Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko

Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko

GHARAMA KUBWA IKO KWENYE MBEGU, GRAM 250 ZA KUTOSHA EKA 1 ITAKUGHARIMU KATI YA 1110,000-140,000, GHARAMA NYINGINE NI YA MAJI (KAMA UTATUMIA PUMP, SO GHARAMA YA MAFUTA) KUTEGEMEA NA PUMP UTAKAYOKUWA NAYO UNAWEZA JIKUTA KWA SIKU UNATUMIA MPAKA LITA 7-10, SASA ZDISHA KWA BEI YA FUEL YA SASA MARA SIKU 70 ZA KUKAA SHAMBANI, SAMBAMBA NA HILO JE PUMP YA KUMWAGILIA NI YAKO.. KAMA NI YA KUNUNUA SI CHINI YA LAKI3 PUMP NZURI, YA KUKODI KWA MUDA WA MIEZI 3 HIYO SI CHINI YA LAKI 2. KUTEGEMEA NA MSIMU ULIOLIMA (JE NI WA JUA AU MVUA??) KAMA NI WA MVUA GHARAMA NYINGINE ITAKUWA KATIKA MADAWA YA UKUNGU NA WADUDU. KWA UCHACHE KABISA GHARAMA YA EKA 1 YA TIKITI MPAKA UNAVUNA ITAKUGALIMU SI CHINI YA MILIONI 2, GHARAMA NYINGINE NI MBOLEA UTAHITAJI MIFUKO MIWILI YA DAP=180,000, UTAHITAJI UREA MIFUKO MIWILI 140,000TSH, UTAHITAJI NA CAN YA KUMALIZIA MIFUKO 3 TSH 210,000 ETC...... KILIMO NI GHARAMA HIVYO NI VYEMA KUJIPANGA VIZURI, ANDAA 2.5 MILIONI NDIO UINGIE SHAMBA.
Asante kilimomaarifa.tajiri nimekuelewa vya kutosha hapo juu ya hilo swala na je faida yake inakuwaje? Pia soko lake linapanda na kuahuka ama liko constant?
 
KWA UTAMU- MUDA WA KUKOMAA UKUBWA (KG) Kampuni

1.SUKARI F1-Mistari ya Punda milia siku 80-90 7-14 kg -East African Seed
2. -Julina F1-Mistari ya punda milia siku 85-90 8-12kg -Kibo seed
3.-Mshindi F1-Mistari ya punda milia Siku 75-80 5-9 kg -East West seed
4. -Daytona F1-Mistari ya Punda milia siku 75-80 10-12 kg -Kibo seed
5. -Jubilee/Tiger stripe siku75-85 5-12kg -East African Seed
6..-Creemson sweet Ni la kijani tu siku 80-85 5-10 kg -Kibo seed

MAGONJWA
1.-Juliana is the best huhimii magonjwa mengi ya ukungu na wadudu
2.-Daytona F1-Huhimili sana magonjwa ya ukungu shambani
3.-Creemson Sweet-Hustahimili magonjwa ya Ubwiri Unga/Ubwiri Poda/Powdery Mildew
-



Ningefurahi sana pia kama tungepata majibu ya hili swali, pia kujua kati ya mbegu zote zilizotajwa ni ipi bora zaidi kwa utamu na ukubwa, ipi isiyoshambuliwa sana na magonjwa, ipi ya muda mfupi zaidi n.k Cc: Asprin Malila riltz Mama Joe na wengine
 
Enorme
ILI KUPATA FAIDA KUBWA itategemea kwanza 1.unamzigo bora na 2. mwingi kiasi gani, lakini pia na demand na upply imekaaje kwa wakati huo??, maana kama demand ni kubwa na supply ni kidogo means mahitaji yatakuwa makubwa, hivyo bei juuu... sasa kama bei iko juuu, na unamzigo mkubwa na bora basi wewe ni tajiri.

