China wanahitaji mamilioni ya tani za parachichi kwa mwaka (umesikia avocado deal waliyosaini Kenya na China)
Hapa ndio utaona uzuri wa kilimo cha matunda ya muda mrefu. Mti wa parachichi unadumu na kuvuna miaka 40+ kwahiyo hata uchumi ukiyumba miaka 7 mfululizo utavuna nakuuza kwa bei nzuri miaka ijayo. Tofauti sana na mazao ya muda mfupi kama mahindi, maharage, spices like ginger etc.
Uchumi hata ukiyumba upande wa chakula hii ni basic human need, research nyingi zina-favor avocado kutokana na health benefits zake nakufanya iwe kilimo salama zaidi.
Watu kila kukicha wanazidi kutambua umuhimu wa matunda kwa afya zao.
Idadi ya watu inazidi kuongezeka na hivyo watumiaji wa agriproducts wanazidi kuongezeka.
Dalili njema ipo hata hapa Tanzania ambapo kila mkoa, wilaya mpaka kijijini bei ya parachichi vibandani/mezani kila mwaka ni 500 iwe masika, kiangazi tofauti na embe, chungwa, pear.
Iwapo utafuata masharti ya soko la nje na kufanya organic farming, utapeta hata uchumi uyumbe vipi.