Kilio cha connection kwa vijana

Kilio cha connection kwa vijana

Natafuta Ajira

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2020
Posts
9,016
Reaction score
24,650
Kilio cha connection kimekua kikubwa sana huku mtaani kiasi kwamba ishaaminika ndio njia ya uhakika kupata ajira mpaka kupekelea baadhi ya watu ambao wanashikilia vitengo vizuri uko maofisini kuonekana wabaya kwa sababu hawatoi fursa za connection kwa vijana wanaotafuta ajira

Ukweli ni kwamba pamoja na kilio kikubwa cha connection ila wapo watu wengi tu wanaopata connection za kazi lakini hawazitumii vizuri, wanazichukulia poa mwishoe inapelekea kujisahau na kualibu vibarua vyao mpaka kufukuzwa kazi

Mimi nina bro alisaidiwa na sista (sio bro na sister wa tumbo moja ni tunafahamiana tu mtaani) akapata kazi benki, miezi michache baada ya kupata kazi nzuri bro alimwacha mwanamke wake wa muda mrefu aliesota nae nyakati za shida na ashazaa nae mtoto akaoa pisi kali

Ile ndoa haikwenda vizuri migogoro kila siku bro akawa mtu wa pombe sana, baadae akaja kufukuzwa kazi sababu ni ulevi na inasemakana kuna hela alipiga ofisini baada ya hapo pisi kali akamkimbia broo maana alichokifata akipo tena

Maisha yakawa magumu kwa broo na stress kibao akawa mlevi kupindukia akauza gari lake na pesa ikaishia kwenye pombe

Pisi kali akaenda kuolewa na mwanaume mwingine na kipindi anamwacha bro walikua tayari wana mtoto mchanga, mara ya mwisho bro anaonana na mwanae mtoto alikua anamwita broo anko yaan mtoto ajui kama broo ndo baba ake, hata ndugu wa broo wakiomba mtoto aje awajue ndugu zake wa upande wa baba yule pisi kali hataki kabisa.

Mwanamke wake aliezaa nae na akamwacha baada ya maisha kumnyokea alivyosikia ivyo akamsaidia broo wakarudiana akampa hifadhi kwake (huyu mwanamke sio mambo safi ni mchakalikaji wa mishe ndogo ndogo mitaani) ila broo tayari alikua addicted na pombe mpaka ikapelekea kifo chake siku alikunywa pombe kali nyingi sana alafu hajala chochote sukari ikashuka akiwa usingizini kufikia asubuhi akawa tayari ashafariki na uyo ndo mke aliemzika broo.. yule pisi kali hakutokea msibani wala hajawahi kufika kwa ndugu wa broo kutoa pole na taarifa anazo niliona post yake facebook siku broo amefariki.

Katika hali kama iyo unafikiri hata sista atakua na hamu tena ya kumsaidia mtu? Hata uko ofisini kwao akipendekeza jina ofisi ya HR hawezi kumwamini tena maana mtu wa mwisho kumleta alishafanya madudu

Fundisho kwetu job seekers wote ukipata connection ya ajira fanya kazi kwa bidii chunga mienendo yako mtaani, ukifanya vizuri wewe ndani na nje ya ofisi utatengeneza jina zuri kwa job seekers wote ambao bado tupo huku mtaani, ni kweli wapo ambao wanasaidiwa connection na kutengeneza sifa nzuri lakini kama unavyojuwa baya moja linaweza kufunika mazuri yote ila zuri moja haliwezi kufunika mabaya yote, ivyo basi ukipata connection juwa kwamba wewe ni balozi wa sisi ambao bado tupo huku mtaani tunatafuta ajira, tuwakilishe vyema.
 
Kilio cha connection kimekua kikubwa sana huku mtaani kiasi kwamba ishaaminika ndio njia ya uhakika kupata ajira mpaka kupekelea baadhi ya watu ambao wanashikilia vitengo vizuri uko maofisini kuonekana wabaya kwa sababu hawatoi fursa za connection kwa vijana wanaotafuta ajira

Ukweli ni kwamba pamoja na kilio kikubwa cha connection ila wapo watu wengi tu wanaopata connection za kazi lakini hawazitumii vizuri, wanazichukulia poa mwishoe inapelekea kujisahau na kualibu vibarua vyao mpaka kufukuzwa kazi