Sasa bila kufichana soko la tikiti huwa linacompete sana na Matunda mengine kama maembe na mananasi, HIVYO UKITAKA KUWIN BEI NZURI YA TIKITI FANYA USHUSHUSHU JUU YA MAEMBE NA MANANASI NI WAKATI GANI YANAKUWA HAYAPO SOKONI THEN WEWE NDIO WAKATI HUO UWE UNAVUNA MATIKITI YAKO, OTHERWISE, UTAKUTANA NA BEI NDOGO... KWA SABABU MATUMIZI MAKUBWA YA TIKITI NI KATIKA JUICE ETC, SO MTU ATAWAZA EMBE 1 LABDA NI TSH 500, NANASI MOJA NI TSH 500-1000 LAKINI TIKITI LABDA NI TSH 3000, SO MTU ANAPIGA HESABU HAPO.... BILASHAKA MWEZI WA 7 HADI WA 11 NI MZURI KWA TIKITI. MAANA UKUMBUKE PIA TIKITI HALIHITAJI MAJI MENGI LINAPOKUWA LIMEKOMAAA, NI KAMA KITUNGUU...KAMA UTAVUNA TIKITI LIKAKUTANA NA MVUA UWEZEKANO WA KUHARIBIKA NI MKUBWA SANAAA (UZOEFU HUO NINAO) ... .. CHUKUA TAHADHARI SANA UNAPOKARIBIA KUVUNA TIKITI NA VITUNGUU.....
Asante kilimomaarifa.tajiri nimekuelewa vya kutosha hapo juu ya hilo swala na je faida yake inakuwaje? Pia soko lake linapanda na kuahuka ama liko constant?
 
Nauliza, Hivi hakuna kiwanda kinanunua haya matikiti maji kwa bei ya jumla na je kama kipo, ni shilingi ngapi kwa kuilo?
 
Ni hakika elimu pana sana inatolewa ktk uzi huu.

Ningependa kufahamu mtu ambaye anafanya kilimo cha Matikiti ktk mkoa wa Tanga.


Natanguliza shukran.
🙂
 
Mkuu,

Kwa wastan unaweza pata mashimo 1,200 kwa ekari moja.

Kila shimo moja unaweza panda miche mi 3. Hivyo, kwa shamba moja unaweza kuwa na miche 3,600

Mkuu nimekuelewa kwa uzuri. Labda ningependa fahamu kwa mche mmoja approximately inaweza zaa matunda/matikiti mangapi??

Natanguliza shukran kwako.
 
mimi n
Shukran for the notable hint!

Cha msingi ni business plan!
ilijaribu hii kitu tena kwa kutumia mbegu ya hybrid sugar 1 kwa heka moja, shamba lilipendeza sana. unfortunately muda wa mavuno ulipokaribia nikapatwa na msiba mzito.

Kuja kuzinduka mmmh tatu bila!
 
mimi n

ilijaribu hii kitu tena kwa kutumia mbegu ya hybrid sugar 1 kwa heka moja. shamba lilipendeza sana. unfortunately muda wa mavuno ulipokaribia nikapatwa na msiba mzito. kuja kuzinduka mmmh tatu bila!
Pole mkuu ni challenge tu hizo. Ila kwa ushauri niliosoma juu huko ni kuwa mbegu ya hybrid huwa haina matokeo mazur au una maana ni ile ya kununua ktk maduka ya pembejeo?
 
Pole mkuu ni challenge tu hizo. Ila kwa ushauri niliosoma juu huko ni kuwa mbegu ya hybrid huwa haina matokeo mazur au una maana ni ile ya kununua ktk maduka ya pembejeo?
Hii ni mbegu inayovuma sasa. inatolewa na East african Seed company ya kenya, wanaofisi zao Arusha. inauzwa ghali sana. 1kg ilikuwa sh 150, 000. kwaenye maduka mengi ya kilimo haipo as bei ni kubwa sana.
 
Hii ni mbegu inayovuma sasa. inatolewa na East african Seed company ya kenya, wanaofisi zao Arusha. inauzwa ghali sana. 1kg ilikuwa sh 150, 000. kwaenye maduka mengi ya kilimo haipo as bei ni kubwa sana.
Okay nimekupata mkuu...sasa tatizo ilikuwa nini ikapelekea kutopata mavuno yaliyo bora? Magonjwa, uhaba wa maji au upandaji wa mbegu? [emoji134]
 
Okay nimekupata mkuu...sasa tatizo ilikuwa nini ikapelekea kutopata mavuno yaliyo bora? Magonjwa, uhaba wa maji au upandaji wa mbegu? [emoji134]
tatizo niilichelewa kuvuna yakaanza kuharibika.
 
Back
Top Bottom