Kilimo cha mpunga Tanzania

Kilimo cha mpunga Tanzania

Sehemu nyingi za morogoro huwa hawalindii ndege mashambani kwa sababu , mipunga mingi inakuwa imekwiva kwa hiyo swala la ndege linakuwa hadidhi unaweza kuta sehemu ekali zaid ya 300 kote ni mashamba ya watu ya mpunga na wote umeiva kwa pamoja sasa hapo hakuna ndege . Kuna kilimo cha kupanda umpunga ,unapanda kama unavyopanda mahindi hiki pia huongeza kipato tofauti na kilimo cha kumwaga mbegu,
 
Huu ni uzi utakaobeba mambo mengi kama sio yote kuhusiana na kilimo cha mpunga nchini Tanzania.

MPUNGA
Hili ni zao la chakula linalolimwa kwa wingi kwenye maeneo ya ukanda wa joto.

Zao hili linastawi zaidi kwenye udongo wa tifu tifu na eneo lenye maji ya kutosha. Baadhi ya maeneo (,Mikoa) yanayolima zao hili kwa wingi na kulitumia kama zao la biashara ni Morogoro,Mbeya, Tabora, singida na shinyanga.

NAMNA YA KULIMA MPUNGA
Kwa Tanzania mpunga huzalishwa kwa mifumo ya aina mbili. Yaani kumwaga/ kusia na kupandikiza miche.

1: KILIMO CHA KUMWAGA/ KUSIA
Huu ni mfumo wa kulima mpunga kwenye maeneo yenye uhaba wa maji. Katika kilimo hiki mkulima hukwatua shamba na kulitifua tifua/ kupiga piga mabonge na kuanza kumwaga mpunga katika eneo lote la shamba. Baada ya kumwaga mpunga hutifua tifua tena ili kuufukia mpunga kwenye udongo tayari kwa kuoteshwa.

Wakati mwingine kama eneo lina maji basi mkulima huloweka mbegu kwa masaa 24, huiopoa na kuivundika kwa siku tatu. Ikianza kuota basi hubebwa na kumwagwa shambani bila kufukiwa tayari kwa ukuaji. Katika umwagaji huu hatua ya kukatua na kuvuruga/ kutifua eneo haikwepeki. Baada ya kumwaga mkulima anatakiwa kuhakikisha ulinzi wa ndege unakuwepo.

Kutokana na maendeleo ya teknologia kazi zote zinzfanywa na mashine kwa wenye mitaji. Mfano kazi ya kukatua hufanywa na trekta, kazi ya kutifua / kuvuruga hufanywa na trekta na pawatila zenye rota. Vile vile kazi ya kumwaga mpunga hupandikizwa kwa kutumia mashine maalumu.

Maeneo mengi nchini hutumia mfumo huu lakini maeneo maarufu ni Morogoro na Kyela Mbeya.

GHALAMA ZA UZALISHAJI KWENYE KILIMO CHA KUMWAGA

Ghalama za kilimo hiki ni kama ifuatavyo.

a) Kukodi shamba ....... Tsh 50,000 - 100,000 kwa heka kutegemeana na location kwa Moro ni 50,000 kwa heka.

b) kukatua shamba kwa disc ....... Tsh 40,000 - 65,000.

c) kumwaga ........Tsh 30,000

d) Kung'olea/ kupalia ........Tsh 30,000- 60,000

e) kuvuna ......... Tsh 30,000 - 60,000

Ghalama nyingine ni roundup, 2-4D ambazo ni Tsh 30,000- 45,000, kufukia mpunga kwa rota 30,000 - 50,000, Mbegu debe 2-3 kwa Tsh 20,000/30,000.

Jumla ya ghalama za uzalishaji kwa kilimo cha kumwaga kwa wastani ni Tsh 200,000- 300,000.

Kipato kwa kilimo cha kumwaga wastani ni gunia 4- 8.


