Kilimo cha Mitiki: Utaalamu na biashara yenyewe

Kilimo cha Mitiki: Utaalamu na biashara yenyewe

Wadau naomba kupata ukweli juu ya hii miti ya mitiki,kuna mengi yanasemwa juu ya miti hii,kifupi mimi naomba kujua,je ni 1: kweli kua miti hii ni ghali sana kidunia? 2: ni kweli kua zipo baadhi ya banks hapa nchini zinatoa mikopo ukiwa na miti hii?kama ni kweli je ni bank gani hizo? 3:je mitiki uwa inachukua muda gani kuanza kukua mpaka kufikia hatua ya kuingizwa sokoni?kuna mtu aligusia kua kuna aina tofauti tofauti za miteak na ukuaji wake,ila nae hana uhakika sana juu ya ilo

Wakuu, mimi mwenyewe nasubiri majibu ya kiundani zaidi kuhusu hiki kilimo cha mitiki.
Nataka nianze mchakato 2014, ili by 2035 nikiwa NIMESHAKUFA (au nikiwa bado niko hai at 60's) mwanangu aliye na miaka 3 sasa atakuwa ana 25 yrs (akiwa Chuo Kikuu akisomea masuala ya Public Administration, Bussiness Administration na/ au mambo mengine yanayofanana na hayo) ili akimaliza Chuo kikuu atumie hizo billioni kadhaa zitakazo kuwa zimetokana na mitiki kusimamia kazi zake kwa kuhakikisha anaajiri wataalamu watakaoendesha miradi yake kwa ufanisi.

.....Maige alisema wakati mahitaji ya mbao nchini kwa mwaka yanafikia meta za mraba milioni tano, uwezo wa mashamba yaliyopo ni kuzalisha meta za mraba milioni 1.5 tu. Alisema Sh milioni 40 zinatosha kuhudumia ekari moja ya shamba la mitiki kwa miaka 20, lakini mazao yake yakazalisha zaidi ya Sh bilioni 3. .......
Reference (March 2012): MOROGORO FAMILY - MOROGORO YETU: TANAPA 'YALIWA' KWENYE MAGOGO YA MITIKI.
 
Ni kweli mitiki ni miti yenye thamani sana. kitaalam inaitwa "tectona grandis". thamani yake inakuja kutokana na matumizi yake. unaweza kuitumia kwa matumizi yoyote kama mbao nyingine lakini matumizi yanayoipa thamani miti hii ni kutengenezea sakafu na vifaa vya muziki kama piano na magita. Miti hii inakuwa na thamani kubwa ikifikisha angalau miaka 50. Najua sisi waafrika huwa tunapenda miradi inayolipa chapchap kwa sababu sisi ni wabinafsi hatufikirii vizazi vyetu, najua kwa kukupa taarifahizi umeshakata tamaa.chini ya umri nilioutaja thamani yake ni ndogo sana kwa sababu haijajaza uzito (density) na upana unaotakiwa.Sina uhakika na benki inayokopesha kwa kutumia miti lakini nafikiri benki wanaangalia ukubwa wa eneo, eneo lililopo (location), na hati miliki. PANDA MITIKI LEO KWA FAIDA YA VIZAZI VYAKO ACHA UBINAFSI. google kwenye mtandao jina hilo la kisayansi utapata taarifa nyingi sana za mti huo.
 
Mimi nimesnza kupanda hii miti.ukienda wakala wa mbegu za misitu morogoro utapata taarifa nyingi.ila inaanza kuvu nwa baada ya miaka kumi
 
Fifty years ! Hiyo ni hazina ya mjukuu wa mtoto wako ! endeleza kizazi chako watengenezee urithi uliotukuka.
 
Kuvuna ni maiak 20?

Sasa hapo jamani si nitakuwa nishazeeka kama nitakoswa koswa na magonjwa, polution, ajali , nk:biggrin:
 
Je unapotaka kupanda mitiki je mbegu zinauzwa wapi?
· Mbegu zinauzwa National tree seed cenre _morogoro
· Pia unaweza kufanya local seed collection katika mashamba ya miti ya serikali(mtibwa, longuza Tanga, Rondo lindi) – hapa bei ni very cheap
·Mbegu zinasiwa baada ya kubabuliwa kidogo kwa moto( juu weka nyasi kiasi halafu choma, kama unyebabua samaki)
· Mbegu unaweza kuzipandikiza kwenye viriba
· Au unaweza ukaziacha mbegu ziendelee kukua kwenye matuta, kasha kabla ya kupandikiza shambani unangoa ile miche na kuikata kichwa na kuchonga mizizi yote(ili mche ubaki kama stump) baada ya hapo unapandikiza kile kijiti shambani kwako kwa kufuata vipimo vya 2.5Mx 2.5M

· Ha moja inapandwa miche 1600
· Nguzo zinaanza kuvunwa baada ya miaka 10 ya kwanza
· Mbao ni miaka 40
· Bei ya miti hiyo unauza kwa zaidi ya 160,000 kwa cubic meter moja, na mti mmoja unaweza kukupa cubic metre 3



Nawasilisha
 
Heshima kwenu wakuu.
dar ninashamba la hekari nne nahitaji kupanda miti ya MITIKI ila nikipiga hesabu ya kununua miche naona sitoweza kutokana na uchumi wangu.
Naomba mnishauri ni wapi nitapata mbegu za mitiki ili nianzishe bustani
_Natanguliza shukrani za dhati.
 
