Kwanza unachagua shamba zuri lisilo na bakteria, uliza historia ya shamba.
Angalia majani yalivyoshamili au mazao yaliopo yapoje.chunguza chanzo cha maji kilipo, hakikisha maji ni ya uhakika na ya siwe ya kugombania utakula hasara.
Mbegu bora ni kala na tigo na obama ipo mbegu nyingine nyeupe ipo kama tigo ni nzuri ina zaa sana na ina wahi kukomaa.heka moja unaihitaji gunia nane.
Mbolea dap npk na can, pandia dap mfuko mmoja na nusu au miwili.can mifuko 2 na mpaka 1,weka kabla ya palizi ya pili mwagilia wiki ya kwanza kisha acha vipumue siku hata tano, rudia tena mzunguko wa kumwagia na kupumua.vikichomoza, wiki ya pili anza kutifulia, vikianza kutoa watoto chini weka mbolea can na npk wiki ya 3 mpaka ya 5, mbolea weka upande wa juu usiweke mteremkoni. Kama utawahi mwezi 5 piga dawa za ukungu na mbolea za majani busta wiki ya 1 na 2.
Baadae piga npk na utamalizia vigmax wiki tatu kabla havijakomaa kutegemea aina ya viazi usiwahi vitaoza. Kama utapanda wa sita huna haja ya dawa za ukungu. Zingatia maji ukiweza weka sprinkta tatu au mbili. Kama maji mengi tumia mpira wa nchi moja hutajuta. Usitumie wasimamizi watakudanganya na utavuna mabua.
Kazi njema karibu kwa maswali zaidi.