2: KUPANDIKIZA MICHE
Huu ni mfumo ambao hutumia mbegu iliyooteshwa kwenye vitalu katika kupandikiza mpunga. Mbegu hii huandaliwa kwa namna mbali mbali kama vile.

i) kumwaga mpunga mkavu moja kwa moja. Katika njia hii mkulima huandaa kitalu, na kumwaga mpunga alioutenga kwaajili ya mbegu. Baada ya kumwaga humwagilia maji ili mpunga upate maji tayari kwa kuota. Kitalu ili kilete manufaa inashauriwa kifunikwe kwa turubai la mifuko ya maroba au nyasi.

Kipimo kizuri cha kitaru kwa heka moja ni hatua/ mita 10× 15 na mpunga ni debe 3 kwa mpunga usio na taka taka. Ukikata kitaru cha 10×15 basi unatakiwa kugawanya Mara tatu yaani upate vitaru vya 3×10 ambavyo utamwaga debe moja la mpunga kwa kila kitaru.

ii) Kumwaga mpunga uliooteshwa
Katika mfumo huu, mbegu ya mpunga huandaliwa na kulowekwa kwa masaa 24. Baada ya kulowekwa huvundikwa kwenye mfuko au katika kifaa chenye sifa sawa na hicho kwa siku tatu na kwenda kumwaga. Kitaru kitakuwa na sifa sawa na zile za 2(i) lakini hapa lazima kiwe na unyevu wa kutosha kama sio ubichi kabisa ili mbegu isiungue. Kitaru kisiwe na maji ili kuepusha mbegu kuoza.

Kwa wanaotumia planter wao hutumia njia hii lakini wao huvundika kwenye trei au kumwaga kwenye vitalu vinavyotandikwa kitambaa au kitu mfano wa kapet maalum. Hapa sitaeleza sana maana hapa nchini ni wakulima wachache wanaotumia planters.

Kwa kawaida miche ya mbegu huwa tayari kupandikizwa baada ya siku 21 na haishauriwi kuipandikiza ikiwa na siku 45. Kuna wale watu wa shadidi mbegu zao huwa tayari kupandwa ndani ya siku 7-14.

Mfumo huu wa kuwatika mbegu unatumiwa sana maeneo mengi yanayoendesha kilimo cha umwagiliaji hasa Mbarali (Mbeya), na maeneo mengine yenye mvua za uhakika.


GHALAMA ZA UZALISHAJI KWA HEKA

a) kukodi Shamba ...... Tsh 100,000 - 300,000 kutegemeana na location

b) kukatua ....... Tsh 60,000- 70,000

c) kukata matuta ...... Tsh 15,000

d) kuvuruga/ kuchabanga .......Tsh 60,000- 70,000.

e) Kupanda ...... 60,000- 90,000

f) kungo'olea/ kupalia ...... Tsh 30,000- 45,000

g) kulinda/ kuamia ndege..... Tsh 30,000- 40,000

h) kuuvuna .....Tsh 200,000 kwa combine/ 150,000 kwa kutumia nguvu kazi.

Ghalama nyingine ni mbegu debe 3 (30,000), 2-4D (10,000-15,000), mbolea mifuko 2-4 ( 120,000- 200,000), kuandaa kitalu cha mbegu 10,000.

Jumla ya ghalama za Uzalishaji kwa heka kwa wastani ni Tsh 500,000 bila mbolea na 700,000 pamoja na mbolea

Kipato ni gunia 10 - 35 kwa heka kutegemeana na eneo na matunzo.

MATUMIZI YA CHEMIKALI KWENYE KILIMO CHA MPUNGA.

Kilimo cha mpunga hutumia chemikali za aina mbali mbali kama vile.

1. Dawa za kuunguza majani aina zote.

Hizi dawa hutumika kuangamiza majani yote shambani ili shamba likatuliwe au kuvurugwa. Dawa zinazotumika na muda wa kuisha makali shambani ni kama ifuatavyo; Round up ..... Siku 21, melaxone.... Siku 7 na chemikali nyingine zenye sifa sawa na hizo.

