awamu ya kwanza na ya pili jumla 210,000/= awamu ya kwanza 105,000/= @ekari 35,000/=
Mpaka sasa nimevuna ekari 2 nilizivuna mwishoni mwa mwezi wa tano, nilitumia Tsh50,000/=
Mifuko 40@10000=40,000/=
Kupukuchua 1@2000 nilivuna gunia 38@2000=76,000/=
Huo ndio mchanganuo ninaoukumbuka katika awamu ya pili ya mahindi niliyolima.
Katika ekari mbili nilizo vuna nimepata gunia 38, ambazo niliziuza 3,465,000/=
Hivyo mtaji wangu wa kilimo misimu miwili una jumla ya milioni tano.
Katika kukuza mtaji nimechukua milioni mbili iliyobaki mwaka jana baada ya kutoa gharama za kilimo awamu ya pili nimeongeza za sasa hivi nimeanza kununua mahindi maana bei kwa sasa imeshuka gunia la mahindi linauzwa Tsh 50,000/=ila nina uhakika kwa hali ya chakula iliyopo nchini kufikia mwezi wa tisa gunia litakuwa linauzwa laki,maana nimetembelea mikoa ya Geita, Tabora, Mwanza, baadhi ya maeneo mkoa wa Mara na simiyu, katika mikoa hiyo hali ya chakula ni tete.
Ekari ya tatu ambayo sijavuna nategemea kupata gunia 17~20 haya nitayachanganya na ambayo nanunua sasa hivi ili niyauze bei ikipanda.
Faida nyingine niliyoiona kwenye kilimo ni kwamba ni biashara pekee ambayo usimamizi wake ni mdogo mimi nipo Mwanza lakini nafanya kilimo Tarime na mambo yanasonga tu, katika mashamba yote nilienda kuvuna tu wakati mwingine wote nilikuwa natuma pesa..
Nawaasa vijana wenzangu ambao hamjapata ajira msikae kuzunguka na bahasha tuu, geukieni kilimo kinalipa, sisemi kwamba muwe wakulima, hapana, ila kilimo ni njia nzuri ya kupata mtaji kwa haraka kama nilivyo fanya mimi.
Rejea,
Kilimo ni biashara pekee inayolipa kwa 100%