Je unapotaka kupanda mitiki je mbegu zinauzwa wapi?
· Mbegu zinauzwa National tree seed cenre _morogoro
· Pia unaweza kufanya local seed collection katika mashamba ya miti ya serikali(mtibwa, longuza Tanga, Rondo lindi) – hapa bei ni very cheap
·Mbegu zinasiwa baada ya kubabuliwa kidogo kwa moto( juu weka nyasi kiasi halafu choma, kama unyebabua samaki)
· Mbegu unaweza kuzipandikiza kwenye viriba
· Au unaweza ukaziacha mbegu ziendelee kukua kwenye matuta, kasha kabla ya kupandikiza shambani unangoa ile miche na kuikata kichwa na kuchonga mizizi yote(ili mche ubaki kama stump) baada ya hapo unapandikiza kile kijiti shambani kwako kwa kufuata vipimo vya 2.5Mx 2.5M

· Ha moja inapandwa miche 1600
· Nguzo zinaanza kuvunwa baada ya miaka 10 ya kwanza
· Mbao ni miaka 40
· Bei ya miti hiyo unauza kwa zaidi ya 160,000 kwa cubic meter moja, na mti mmoja unaweza kukupa cubic metre 3



Nawasilisha

asante sana mods
asante sana mkuu. Sendoro Mbazi kama unaweza naomba namba za simu za huko morogoro nikanunue hizo mbegu
 
Last edited by a moderator:
Habarini wanajf, kwa muda mrefu nimekuwa nikisikia zao la miti aina ya Mitiki kuwa ni ya thamani sana. Ukweli ni kwamba muda wote sijapata maelezo ya kitaalamu kuwa;
(a) Inalimwa wapi na inakomaa kwa muda gani
(b) Inastawi uoto gani
(c)Faida na masoko yake.

Naombeni msaada wa kitaalam ili niweze kuufanyia kazi@ Kilimo kwanza.
 
Jamani habari zenu!

Naomba msaada wenu wa maelezo ya kitaalamu kuhusu hii miti ya mitiki, sifa zake, aina, upatikanaji wa mbegu zake - wapi na gharama! Hali ya hewa stahiki, umri mpaka kuwa tayari kuvunwa.

Shukrani sana.
 
Jamani habari zenu!

Naomba msaada wenu wa maelezo ya kitaalamu kuhusu hii miti ya mitiki, sifa zake, aina, upatikanaji wa mbegu zake - wapi na gharama! Hali ya hewa stahiki, umri mpaka kuwa tayari kuvunwa.

Shukrani sana.

Mkuu, wakati unasubiri majibu kwenye uzi wako, jaribu kutafuta (search) hapa hapa jamvini Uzi uliowahi kuzungumzia Mitiki. Nadhani ni Wiki iliyopita tu kulikuwa na mazungumzo kuhusu Mitiki. Kuna kama Uzi mbili-tatu hivi hapa hapa zenye maelezo ya kutosha kuhusu hili. Unaweza vilevile kutembela Blogu ya Mitiki (mitiki.blogspot)
 
Tanzania Tree Seed Agency watashiriki maonyesho ya sabasaba mwaka huu na watapatikana kwenye banda la Maliasili na utalii watakuja na aina mbali mbali za mbegu za miti kwa kuuza. Ni kipindi kizuri basi kuwaona na kupata taarifa za kina kuhusu aina mbalimbali za miti, zinastawi wapi, bei zake na masoko.

Wataalamu wa kilimo wa chuo kikuu cha SUA, Morogoro nao watashiriki, wanakuwa na taarifa nyingi nzuri kupita maelezo kuhusu kilimo, ufugaji, uvuvi, masoko n.k. Kwa wale walioko Dar na mikoa ya jirani na umedhamiria kulima, hakikisha unakutana na hao wataalamu wetu.

Nashukuru mama porojo, umenifungua macho hapa
 
Wadau nna km ekari 2 maeneo ya vigwaza huko zina km miaka 2 hazilimwi chochote sasa nataka kulima hii miti ya mitiki ambayo hutumika kwa nguzo za umeme ila sijajua process za ulimaji wake zikoje

Kwa mwenye ujuzi wa ulimaji wake pamoja na upatikanaji wa mbegu tafadhali anisaidie wadau

Natanguliza shukrani
 
Kabla ya yote ingefaa usearch nyuzi zote zinazohusiana na kilimo cha mitiki upandaji,matunzo,uthamani wake na soko lake limekaaje. Vyote hivyo vimo humu na vishaongelewa sana ndugu!
Kisha mimi ntakusaidia kupata mbegu zake iwe kwa punje(uoteshe kitaru chako mwenyewe) ama mche(upande moja kwa moja miche iliyokwisha andaliwa)
Kwa kukuondoa tongotongo tu ni kwamba wazo ulilofikiria ni hatuamoja mhimu na adhimu ya kuupiga teke umasikini na kusonga mbele zaidi.
Nakushauri usirudi nyuma mkuu mimi nipo kwenye mchakato wa kuvuta kitu kama M300 mkopo kutokana na mitiki. Je, unahisi kuna uwezekano wa kuwa masikini tena?!
Nawasikitikia sana vijana wenzangu kuendelea kutumikishwa na mkoloni na vilio visivyoisha juu ya mtaji wamesahau kuwa Bongoland full tambarareeeee!
 
sawa mkuu,shukrani sana ngoja nizitafute hizo thread ila km kuna yoyote unayoijua kwa title bac nitashkuru km ukiniekea link hapa
 
Mkuu usiwe mvivu kihivyo mkuu.
Ukisearch "mitiki" utapata kila kitu hapa jf kwenye jukwaa la ujasiriamali.
Angalia hapa; Kilimo cha mitiki: Utaalamu na biasha yenyewe.
Kisha search tena; Biashara ya upandaji wa miti ya mbao.
Pitia zote upate pa kuanzia mkuu!
 
Back
Top Bottom