2: Dawa za kuua majani yenye asili ya majani mapana na ndago. Hizi hufahamika kama 2-4D, hutumika kudhoofisha na kuua kabisa magugu yasiyotakiwa kwenye mpunga. Majani yenye asili ya mpunga hayafi ndio maana inashauriwa baada ya kupiga dawa ungolee ili kuondoa magugu yasiyokufa kwa dawa. Dawa hizi zipigwe siku 21 toka siku ya kupanda mpunga na kwa wanao mwaga wapige siku 28 -30 toka siku ya kumwaga. Haishauriwi kupiga awamu mbili au zaidi kwani licha ya kuua magugu hudhoofisha mpunga.

3: Dawa za kuzuia magugu kuota.

Hizi ni dawa ambazo hupigwa siku ya tatu baada ya kupanda mpunga wakati shamba likiwa katika hali ya tope tope. Huzuia mbegu za magugu zisipasuke na kuota. Haishauriwi kupigwa kwenye mpunga wa kumwaga maana hatà mpunga hautaota . baadahi ya dawa hizo ni RILO R500, na Maguguma na dawa nyinginezo zenye sifa sawa na hizo.

4:Mbolea

Kuna aina mbali mbali za mbolea lakini kwa kifupi ni

DAP... Kupandia, hupigwa siku saba toka siku ya kupandikiza au siku ya kupandikiza.

UREA......Kukuuzia hupigwa siku 21 toka siku ya kupandikiza.

S.A ..... Mbolea ya magadi hupigwa pamoja na mbolea za kukuuzia au kuzalishia.

CAN..... mbolea ya kuzalishia hupigwa wakati mpunga umeanza kufunga(mimba)

AMIDAS..... Kukuuzia, kuondoa magadi, kuzalishia.

Utaratibu wa upigaji mbolea ni siku 14 toka mbolea ya awamu ya mwan



BIG UP SANA mkuu. Mimi ndio nimeagiza hiyo planter natumaini nitaanza kuitumia kuanzia msimu ujao. Msimu huu inachelewa kufika
 
Mpunga sikuhizi kyela hakuna kitu ns usangu wanaweka mbolea na madawa mpunga mzuri ni wa kamsamba rukwa huo ndo super kwa sasa ni mtamu na unanukia balaa na kule hawaruhusu mbolea mashambani mwao
mpunga Ni biashara, ili kuongeza kipato hakuna mpunga usiopigwa mbolea. Watu wako radhi kupiga mbolea usiku wa manane
 
Huu ni uzi utakaobeba mambo mengi kama sio yote kuhusiana na kilimo cha mpunga nchini Tanzania.

MPUNGA
Hili ni zao la chakula linalolimwa kwa wingi kwenye maeneo ya ukanda wa joto.

Zao hili linastawi zaidi kwenye udongo wa tifu tifu na eneo lenye maji ya kutosha. Baadhi ya maeneo (,Mikoa) yanayolima zao hili kwa wingi na kulitumia kama zao la biashara ni Morogoro,Mbeya, Tabora, singida na shinyanga.

NAMNA YA KULIMA MPUNGA
Kwa Tanzania mpunga huzalishwa kwa mifumo ya aina mbili. Yaani kumwaga/ kusia na kupandikiza miche.

1: KILIMO CHA KUMWAGA/ KUSIA
Huu ni mfumo wa kulima mpunga kwenye maeneo yenye uhaba wa maji. Katika kilimo hiki mkulima hukwatua shamba na kulitifua tifua/ kupiga piga mabonge na kuanza kumwaga mpunga katika eneo lote la shamba. Baada ya kumwaga mpunga hutifua tifua tena ili kuufukia mpunga kwenye udongo tayari kwa kuoteshwa.

Wakati mwingine kama eneo lina maji basi mkulima huloweka mbegu kwa masaa 24, huiopoa na kuivundika kwa siku tatu. Ikianza kuota basi hubebwa na kumwagwa shambani bila kufukiwa tayari kwa ukuaji. Katika umwagaji huu hatua ya kukatua na kuvuruga/ kutifua eneo haikwepeki. Baada ya kumwaga mkulima anatakiwa kuhakikisha ulinzi wa ndege unakuwepo.