Mimi nina bro alisaidiwa na sista (sio bro na sister wa tumbo moja ni tunafahamiana tu mtaani) akapata kazi benki, miezi michache baada ya kupata kazi nzuri bro alimwacha mwanamke wake wa muda mrefu aliesota nae nyakati za shida na ashazaa nae mtoto akaoa pisi kali

Ile ndoa haikwenda vizuri migogoro kila siku bro akawa mtu wa pombe sana, baadae akaja kufukuzwa kazi sababu ni ulevi na inasemakana kuna hela alipiga ofisini baada ya hapo pisi kali akamkimbia broo maana alichokifata akipo tena

Maisha yakawa magumu kwa broo na stress kibao akawa mlevi kupindukia akauza gari lake na pesa ikaishia kwenye pombe

Pisi kali akaenda kuolewa na mwanaume mwingine na kipindi anamwacha bro walikua tayari wana mtoto mchanga, mara ya mwisho bro anaonana na mwanae mtoto alikua anamwita broo anko yaan mtoto ajui kama broo ndo baba ake, hata ndugu wa broo wakiomba mtoto aje awajue ndugu zake wa upande wa baba yule pisi kali hataki kabisa.

Mwanamke wake aliezaa nae na akamwacha baada ya maisha kumnyokea alivyosikia ivyo akamsaidia broo wakarudiana akampa hifadhi kwake (huyu mwanamke sio mambo safi ni mchakalikaji wa mishe ndogo ndogo mitaani) ila broo tayari alikua addicted na pombe mpaka ikapelekea kifo chake siku alikunywa pombe kali nyingi sana alafu hajala chochote sukari ikashuka akiwa usingizini kufikia asubuhi akawa tayari ashafariki na uyo ndo mke aliemzika broo.. yule pisi kali hakutokea msibani wala hajawahi kufika kwa ndugu wa broo kutoa pole na taarifa anazo niliona post yake facebook siku broo amefariki.

Katika hali kama iyo unafikiri hata sista atakua na hamu tena ya kumsaidia mtu? Hata uko ofisini kwao akipendekeza jina ofisi ya HR hawezi kumwamini tena maana mtu wa mwisho kumleta alishafanya madudu

Fundisho kwetu job seekers wote ukipata connection ya ajira fanya kazi kwa bidii chunga mienendo yako mtaani, ukifanya vizuri wewe ndani na nje ya ofisi utatengeneza jina zuri kwa job seekers wote ambao bado tupo huku mtaani, ni kweli wapo ambao wanasaidiwa connection na kutengeneza sifa nzuri lakini kama unavyojuwa baya moja linaweza kufunika mazuri yote ila zuri moja haliwezi kufunika mabaya yote, ivyo basi ukipata connection juwa kwamba wewe ni balozi wa sisi ambao bado tupo huku mtaani tunatafuta ajira, tuwakilishe vyema.
You have highlighted a good topic.

Good[emoji482]
 
Kuna konekshen imeletwa na samia leo aliniletea mkuu wa mkoa na ras wote naweza kuwaingia.

Kuanzia septemba nanyoa ndevu na nywele, pia nanunua suluari za vitambaa anavyopenda ras. Na ntashooa makahunda matano kwa ajir ya kuwapawawisha masijara waniruhusu nimsalimie na unakuwa mchezo.

Ntapga uchawa wa mwaka mzima ujao lazma michongo yangu itik kama miwili. Hadi nitajifunza kilugha cha ras.

Kufikia jun bila bila naanza kuloga.

2024 nikiwa hai lazma kuna chaka linatik na kuanza kula na wazabuni.

Ukishupaza shngo utaona wengne wanapeta.
 
Mimi nlipata rafiki yangu mlokole nkamuomba akaenda kunchukulia troo zile za ming'ao za kilokole nkanyoa low cut nkaibuka mara moja tu mahali nkaotea mchongo
 
Mimi nlipata rafiki yangu mlokole nkamuomba akaenda kunchukulia troo zile za ming'ao za kilokole nkanyoa low cut nkaibuka mara moja tu mahali nkaotea mchongo
Ongera sana mkuu, mambo yakiwa mazuri tuchekie chekie nafasi hapo., mtaani hali sio shwari
 
Umeongea kijana. Yaliyomo na unayoyajua. Nikiri tu kwamba haya mambo yapo! Ila jina lako halihitaji ujielezee sna. WANAKUJA
Nimefatilia coment zako brow tupeane conection nipo kibo still natafuta shuhuli ya kunipatia kipato niweze kuish mimi na wanaonitegemea.
 
Back
Top Bottom