Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko

Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko

Mimi nina kisima cha pump ya umeme ninataka kutumia mpira hoose pipe. Kumwagilia heka moja nitakuwa sawa?
 
ameeleza vizuri HESABU KALI nadhani nami ningekueleza hivyo, na muhimu hapo ni maji tu iwe mashine,pump au ndoo kwa hivyo ni sawa tu kwa hicho kisima
 
Kwanza hongera kwa kuamua kuingia shambani, mimi nalima matikiti na nimeshajilipua kulima ktk kipindi hiki cha masika, kubwa zaidi tafuta mbegu bora kwenye maduka ya kilimo mfano pitia kariakoo, mimi nalima Hybrid F1 sugar queen, na kiwango cha ekari moja utatakiwa kuwa na gram 300 na kila shimo panda mbegu 2 japo wapo wanaopanda mpaka 3, na hapa utatakiwa kuwa na mshimo kama 2000.
Andaa shamba vizuri japo wiki tatu kabla ya kupanda na hakikisha eneo lako lina maji ya kutosha kwani tikiti linahitaji maji mengi katika uhai wake, Panda kwa mbolea, ni vema zaidi kama utapata samadi na kama utatumia ya viwandani zipo kama vile winner(hapa kuna kiambato chake, utamuuliza muuzaji), kwa kukuzia utatumia CAN, andaa dawa za wadudu wanaokata majani pindi matikiti yanapoanza kuota tu na pindi unapoona dalili za matikiti kushambuliwa majani (karate itakufaa).
Unahitaji uangalizi wa karibu sana kuanzia mwanzo mpaka mwisho na hakikisha unakuwa na dawa za kutosha kwa ajili ya kuzuia wadudu waharibifu, ukungu hasa kipindi hiki na magonjwa yanayoshambulia majani, maua na matunda.
Gharama kubwa utakayoingia kwenye kilimo hiki ni kwenye mbegu( ekari moja ni gram 300= 250,000 kwa Dar), dawa( hapa inategemea na hali ya eneo na jinsi magonjwa na wadudu wanavyoshambulia), nguvu zako mwenyewe kwenye kumwagilia( hapa kama unatumia ndoo, ila kama unatumia mashine ya kuvutia maji basi utahitaji wastani wa lita 5 kwa ekari moja kila unapomwagilia) na kutunza shamba, kama unatumia kijana basi hapo ni makubaliano yenu, bomba la kupigia dawa ni muhimu sana.
Mavuno ni kuanzia siku 65 mpaka 75 inategemea na eneo lenyewe na aina ya mbegu, na kiasi cha mavuno kwa ekari moja ni kiasi cha matikiti kama 7000( kila mche mmoja utoe matikiti 2 tu yenye afya nzuri) na soko likiwa nuri basi utauza kwa wastani wa Tsh 1500 au zaidi shambani, na ukiMU kwenda mwenyewe sokoni mfano Buguruni unaweza kuuza bei nzuri kama ni kipindi mmea huo haupatikani.
Ushauri: usiende shambani na matarajio makubwa zaidi ya kupata hela nyingi ukasahau changamoto zake( mavuno kidogo, hasara na muda), shambani kunahitaji uangalizi wa karibu sana na usijaribu kulima kwa simu hasa kama una watu wasio waaminifu watakuua kwa ugonjwa wa moyo. Pia hizo faida zinazopatiakana ni pale tu utakapo fata ushauri wa kitaalamu na ukaamua kwa dhati kufanya kilimo. Nimejaribu kueleza kile ninachofahamu japo sio kwa utaalamu zaid, mengine wajuzi watakuja kujazia.
Karibu sana shambani
Asante kwa ushauri mkuu....umenifungua macho
 
Ok nashukuru.

Pia nahitaji maelezo ya kina kwenye upandaji maana Mimi tayari nimeshanunua mbegu aina ya Juliana (Hybrid), mbolea DAP, Yaramila, Easygrower, Farmguard, Booster, Poly-Feed Starter na Bomba la kunyunyizia dawa.

Sasa nahitaji kujua jinsi ya kupanda spacing, uchimbaji vishimo na kuchanganya mbolea na kadhalika.
 
Me nngependa kujua ekari moja unaweza kutumia sh ngap kuanzia mwanzo yaan uandaaji wa shamba had mavuno,am interested ktk hk kilimo, najipanga
 
Naomba msaada kuhusu kilimo cha Matikiti Maji (Watermelon) kwa kuzingatia maeneo yafuatayo:-

- Mbegu
- Upatikanaji wa mbegu
- Upandaji
- Aina ya mbolea
- Madawa
- Magonjwa
- Uvunaji
- Uuzaji
- Faida ya kilimo cha Matikiti

Nadhani hiyo itasaidia zaidi!
 
Naomba mada hii kuhusu kilimo cha Matikiti Maji (Watermelon) ijibiwe kwa mtiririko huu:-
- Mbegu
- Upatikanaji wa mbegu
- Upandaji
- Aina ya mbolea
- Madawa
- Magonjwa
- Uvunaji
- Uuzaji
- Faida ya kilimo cha Matikiti
Nadhani hiyo itasaidia zaidi!
 
nimeshauza mkuu ila nilipata hasara.
ndugu kilimo kinaitaji timing na kufuata taratibu zake zote, pia kua makini na madalali hawa wanaletaga presha zisizo na msingi, hawajui ugumu wa kazi ulivyo na gharama zake wao wanachojua ni kupiga faida tu kuijanjaujanja.

Usife moyo Mungu atakupigania, hayo ndio majaribu, jipange upya nenda kwa step utatoka, Mungu akutangulie
 
Hivi haya ya kisasa yana nini zaidi? Maana naona kama wakulima wanaachana na matikiti ya asili
 
kuna maji huko hakufai jumanne ya 26 April nimeenda kuna mabonde ya maji na barabara imekuwa kama mt o
 
Ndo maana watanzania hatuendelei,kila kitu peaa kweli hata kwa masuala ya kiuchu namna hii kuungwa mnataka pesa ,nani kawaloga ?
 
Back
Top Bottom