Kutokana na maendeleo ya teknologia kazi zote zinzfanywa na mashine kwa wenye mitaji. Mfano kazi ya kukatua hufanywa na trekta, kazi ya kutifua / kuvuruga hufanywa na trekta na pawatila zenye rota. Vile vile kazi ya kumwaga mpunga hupandikizwa kwa kutumia mashine maalumu.

Maeneo mengi nchini hutumia mfumo huu lakini maeneo maarufu ni Morogoro na Kyela Mbeya.

GHALAMA ZA UZALISHAJI KWENYE KILIMO CHA KUMWAGA

Ghalama za kilimo hiki ni kama ifuatavyo.

a) Kukodi shamba ....... Tsh 50,000 - 100,000 kwa heka kutegemeana na location kwa Moro ni 50,000 kwa heka.

b) kukatua shamba kwa disc ....... Tsh 40,000 - 65,000.

c) kumwaga ........Tsh 30,000

d) Kung'olea/ kupalia ........Tsh 30,000- 60,000

e) kuvuna ......... Tsh 30,000 - 60,000

Ghalama nyingine ni roundup, 2-4D ambazo ni Tsh 30,000- 45,000, kufukia mpunga kwa rota 30,000 - 50,000, Mbegu debe 2-3 kwa Tsh 20,000/30,000.

Jumla ya ghalama za uzalishaji kwa kilimo cha kumwaga kwa wastani ni Tsh 200,000- 300,000.

Kipato kwa kilimo cha kumwaga wastani ni gunia 4- 8.


2: KUPANDIKIZA MICHE
Huu ni mfumo ambao hutumia mbegu iliyooteshwa kwenye vitalu katika kupandikiza mpunga. Mbegu hii huandaliwa kwa namna mbali mbali kama vile.

i) kumwaga mpunga mkavu moja kwa moja. Katika njia hii mkulima huandaa kitalu, na kumwaga mpunga alioutenga kwaajili ya mbegu. Baada ya kumwaga humwagilia maji ili mpunga upate maji tayari kwa kuota. Kitalu ili kilete manufaa inashauriwa kifunikwe kwa turubai la mifuko ya maroba au nyasi.

Kipimo kizuri cha kitaru kwa heka moja ni hatua/ mita 10× 15 na mpunga ni debe 3 kwa mpunga usio na taka taka. Ukikata kitaru cha 10×15 basi unatakiwa kugawanya Mara tatu yaani upate vitaru vya 3×10 ambavyo utamwaga debe moja la mpunga kwa kila kitaru.

ii) Kumwaga mpunga uliooteshwa
Katika mfumo huu, mbegu ya mpunga huandaliwa na kulowekwa kwa masaa 24. Baada ya kulowekwa huvundikwa kwenye mfuko au katika kifaa chenye sifa sawa na hicho kwa siku tatu na kwenda kumwaga. Kitaru kitakuwa na sifa sawa na zile za 2(i) lakini hapa lazima kiwe na unyevu wa kutosha kama sio ubichi kabisa ili mbegu isiungue. Kitaru kisiwe na maji ili kuepusha mbegu kuoza.

Kwa wanaotumia planter wao hutumia njia hii lakini wao huvundika kwenye trei au kumwaga kwenye vitalu vinavyotandikwa kitambaa au kitu mfano wa kapet maalum. Hapa sitaeleza sana maana hapa nchini ni wakulima wachache wanaotumia planters.

Kwa kawaida miche ya mbegu huwa tayari kupandikizwa baada ya siku 21 na haishauriwi kuipandikiza ikiwa na siku 45. Kuna wale watu wa shadidi mbegu zao huwa tayari kupandwa ndani ya siku 7-14.

Mfumo huu wa kuwatika mbegu unatumiwa sana maeneo mengi yanayoendesha kilimo cha umwagiliaji hasa Mbarali (Mbeya), na maeneo mengine yenye mvua za uhakika.


GHALAMA ZA UZALISHAJI KWA HEKA

a) kukodi Shamba ...... Tsh 100,000 - 300,000 kutegemeana na location

b) kukatua ....... Tsh 60,000- 70,000

c) kukata matuta ...... Tsh 15,000

d) kuvuruga/ kuchabanga .......Tsh 60,000- 70,000.

e) Kupanda ...... 60,000- 90,000

f) kungo'olea/ kupalia ...... Tsh 30,000- 45,000

g) kulinda/ kuamia ndege..... Tsh 30,000- 40,000

h) kuuvuna .....Tsh 200,000 kwa combine/ 150,000 kwa kutumia nguvu kazi.

Ghalama nyingine ni mbegu debe 3 (30,000), 2-4D (10,000-15,000), mbolea mifuko 2-4 ( 120,000- 200,000), kuandaa kitalu cha mbegu 10,000.

Jumla ya ghalama za Uzalishaji kwa heka kwa wastani ni Tsh 500,000 bila mbolea na 700,000 pamoja na mbolea

Kipato ni gunia 10 - 35 kwa heka kutegemeana na eneo na matunzo.

MATUMIZI YA CHEMIKALI KWENYE KILIMO CHA MPUNGA.

Kilimo cha mpunga hutumia chemikali za aina mbali mbali kama vile.

1. Dawa za kuunguza majani aina zote.

Hizi dawa hutumika kuangamiza majani yote shambani ili shamba likatuliwe au kuvurugwa. Dawa zinazotumika na muda wa kuisha makali shambani ni kama ifuatavyo; Round up ..... Siku 21, melaxone.... Siku 7 na chemikali nyingine zenye sifa sawa na hizo.

2: Dawa za kuua majani yenye asili ya majani mapana na ndago. Hizi hufahamika kama 2-4D, hutumika kudhoofisha na kuua kabisa magugu yasiyotakiwa kwenye mpunga. Majani yenye asili ya mpunga hayafi ndio maana inashauriwa baada ya kupiga dawa ungolee ili kuondoa magugu yasiyokufa kwa dawa. Dawa hizi zipigwe siku 21 toka siku ya kupanda mpunga na kwa wanao mwaga wapige siku 28 -30 toka siku ya kumwaga. Haishauriwi kupiga awamu mbili au zaidi kwani licha ya kuua magugu hudhoofisha mpunga.

3: Dawa za kuzuia magugu kuota.

Hizi ni dawa ambazo hupigwa siku ya tatu baada ya kupanda mpunga wakati shamba likiwa katika hali ya tope tope. Huzuia mbegu za magugu zisipasuke na kuota. Haishauriwi kupigwa kwenye mpunga wa kumwaga maana hatà mpunga hautaota . baadahi ya dawa hizo ni RILO R500, na Maguguma na dawa nyinginezo zenye sifa sawa na hizo.

4:Mbolea

Kuna aina mbali mbali za mbolea lakini kwa kifupi ni

DAP... Kupandia, hupigwa siku saba toka siku ya kupandikiza au siku ya kupandikiza.

UREA......Kukuuzia hupigwa siku 21 toka siku ya kupandikiza.

S.A ..... Mbolea ya magadi hupigwa pamoja na mbolea za kukuuzia au kuzalishia.

CAN..... mbolea ya kuzalishia hupigwa wakati mpunga umeanza kufunga(mimba)

AMIDAS..... Kukuuzia, kuondoa magadi, kuzalishia.

Utaratibu wa upigaji mbolea ni siku 14 toka mbolea ya awamu ya mwanzo.
Kuna kile kilimo cha umwagiliaji ambapo unaweza vuna mwezi wa tano na June ukapanda tena ukavuna November.
Nipe tofauti ya uvunaji wake .
 
Kuna kile kilimo cha umwagiliaji ambapo unaweza vuna mwezi wa tano na June ukapanda tena ukavuna November.
Nipe tofauti ya uvunaji wake .
Mavuno huwa ni kidogo Sana tofauti na kulima wakati wa mvua. Vile vile kulima Mara mbili inawezekana iwapo utakua na chanzo Cha maji Cha uhakika.
 
Huu ni uzi utakaobeba mambo mengi kama sio yote kuhusiana na kilimo cha mpunga nchini Tanzania.

MPUNGA
Hili ni zao la chakula linalolimwa kwa wingi kwenye maeneo ya ukanda wa joto.

Zao hili linastawi zaidi kwenye udongo wa tifu tifu na eneo lenye maji ya kutosha. Baadhi ya maeneo (,Mikoa) yanayolima zao hili kwa wingi na kulitumia kama zao la biashara ni Morogoro,Mbeya, Tabora, singida na shinyanga.

NAMNA YA KULIMA MPUNGA
Kwa Tanzania mpunga huzalishwa kwa mifumo ya aina mbili. Yaani kumwaga/ kusia na kupandikiza miche.

1: KILIMO CHA KUMWAGA/ KUSIA
Huu ni mfumo wa kulima mpunga kwenye maeneo yenye uhaba wa maji. Katika kilimo hiki mkulima hukwatua shamba na kulitifua tifua/ kupiga piga mabonge na kuanza kumwaga mpunga katika eneo lote la shamba. Baada ya kumwaga mpunga hutifua tifua tena ili kuufukia mpunga kwenye udongo tayari kwa kuoteshwa.

Wakati mwingine kama eneo lina maji basi mkulima huloweka mbegu kwa masaa 24, huiopoa na kuivundika kwa siku tatu. Ikianza kuota basi hubebwa na kumwagwa shambani bila kufukiwa tayari kwa ukuaji. Katika umwagaji huu hatua ya kukatua na kuvuruga/ kutifua eneo haikwepeki. Baada ya kumwaga mkulima anatakiwa kuhakikisha ulinzi wa ndege unakuwepo.

Kutokana na maendeleo ya teknologia kazi zote zinzfanywa na mashine kwa wenye mitaji. Mfano kazi ya kukatua hufanywa na trekta, kazi ya kutifua / kuvuruga hufanywa na trekta na pawatila zenye rota. Vile vile kazi ya kumwaga mpunga hupandikizwa kwa kutumia mashine maalumu.

Maeneo mengi nchini hutumia mfumo huu lakini maeneo maarufu ni Morogoro na Kyela Mbeya.

GHALAMA ZA UZALISHAJI KWENYE KILIMO CHA KUMWAGA

Ghalama za kilimo hiki ni kama ifuatavyo.

a) Kukodi shamba ....... Tsh 50,000 - 100,000 kwa heka kutegemeana na location kwa Moro ni 50,000 kwa heka.

b) kukatua shamba kwa disc ....... Tsh 40,000 - 65,000.

c) kumwaga ........Tsh 30,000

d) Kung'olea/ kupalia ........Tsh 30,000- 60,000

e) kuvuna ......... Tsh 30,000 - 60,000

Ghalama nyingine ni roundup, 2-4D ambazo ni Tsh 30,000- 45,000, kufukia mpunga kwa rota 30,000 - 50,000, Mbegu debe 2-3 kwa Tsh 20,000/30,000.

Jumla ya ghalama za uzalishaji kwa kilimo cha kumwaga kwa wastani ni Tsh 200,000- 300,000.

Kipato kwa kilimo cha kumwaga wastani ni gunia 4- 8.


2: KUPANDIKIZA MICHE
Huu ni mfumo ambao hutumia mbegu iliyooteshwa kwenye vitalu katika kupandikiza mpunga. Mbegu hii huandaliwa kwa namna mbali mbali kama vile.

i) kumwaga mpunga mkavu moja kwa moja. Katika njia hii mkulima huandaa kitalu, na kumwaga mpunga alioutenga kwaajili ya mbegu. Baada ya kumwaga humwagilia maji ili mpunga upate maji tayari kwa kuota. Kitalu ili kilete manufaa inashauriwa kifunikwe kwa turubai la mifuko ya maroba au nyasi.

Kipimo kizuri cha kitaru kwa heka moja ni hatua/ mita 10× 15 na mpunga ni debe 3 kwa mpunga usio na taka taka. Ukikata kitaru cha 10×15 basi unatakiwa kugawanya Mara tatu yaani upate vitaru vya 3×10 ambavyo utamwaga debe moja la mpunga kwa kila kitaru.

ii) Kumwaga mpunga uliooteshwa
Katika mfumo huu, mbegu ya mpunga huandaliwa na kulowekwa kwa masaa 24. Baada ya kulowekwa huvundikwa kwenye mfuko au katika kifaa chenye sifa sawa na hicho kwa siku tatu na kwenda kumwaga. Kitaru kitakuwa na sifa sawa na zile za 2(i) lakini hapa lazima kiwe na unyevu wa kutosha kama sio ubichi kabisa ili mbegu isiungue. Kitaru kisiwe na maji ili kuepusha mbegu kuoza.

Kwa wanaotumia planter wao hutumia njia hii lakini wao huvundika kwenye trei au kumwaga kwenye vitalu vinavyotandikwa kitambaa au kitu mfano wa kapet maalum. Hapa sitaeleza sana maana hapa nchini ni wakulima wachache wanaotumia planters.

Kwa kawaida miche ya mbegu huwa tayari kupandikizwa baada ya siku 21 na haishauriwi kuipandikiza ikiwa na siku 45. Kuna wale watu wa shadidi mbegu zao huwa tayari kupandwa ndani ya siku 7-14.

Mfumo huu wa kuwatika mbegu unatumiwa sana maeneo mengi yanayoendesha kilimo cha umwagiliaji hasa Mbarali (Mbeya), na maeneo mengine yenye mvua za uhakika.


GHALAMA ZA UZALISHAJI KWA HEKA

a) kukodi Shamba ...... Tsh 100,000 - 300,000 kutegemeana na location

b) kukatua ....... Tsh 60,000- 70,000

c) kukata matuta ...... Tsh 15,000

d) kuvuruga/ kuchabanga .......Tsh 60,000- 70,000.

e) Kupanda ...... 60,000- 90,000

f) kungo'olea/ kupalia ...... Tsh 30,000- 45,000

g) kulinda/ kuamia ndege..... Tsh 30,000- 40,000

h) kuuvuna .....Tsh 200,000 kwa combine/ 150,000 kwa kutumia nguvu kazi.

Ghalama nyingine ni mbegu debe 3 (30,000), 2-4D (10,000-15,000), mbolea mifuko 2-4 ( 120,000- 200,000), kuandaa kitalu cha mbegu 10,000.

Jumla ya ghalama za Uzalishaji kwa heka kwa wastani ni Tsh 500,000 bila mbolea na 700,000 pamoja na mbolea

Kipato ni gunia 10 - 35 kwa heka kutegemeana na eneo na matunzo.

MATUMIZI YA CHEMIKALI KWENYE KILIMO CHA MPUNGA.

Kilimo cha mpunga hutumia chemikali za aina mbali mbali kama vile.

1. Dawa za kuunguza majani aina zote.

Hizi dawa hutumika kuangamiza majani yote shambani ili shamba likatuliwe au kuvurugwa. Dawa zinazotumika na muda wa kuisha makali shambani ni kama ifuatavyo; Round up ..... Siku 21, melaxone.... Siku 7 na chemikali nyingine zenye sifa sawa na hizo.

2: Dawa za kuua majani yenye asili ya majani mapana na ndago. Hizi hufahamika kama 2-4D, hutumika kudhoofisha na kuua kabisa magugu yasiyotakiwa kwenye mpunga. Majani yenye asili ya mpunga hayafi ndio maana inashauriwa baada ya kupiga dawa ungolee ili kuondoa magugu yasiyokufa kwa dawa. Dawa hizi zipigwe siku 21 toka siku ya kupanda mpunga na kwa wanao mwaga wapige siku 28 -30 toka siku ya kumwaga. Haishauriwi kupiga awamu mbili au zaidi kwani licha ya kuua magugu hudhoofisha mpunga.

3: Dawa za kuzuia magugu kuota.

Hizi ni dawa ambazo hupigwa siku ya tatu baada ya kupanda mpunga wakati shamba likiwa katika hali ya tope tope. Huzuia mbegu za magugu zisipasuke na kuota. Haishauriwi kupigwa kwenye mpunga wa kumwaga maana hatà mpunga hautaota . baadahi ya dawa hizo ni RILO R500, na Maguguma na dawa nyinginezo zenye sifa sawa na hizo.

4:Mbolea

Kuna aina mbali mbali za mbolea lakini kwa kifupi ni

DAP... Kupandia, hupigwa siku saba toka siku ya kupandikiza au siku ya kupandikiza.

UREA......Kukuuzia hupigwa siku 21 toka siku ya kupandikiza.

S.A ..... Mbolea ya magadi hupigwa pamoja na mbolea za kukuuzia au kuzalishia.

CAN..... mbolea ya kuzalishia hupigwa wakati mpunga umeanza kufunga(mimba)

AMIDAS..... Kukuuzia, kuondoa magadi, kuzalishia.

Utaratibu wa upigaji mbolea ni siku 14 toka mbolea ya awamu ya mwanzo.
Asante kwa darasa🙏
Naomba kujua zaidi upandaji wa mbegu za mpunga kwa vijembe, hasa faida zake na je ni kweli kua unaongeza kipato ukilinganisha na njia nyingine??
 
Niliwahi kusikia zipo mashine unaweka shambani zinatoa mlio wa sauti ambayo hakuna ndege anayeweza kutua eneo hilo kwa mzunguko wa nusu kilomita. Mtaalam hizi mashine zipo, kama ndiyo nitazipataje na bei gani. Nataka nizifunge mwenye mashamba ya mpunga.
Maonyesho ya vyuo vikuu kuna chuo kimekuja na hiyo teknolojia
 
Naomba kuuliza ni Maeneo gani naweza kupata mashamba ya mpunga kukodi kwa bei rahisi
 
Naomba kuuliza ni Maeneo gani naweza kupata mashamba ya mpunga kukodi kwa bei rahisi
Bei rahisi ni morogoro, pwani, na Ruvuma. Uhakika zaidi ni morogoro na pwani maeneo mengine yanakumbwa na ukame wa Mara Kwa Mara hivyo Kama hakuna mfumo wa umwagiliaji kukaanga mtaji ni sekunde.
 
Asante kwa darasa[emoji120]
Naomba kujua zaidi upandaji wa mbegu za mpunga kwa vijembe, hasa faida zake na je ni kweli kua unaongeza kipato ukilinganisha na njia nyingine??
Njia pekee inayoongeza kipato ni upandaji wa mpunga Kwa kupandikiza Miche michanga(shadidi). Njia ya vijembe Sina utaalam nayo lakini naamini itakua ni mbadala wa usiaji(umwagaji ) wa mpunga. Kama itakua ni hivyo basi itakua na faida kuliko kumwaga kwani itatoa nafasi ya Miche kukua na kupacha lakini haiwezi kufikia kipato Cha upandaji wa kupandikiza Miche.
 
Njia pekee inayoongeza kipato ni upandaji wa mpunga Kwa kupandikiza Miche michanga(shadidi). Njia ya vijembe Sina utaalam nayo lakini naamini itakua ni mbadala wa usiaji(umwagaji ) wa mpunga. Kama itakua ni hivyo basi itakua na faida kuliko kumwaga kwani itatoa nafasi ya Miche kukua na kupacha lakini haiwezi kufikia kipato Cha upandaji wa kupandikiza Miche.
Mkuu je nikitaka kukodi heka 50 naweza kupata sehemu moja kwa mkoa wa morogoro?
 
Back
Top Bottom